Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Kama Serikali ya CCM inapinga kweli ushoga basi ikafute kipengele cha Katiba kinachoinyima Serikali kuingilia faragha ya mtu

Kuhamasisha wanaume kufanya ushoga ni akili kubwa??? Dah Na wewe unashangilia kabisaaa
Katiba yetu inaruhusu mahusiano/ndoa za jinsia tofauti nenda katafute mwenyewe
Wewe kiazi kweli, niletee hapa sauti au andiko la Lissu lolote analohamasisha Wanaume kufanya ushoga




Acha Utopolo namatope kichwan... Mbuzi wee "!
 
Kumbe nimeamini kuongoza nchi hii ni rahisi sana hata chizi anaweza kuwa raisi wa tanzania! Kama mijitu inayotuongoza ndio kwanza hata katiba hawaijui alafu migumu kuelewa japo lisu anajitahd kuielewesha! Tupo pagumu sana!” Mana wanaotuongoza ni machizi.
 
sawa
images(4).jpg
 
Makamanda wanadai uhuru na haki yao yakufukuliwa tope.
Daah... Maisha yapo Kasi sanaa.
Ni baba mpumbavu pekee kama stone anayeweza kusifiwa kwa kumnunulia mkewe Iphone X lakini aliacha mwanae akafa kwa kukosa laki moja ya matibabu. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 8[1](a) inasema "Lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa (wananchi) WATU sio ustawi wa VITU. Asomaye na afahamu.!
 
Na kwani huyo Lissu ameoa jinsia Gani? Anayeshinda anatutangazia huo uchafu ndo anafanya huo uchafu kimya kimya.
 
Makonda alijitia bingwa wa kupinga ushoga lakini serikali ikamshughulikia haraka haraka akafunga domo sikumsikia mpaka leo akizungumza tena habari ya shoga!

Wakatoa na kabarua chap chap ati Tanzania inaheshimu haki za binadamu haihusiki na kupinga ushoga!

Duuhh!
Serikali ya John Pombe Magufuli inasapoti "Ushoga".
 
Si Dhani kama aliponywa na Mungu bali hirizi anazovaa! Muulize atakuambia ukweli.Maana aliyeponywa na Mungu asingesapoti ufiraji,Asingesema kitanuka asipotangazwa mshindi
Tulimwomba Mungu, na Mungu alimponya. Hata yeye anashuhudia kila mara kwamba kapona kwa Neema ya Mungu.

Kumbuka baada ya kutoka Misri kwa Mkono wa Nguvu wa Mungu, walifika njiani wakasimika ndama ya dhahabu na kuifanya kuwa ndiye Mungu aliyewatoa Misri.

Wanadamu wana tabia za kujichanganya waakti sufuri na ndiyo sababu tunatakiwa kuwa katika uwpo wa Mungu nyakati zote.
 
Nijuavyo faragha inayozungumziwa ni tendo la ndoa au mapenzi kati ya mwanaume na mwanamke.
Tendo la ndoa likifanyika faragha haina tatizo ndio mahala pake ila likifanyika hadharani ni kosa kijamii nakisheria. Ushoga ukifanyika kwa faragha ni kosa na ukifanyika hadharani ni kosa pia.
Hivyo ushoga hauna habari ya unafanyika kwenye faragha.
Hatuwezi kukaa kimya vijana wetu wakianza vitendo vya ushoga na tukajua tukasema hatuna ushahidi kwasababu wanafanyia faragha hivyo tusiwaonye.
Wanasiasa wanachofanya nikucheza na maneno tu basi ili wasiwaudhi wafadhili wao na wanaobeba ajenda zao.
Ningekua mwanasiasa au mgombea ningeupinga ushoga kwasababu Za kijamii ukiacha mambo ya Sheria n.k. wanasiasa wanaushawishi hivyo wanapaswa kutumia ushawishi wao Kueleza ubaya wa ushoga ili jamii na vijana wasijiingize huko ila unaona wanatafuta mbinu yakutolipinga suala hilo kwa kujificha mara kwenye Sheria mara kwenye haki ili tu kuwafurahisha watoa misaada.
Serikali na wanasiasa upingeni ushoga waziwazi na ielimisheni Jamii iache vitendo hivyo acheni uoga hata Kama waliowatuma nakuwapa fedha niwakali wataelewa watanzani wanamsimamo wao juu ya Hili.
Tunaupinga ushoga kama jamii sheria haziwezi kuzuia ushoga ila Jamii inaweza kuzuia, hawa wanasiasa wanawaza sheria muda wote nakutafuta matobo kwenye Sheria kuhalalisha uovu.
Ushoga haufai kuhalalishwa kwa kucheza na maneno kwa namna yeyote Ile. Siku watoto wa hao wanasiasa watakapotumbukia kwenye ushoga Ndipo watajua hiyo sio faragha ni jambo baya na linafaa kukemewa.

Sent from my Infinix X603 using JamiiForums mobile app
 
Lissu ni mgombea wa hovyo kabisa kuwahi kutolewa na upinzani
leo hii anaunga mkono katiba hiii hii kisa tu kipengele kinaunga mkono ushoga,kesho atasimama tena na kutaka katiba ya warioba
 
Mwamba kaamua kujipambanua kabisa katika mambo ya ushoga.. Ni bora kaweka wazi tumjue mapema kabisa
 
Nakujibu hivi:
Wakati walipokamatwa hadi kuhukumiwa ulifuatilia mtiririko wote au ulikuwa mtoto wakati huo?
Kwanza mimi niliweka rekodi sawa kuwa walihukumiwa kwa kubaka sio kulawiti.

Mtu yeyote akihukumiwa kwa kosa la jinai kisha akatumikia adhabu yake haendelei kuwa mhalifu wa kosa lile lile baada ya kumaliza adhabu. Hivyo Babu Seya wakati anaalikwa ikulu hakuwa mhalifu.
Wewe hapo inawezekana uliwahi kushiriki utoaji mimba ya mpenzi wako, je utoaji mimba na ubakaji lipi kosa kubwa zaidi?

Wakati wa kesi yake Kisutu, kuna mwalimu wa kike alikiri mahakamani kuwa yeye mwalimu ndiye alikuwa anawachukua hao watoto wa shule na kuwapeleka kwa babu Seya na wanawe wakafanye mapenzi lakini mwalimu huyo aliachiwa huru; sasa jiulize kwa nini huyo mwalimu hakufungwa wakati yeye ndiye mhusika namba moja? Katika akili ya kawaida tu inawezekana vipi baba na wanawe watatu wote kwa pamoja na wakati mmoja na mahali pamoja wafanye mapenzi na watoto tena katika nyumba ambayo mama yake mzazi babu Seya alikuwa akiishi hapo? Kumbuka babu Seya sio wa kizazi cha dot com.

Kwa nini mahakama ya rufaa Tanzania iliwaachilia watoto wawili wa babu Seya (nusu yao) wakati huo wameishakaa gerezani muda mrefu tu?

Kwa nini mtoto wa mwisho wa babu Seya (Francis) alihukumiwa kama mtu mzima wakati yeye wakati huo alikuwa mtoto wa miaka 17?
Ingawa ninaheshimu uamuzi wa mahakama, lakini kesi ile kuna mengi chini ya kapeti inawezekana kabisa ilitengenezwa ili kumkomoa.

NB: Mashambulizi mengi dhidi ya Rais Magufuli yanatokana na chuki binafsi kwa sababu tu ameziba mianya ya ufisadi na wizi wa fedha za umma ambazo wengi humu mlinufaika nazo aidha kwa kuiba moja kwa mija au kufaidika kupitia mnyororo wa wizi/ ufisadi baada ya wale walioiba kuja kuzitumia huku mitaani. Ndio maana hamuoni hata zuri moja alilofanya JPM.

ulisoma hukumu?
 
nmeshindwa hata kumalza kusoma hii post ya jamaa ama Kwa Hakka upuuz unao usapot my dear Friend your wrong
Mungu akusamehe bure
 
Nakujibu hivi:
Wakati walipokamatwa hadi kuhukumiwa ulifuatilia mtiririko wote au ulikuwa mtoto wakati huo?
Kwanza mimi niliweka rekodi sawa kuwa walihukumiwa kwa kubaka sio kulawiti.

Mtu yeyote akihukumiwa kwa kosa la jinai kisha akatumikia adhabu yake haendelei kuwa mhalifu wa kosa lile lile baada ya kumaliza adhabu. Hivyo Babu Seya wakati anaalikwa ikulu hakuwa mhalifu.
Wewe hapo inawezekana uliwahi kushiriki utoaji mimba ya mpenzi wako, je utoaji mimba na ubakaji lipi kosa kubwa zaidi?

Wakati wa kesi yake Kisutu, kuna mwalimu wa kike alikiri mahakamani kuwa yeye mwalimu ndiye alikuwa anawachukua hao watoto wa shule na kuwapeleka kwa babu Seya na wanawe wakafanye mapenzi lakini mwalimu huyo aliachiwa huru; sasa jiulize kwa nini huyo mwalimu hakufungwa wakati yeye ndiye mhusika namba moja? Katika akili ya kawaida tu inawezekana vipi baba na wanawe watatu wote kwa pamoja na wakati mmoja na mahali pamoja wafanye mapenzi na watoto tena katika nyumba ambayo mama yake mzazi babu Seya alikuwa akiishi hapo? Kumbuka babu Seya sio wa kizazi cha dot com.

Kwa nini mahakama ya rufaa Tanzania iliwaachilia watoto wawili wa babu Seya (nusu yao) wakati huo wameishakaa gerezani muda mrefu tu?

Kwa nini mtoto wa mwisho wa babu Seya (Francis) alihukumiwa kama mtu mzima wakati yeye wakati huo alikuwa mtoto wa miaka 17?
Ingawa ninaheshimu uamuzi wa mahakama, lakini kesi ile kuna mengi chini ya kapeti inawezekana kabisa ilitengenezwa ili kumkomoa.

NB: Mashambulizi mengi dhidi ya Rais Magufuli yanatokana na chuki binafsi kwa sababu tu ameziba mianya ya ufisadi na wizi wa fedha za umma ambazo wengi humu mlinufaika nazo aidha kwa kuiba moja kwa mija au kufaidika kupitia mnyororo wa wizi/ ufisadi baada ya wale walioiba kuja kuzitumia huku mitaani. Ndio maana hamuoni hata zuri moja alilofanya JPM.

..hayo maswali yajo nenda kawaulize mahakama ya rufaa ya Tanzania.

..hao jamaa zako walihukumiwa kwa kulawiti na kunajisi watoto wa shule.

..ukihukumiwa, ukatumikia kifungo, maana yake una rekodi ya kosa ulilolifanya.

NB:

..wewe umeona wapi mtu aliyepatikana na hatia ya kulawiti na kunajisi watoto wa shule akapata nafasi ya kupokelewa IKULU?
 
64 Reactions
Reply
Back
Top Bottom