only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
Kufuatia kufanyiwa fujo na wale wanaosadikiwa kuwa wanachama wa CDM na kupelekea kukamatwa kwa wabunge wawili wa CDM..hatimaye leo asubuhi hapa Igunga CDM wametoa tamko kupita kwa mkurugenzi wa haki na sheria Mh.Tundu Lissu..
Akizungumza kwa hisia na kwa uchungu,Tundu amedai amesikitishwa na kitendo cha polisi kuwakamata wanachama na wabunge wawili wa CDM na kuwapeleka kituo cha polisi cha Tabora mjini badala ya kile cha Igunga ambacho ndipo walipokamatwa....Aliendelea kusema kwa siasa hizi za unyanyasaji na kamatakamata ya polisi Igunga italeteleza maafa makubwa pale wananchi wanaposhoshwa na unyanyasaji huu wa wazi....
Tundu Lissu ameomba serikali kuzingatia sheria na taratibu za uchaguzi hili kuepusha maafa yanayoweza kutokea sio Igunga tu bali hata kwa chaguzi zijazo....
Tundu alimalizia kwa kusema kwa kawaida mabadiliko yanaambatana na changamoto nyingi ambazo kama serikali ya CCM itashindwa kuhimili taifa lataelekea katika maafa makubwa kuliko kawaida....na amewashukuru wana Igunga kwa support yao kubwa wanayotoa kuleta mageuzi Tanzania...
Akizungumza kwa hisia na kwa uchungu,Tundu amedai amesikitishwa na kitendo cha polisi kuwakamata wanachama na wabunge wawili wa CDM na kuwapeleka kituo cha polisi cha Tabora mjini badala ya kile cha Igunga ambacho ndipo walipokamatwa....Aliendelea kusema kwa siasa hizi za unyanyasaji na kamatakamata ya polisi Igunga italeteleza maafa makubwa pale wananchi wanaposhoshwa na unyanyasaji huu wa wazi....
Tundu Lissu ameomba serikali kuzingatia sheria na taratibu za uchaguzi hili kuepusha maafa yanayoweza kutokea sio Igunga tu bali hata kwa chaguzi zijazo....
Tundu alimalizia kwa kusema kwa kawaida mabadiliko yanaambatana na changamoto nyingi ambazo kama serikali ya CCM itashindwa kuhimili taifa lataelekea katika maafa makubwa kuliko kawaida....na amewashukuru wana Igunga kwa support yao kubwa wanayotoa kuleta mageuzi Tanzania...