Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara Ndg Tundu Lissu amesema, chama hakijapokea ruzuku yeyote toka serikalini na kama kuna mtu ana ushahidi kuwa wamepokea basi auonyeshe, kaongeza kusema, fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa ni chanzo kimoja tu cha mapato ya chama, kuna vyama havina ruzuku lakini vinaendesha shughuli zao. Chadema kina wanachama 6,700,000 hao wanachama ndio watakaoendesha shughuli za chama.
"Hatujapokea ruzuku yoyote. Katibu Mkuu wa @ChademaTz aliandikiwa barua na Msajili wa Vyama vya siasa aende kwenye mkutano wa kujadili masuala ya ruzuku. Katibu mkuu alikataa, kama wanasema tumepokea ruzuku, waoneshe ni sehemu gani tumepokea na kusaini" Ndg. @TunduALissu.
Kuhusu wanachama 19 waasi waliofukuzwa Lissu kasema, kazi ya Kamati Kuu ni kusimamia katiba na misingi ya chama na wala sio kusimamia kanuni za Bunge, kama wanakwenda bungeni sio kosa letu ni kosa la aliyewapokea.
"Kamati Kuu ya @ChademaTz imeketi na kuamua kuwa wabunge 19 ambao wameasi na kukiuka maamuzi ya chama tuliwafukuza uanachama, kwa mujibu wa katiba ya nchi yetu tangu 1965 tulipoingia rasmi katika mfumo wa chama kimoja mpaka leo, Mbunge akipoteza uanachama wa chama cha siasa anapoteza na ubunge, kama wanakwenda bungeni sio kosa letu ni kosa la wanaowapokea na kuwapa fedha za umma wakati si wabunge”.
"Ni kweli wabunge 19 tuliowafukuza wamekata rufaa. Kwenye kikao cha kamati kuu wiki iliyopita tumefanya maamuzi kuwa, kikao cha Baraza Kuu kitaitishwa kati ya mwezi Machi na Aprili, hatuwezi kuitisha kikao cha Baraza Kuu eti tu kwa ajili ya kuwasikiliza hao waasi" @TunduALissu.
"Hatujapokea ruzuku yoyote. Katibu Mkuu wa @ChademaTz aliandikiwa barua na Msajili wa Vyama vya siasa aende kwenye mkutano wa kujadili masuala ya ruzuku. Katibu mkuu alikataa, kama wanasema tumepokea ruzuku, waoneshe ni sehemu gani tumepokea na kusaini" Ndg. @TunduALissu.
Kuhusu wanachama 19 waasi waliofukuzwa Lissu kasema, kazi ya Kamati Kuu ni kusimamia katiba na misingi ya chama na wala sio kusimamia kanuni za Bunge, kama wanakwenda bungeni sio kosa letu ni kosa la aliyewapokea.
"Kamati Kuu ya @ChademaTz imeketi na kuamua kuwa wabunge 19 ambao wameasi na kukiuka maamuzi ya chama tuliwafukuza uanachama, kwa mujibu wa katiba ya nchi yetu tangu 1965 tulipoingia rasmi katika mfumo wa chama kimoja mpaka leo, Mbunge akipoteza uanachama wa chama cha siasa anapoteza na ubunge, kama wanakwenda bungeni sio kosa letu ni kosa la wanaowapokea na kuwapa fedha za umma wakati si wabunge”.
"Ni kweli wabunge 19 tuliowafukuza wamekata rufaa. Kwenye kikao cha kamati kuu wiki iliyopita tumefanya maamuzi kuwa, kikao cha Baraza Kuu kitaitishwa kati ya mwezi Machi na Aprili, hatuwezi kuitisha kikao cha Baraza Kuu eti tu kwa ajili ya kuwasikiliza hao waasi" @TunduALissu.