samurai
JF-Expert Member
- Oct 16, 2010
- 11,495
- 24,171
Unaongea usiyoyajua. Nina uhakika uelewa wako katika mambo ya kimataifa ni duni sana au haupo kabisa.
Gadaffi alikuwa anaua kila anayehoji utawala wake. Wakati wa utawala wa Gadafi, maisha ungeyaona mazuri sana kama ukikubali kuishi kama perty animal. Ukitaka kuonesha kuwa na wewe ni binadamu, sawa na Gadati, ndiyo mwisho wako wa kuishi Duniani.
Hata wakati wa mapambano ya kuondoa utawala wa Gadafi, wapiganaji wote walipewa maelekezo ya kumkamata Gadafi, wasimjeruhi wala kumwua ili ashtakiwe, lakini yule mpiganaji ambaye hakuwahi kuwa askari alipokutana uso kwa uso na Gadafi, licha ya Gadafi kunyosha mikono ikiwa ishara ya kukubali kukamatwa, alimiminiwa risasi, na askari wengine walipofika walikuta amekwishauawa. Yule askari alikamatwa, alishtakiwa na kuhukumiwa kifo. Lakini katika maelezo yake alisema kuwa alifahamu wazi kuwa hakustahili kumwua lakini yeye aliamua kumwua kwa sababu yeye Gadafi hakuwahi kumpeleka ndugu yake mahakamani, alikamatwa alipelekwa gerezani, na usiku mmoja, yeye pamoja na wenzake waliyltolewa gerezani, wakauawa na kuzikwa kwenye kaburi moja watu 250. Alisema alijua kuwa atauawa lakini angalao ameweza kumwua mtu aliyemwua ndugu yake.
Ghadafi alikuwa mshenzi kwa watu wake hasa wabeghazi lakini pia akajifanya mjuaji kwenye maslahi ya mabeberu.... Ghadafi angesimamia vizuri maslahi ya mabeberu basi angetawala kwa amani kabisa hata kama angekuwa anaua walibya wenzake...
Saadam Iraq aliwekwa madarakani na CIA na akayasimamia vyema maslahi ya USA pamoja na kuwaua waarabu wenzie hakuna aliyemgusa, pale alipoanza kusumbua mabwana zake tu walimshukia faster....Saudia chini ya MBS inasimamia vizuri maslahi ya USA hata MBS afanye nini hakuna wakumgusa ndio maana Kashoghi amekufa kama kuku na iko wazi nani mhusika lakini kimya