Tundu Lissu: CHADEMA haijahodhi mchakato wa Katiba bali inaongoza mapambano, anayetaka ajiunge nayo

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,272
47,268
Makamu Mkiti wa CHADEMA akiongea leo kwenye Forum ya Maria Space inayoongozwa na Mwanaharakati Maria Sarungi iliyoshirikisha watu zaidi ya elfu 6 duniani kote, amesema,

“Kama makundi mengine ya vyama vya kiraia, vyama vya siasa, NGOs, viongozi wa dini wanasita au wanaogopa dola kujitokeza, Chadema haitawasubiri hadi uoga wao uwaishe, Chadema itaongoza mapambano”.

Akaongeza kusema, suala la katiba ni la kila mtu kama mtu au vyama vingine vinaona katiba siyo muhimu kwao Chadema haitavilazimisha atakayeona umuhimu na aje, vyama vyenye mtazamo sawa na CCM vinaweza kuungana na CCM kupinga Katiba Mpya baadaye wananchi watakuja kulinganisha ni upande upi wenye hoja.
 
Haya ndo madhara ya mama kucheka na nyani,na bado mama asipokaza watamzingua mpaka atachutama.

Madai ya katiba mpya sio suala la mama kucheka na watu. Mama alitakiwa akamate waliojiunganishia bomba la mafuta ili kuonyesha uwezo wake maana hao ni wahalifu, sio kupambana na watu wanaodai katiba mpya kwa amani.
 
Madai ya katiba mpya sio suala la mama kucheka na watu. Mama alitakiwa akamate waliojiunganishia bomba la mafuta ili kuonyesha uwezo wake maana hao ni wahalifu, sio kupambana na watu wanaodai katiba mpya kwa amani.
Yaani Rais atoke Ikulu akakamate wezi wa mafuta? Nini kazi ya wasaidizi wake aliowateua kuanzia DC, RC, OCD, RPC, IGP, TAKUKURU? Au bado mnataka ule utawala wa oneman show? Kila kitu hata ikiwa kujenga choo cha primary school hadi Rais aende
 
Yaani Rais atoke Ikulu akakamate wezi wa mafuta? Nini kazi ya wasaidizi wake aliowateua kuanzia DC, RC, OCD, RPC, IGP, TAKUKURU? Au bado mnataka ule utawala wa oneman show? Kila kitu hata ikiwa kujenga choo cha primary school hadi Rais aende
Alipotembelea soko la Kariakoo na kutengua uongozi wake hakutokea ikulu, hakuwa rais au siku hiyo alikuwa DC wa Ilala?
 
Alipotembelea soko la Kariakoo na kutengua uongozi wake hakutokea ikulu, hakuwa rais au siku hiyo alikuwa DC wa Ilala?
Sijawahi kuona msukule wa makengeza mbowe akiwa na akili.

Chaggadema punguzeni ubinafsi, kwamba hamtaki kuzungumza na watu isipokuwa watu ndio wanapaswa kuunga mkono hatakati zenu.
 
26 Reactions
Reply
Back
Top Bottom