VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Mfanyabishara maarufu nchini Tanzania na aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Manji kwasasa yuko mahabusu huku akiwa na mashtaka kadhaa mahakamani. Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA; Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa TLS naye yuko mahabusu tayari kwa kufikishwa mahakamani. Inaelezwa, uchunguzi unaendelea.
Manji alikamatwa. Akahojiwa. Akawekwa mahabusu. Akapelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kufanyiwa vipimo vya mkojo. Akafunguliwa mashtaka ya kutumia madawa kabla ya mapya ya vifaa vya kijeshi na nyaraka mbalimbali. Lissu alikamatwa. Akahojiwa. Akawekwa mahabusu. Akapelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali. Akagoma kupimwa.
Hakika, Lissu hawezi wala haitakuwa rahisi kupitishwa njia aliyopitishwa Yusuph Manji. Lissu ni 'mjanjamjanja' wa kisheria. Anajua anachokisema au anachokifanya. Anajua cha kukataa na kukubali. Anajua cha kupimwa na cha kukataa kupimwa. Anajua kutetea wengine na yeye mwenyewe mahakamani.
Kilichobaki ni kumpeleka mahakamani na kumsomea mashtaka tu kwa kile alichokuwa akishikiliwa na kuchunguzwa kwacho.
Bastola ya nini tena jamani!?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kibiti, Pwani)
Manji alikamatwa. Akahojiwa. Akawekwa mahabusu. Akapelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kufanyiwa vipimo vya mkojo. Akafunguliwa mashtaka ya kutumia madawa kabla ya mapya ya vifaa vya kijeshi na nyaraka mbalimbali. Lissu alikamatwa. Akahojiwa. Akawekwa mahabusu. Akapelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali. Akagoma kupimwa.
Hakika, Lissu hawezi wala haitakuwa rahisi kupitishwa njia aliyopitishwa Yusuph Manji. Lissu ni 'mjanjamjanja' wa kisheria. Anajua anachokisema au anachokifanya. Anajua cha kukataa na kukubali. Anajua cha kupimwa na cha kukataa kupimwa. Anajua kutetea wengine na yeye mwenyewe mahakamani.
Kilichobaki ni kumpeleka mahakamani na kumsomea mashtaka tu kwa kile alichokuwa akishikiliwa na kuchunguzwa kwacho.
Bastola ya nini tena jamani!?
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kibiti, Pwani)