Na wewe unachekesha sasa tshs 200m kwa miaka mitano unaona ni pesa ya kutatua matatizo ya jimbo? Jimbo haliwezi kuendelea kwa posho ya mbunge sahau kabisa. Wala nchi haiwezi kuendelea kwa posho za wabunge. Hizo posho kwanza wabunge wote hawastahili kulipwa kwasababu wanalipwa mishahara na kukaa mbungeni ndio kazi yao. Huwezi mlipa mfanyakazi posho kwa kufanya kazi inayomlipa mshahara. Sasa hapo ni suala la mfumo na sio issue ya mbunge mmoja mmoja kutopokea posho kwa utashi wake au kupokeaElibariki Kingu ni mbunge wa jimbo la Singida Magharibi mkoani Singida.Kutokana na upungufu wa zahanati na madawati kwenye jimbo lake ameamua kukataa posho za vikao vya bunge na kumwandikia spika azielekeze pesa hizo kwenda kutatua matatizo ya wananchi jimboni kwake singida magaribi.Jumla ya fedha za posho kwa miaka mitano ni zaidi ya millioni 200.
Jambo hili ni la kupongezwa sana kwa mbunge huyu kijana Elibariki Kingu, ameonyesha kweli anachukizwa na umasikini wa wapiga kura wake na si kupiga makelele tu with zero actions kama wabunge wengi wanavyofanya.
Tundu Lisu (chadema) ni mbunge wa mkoani singida pia na jimbo lake ni masikini kuliko majimbo yote mkoani hapa. Huduma za Maji, barabara, elimu, afya etc, ni mbovu mno jimboni kwa Lisu.
Swali kwa nini sasa Lisu asipeleke hela ya posho kutatua kero za wananchi jimboni kwake?
Pesa za posho zaidi ya million 200 unapeleka wapi na jimboni huonekani??
Kweli mbunge wa CCM Elibariki Kingu awe na uchungu kwa wananchi wake kuliko wewe Tundu Lisu mbunge wa CHADEMA?
Tundu Lissu jitafakari vinginevyo uchaguzi wa 2020 utang'oka .