Freewine
JF-Expert Member
- Jan 7, 2018
- 257
- 212
Salaam,
Hakika ujumbe huu umenichukua Kama wiki mbili kuuleta. Natumai unaenda kuanzisha harakati mpya ya ukombozi wa Tanzania.
Unajua Kama unaongozwa na chama Fulani zaidi ya miaka 50 mfululizo bila mabadiliko lipo tatizo kwenye nchi hiyo.
Turudi kwenye mada, hivi Kuna anayeweza kuamini kwamba Tundu Lissu alipigwa risasi 16 mwilini halafu akapona kifo hicho pasipo kuwepo mpango wa Mungu?
Hakika Kuna Siri ya Mungu katika ukombozi wa TL kwa kuwa Mungu ndie anaeamua Nani afe leo na Nani afe kesho. Daima Shetani mpango wake kwa wanadamu ni kuwaua tu hivyo sitegemei kwamba uponaji wa TL ni mpango wa Ibilisi.
Hivyo kwa pamoja kiimani tunaamini kwamba kupona kwa Tundu Lissu ni mpango wa Mungu
Je, unajua kwamba mpango wa Mungu huwa na kwa ajiri ya ukombozi wa watu wengi?
Tundu Lissu je unajua kwamba kupona kwako ni mpango uliopangwa na Mungu ili wewe uwe shahidi wa makuu ya Mungu kwa kusaidia watu wake?
Je, Tundu Lissu hicho unachokifanya kupita kwenye vyombo vya habari kumlaumu mheshimiwa unadhani kimetosha kuonesha ukuu wa Mungu kwa uponyaji aliokujalia?
Je, umeonesha kutangaza ukombozi wa watu wengi, una mpango?
Lakini Tundu Lissu unajua kitu kinaitwa "diminishing marginal returns?" Kwamba kadri unavyotumia/ kusikia kitu kile kile inafikia hatua unakichoka na kuunza kukipuuza?
Tazama habari zako zisije kuwa nyepesi na zile zile kuongelea upande wako tu zitasababisha upuuzwe na wazungu hao hata baadhi ya watanzania wenzako.
Usikubali kabisa kuonekana wewe ni kibaraka wa wazungu Kama ambavyo umeanza kutangaza nchini daima onekana unapigania ustawi wa watanzania umeponywa ili kulifanya hilo.
Daima wananchi wengi ni wapenzi wa nchi na viongozi wao hivyo daima mtu atakayetoa yaliyoko ndani kwake na kuyapeleka nje ataonekana msaliti wa taifa.
upuka kuonekana wewe ni msaliti wa taifa hili kwa kupinga Kila tuhuma zitazopandikizwa dhidi yako japo ulikuwa na haki ya kusema wazi wazi maumivu waliyokuletea. Najua upo kwenye chujio la moto ambalo kosa moja punishment nzito wakati kuzichanga vyema karata heshima ya kudumu katika taifa letu la Tanzania.
Hivi unajua kwamba Kuna mchakato wa katiba uliogarimu Pesa na muda mwingi wa watanzania lakini kwa hila za watu wachache umefichwa Hadi leo usionekane.
Je unajua kwamba ukipigania upatikanaji wa katiba mpya utakuwa umeleta ukombozi wa taifa hili?
Je unajua kwamba ukiwezesha suala hili utakuwa ni shujaa wa taifa hili? Kwa kupata katiba mpya Kama nchi itakuwa imejikomboa na uongozi muchungu unaoweza kukaa hata miaka Mia madarakani.
Najua utafatiliwa Sasa hivi ili kukupooza ila mapatano yako na wao yawe ni uazishaji wa kupitisha rasimu ya katiba ifike kwa wananchi na wananchi wenyewe ndo waamua either waipigie kura ya ndio au kura ya hapana.
Ukiwezesha suala hili la upatikanaji wa katiba mpya hakika utakuwa umesaidia UKOMBOZI wa taifa hili na uponyaji wa Mungu aliokujalia hautakuwa na makosa.
Hakika ujumbe huu umenichukua Kama wiki mbili kuuleta. Natumai unaenda kuanzisha harakati mpya ya ukombozi wa Tanzania.
Unajua Kama unaongozwa na chama Fulani zaidi ya miaka 50 mfululizo bila mabadiliko lipo tatizo kwenye nchi hiyo.
Turudi kwenye mada, hivi Kuna anayeweza kuamini kwamba Tundu Lissu alipigwa risasi 16 mwilini halafu akapona kifo hicho pasipo kuwepo mpango wa Mungu?
Hakika Kuna Siri ya Mungu katika ukombozi wa TL kwa kuwa Mungu ndie anaeamua Nani afe leo na Nani afe kesho. Daima Shetani mpango wake kwa wanadamu ni kuwaua tu hivyo sitegemei kwamba uponaji wa TL ni mpango wa Ibilisi.
Hivyo kwa pamoja kiimani tunaamini kwamba kupona kwa Tundu Lissu ni mpango wa Mungu
Je, unajua kwamba mpango wa Mungu huwa na kwa ajiri ya ukombozi wa watu wengi?
Tundu Lissu je unajua kwamba kupona kwako ni mpango uliopangwa na Mungu ili wewe uwe shahidi wa makuu ya Mungu kwa kusaidia watu wake?
Je, Tundu Lissu hicho unachokifanya kupita kwenye vyombo vya habari kumlaumu mheshimiwa unadhani kimetosha kuonesha ukuu wa Mungu kwa uponyaji aliokujalia?
Je, umeonesha kutangaza ukombozi wa watu wengi, una mpango?
Lakini Tundu Lissu unajua kitu kinaitwa "diminishing marginal returns?" Kwamba kadri unavyotumia/ kusikia kitu kile kile inafikia hatua unakichoka na kuunza kukipuuza?
Tazama habari zako zisije kuwa nyepesi na zile zile kuongelea upande wako tu zitasababisha upuuzwe na wazungu hao hata baadhi ya watanzania wenzako.
Usikubali kabisa kuonekana wewe ni kibaraka wa wazungu Kama ambavyo umeanza kutangaza nchini daima onekana unapigania ustawi wa watanzania umeponywa ili kulifanya hilo.
Daima wananchi wengi ni wapenzi wa nchi na viongozi wao hivyo daima mtu atakayetoa yaliyoko ndani kwake na kuyapeleka nje ataonekana msaliti wa taifa.
upuka kuonekana wewe ni msaliti wa taifa hili kwa kupinga Kila tuhuma zitazopandikizwa dhidi yako japo ulikuwa na haki ya kusema wazi wazi maumivu waliyokuletea. Najua upo kwenye chujio la moto ambalo kosa moja punishment nzito wakati kuzichanga vyema karata heshima ya kudumu katika taifa letu la Tanzania.
Hivi unajua kwamba Kuna mchakato wa katiba uliogarimu Pesa na muda mwingi wa watanzania lakini kwa hila za watu wachache umefichwa Hadi leo usionekane.
Je unajua kwamba ukipigania upatikanaji wa katiba mpya utakuwa umeleta ukombozi wa taifa hili?
Je unajua kwamba ukiwezesha suala hili utakuwa ni shujaa wa taifa hili? Kwa kupata katiba mpya Kama nchi itakuwa imejikomboa na uongozi muchungu unaoweza kukaa hata miaka Mia madarakani.
Najua utafatiliwa Sasa hivi ili kukupooza ila mapatano yako na wao yawe ni uazishaji wa kupitisha rasimu ya katiba ifike kwa wananchi na wananchi wenyewe ndo waamua either waipigie kura ya ndio au kura ya hapana.
Ukiwezesha suala hili la upatikanaji wa katiba mpya hakika utakuwa umesaidia UKOMBOZI wa taifa hili na uponyaji wa Mungu aliokujalia hautakuwa na makosa.