Tundu Lissu apata mapokezi ya Kifalme Kijijini kwao Singida

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Mgombea Urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu ameingia jimboni kwake Singida Mashariki na kulakiwa na umati mkubwa wa watu kuwahi kushuhudiwa katika Jimbo Hilo.

Akiwa na msafara mkubwa wa magari, pikipiki, bajaji, baiskeli na Punda kiongozi huyo kipenzi Cha Watanzania ameingia rasmi kwenye Jimbo lake la Singida Mashariki alilokuwa mbunge kwa vipindi viwili kabla hajapigwa risasi 16 mwilini mwake na watu wanaoitwa wasiojulikana.

Lissu amelakiwa na wazee, wanawake, vijana, watoto na vikongwe huku wakitandika kanga na nguo ili mwanamapinduzi huyo anayepewa nafasi kubwa ya kushinda Urais kuweza kupitia juu yake.

Screenshot_20200809-143948.png
Screenshot_20200809-144006.png
Screenshot_20200809-144027.png
IMG-20200809-WA0034.jpg

Tunaendelea kuwaletea kinachojiri. Endelea kutufuatilia.

Yaliyojiri baada ya Kuwasili Ikungi.

Hii ni historia.Hakika ndivyo tunavyoweza kusema.Kwa jinsi Lissu alivyolakiwa hapa wale waliotaka kumuua ni Kama Mungu ameshawapiga pigo Takatifu.

Mapokezi yake tumeelezwa na wazee hapa haijawahi kutokea tangia Uhuru wa Tanzania.

Watu Wazimia.

Wapo watu kadhaa ambao walizimia hususan baada ya kumuona.Wengine labda kwa sababu ya Furaha ya kumuona Tundu Lissu akitembea kwa miguu yake mwenyewe.Lakini wengine walizimia kutokana na umati mkubwa wa watu na kushindwa kuhimili.

Nyalandu aongoza mapokezi.

Kingine kilichovutia ni jinsi Mwenyekiti wa Kanda ya Kati Lazaro Nyalandu alivyoongoza mapokezi ya Lissu.Nyalandu aliapa mbele ya umma wa watu wa Singida jinsi atakavyomuunga mkono Lissu mpaka ahakikishe ameapishwa kuwa Rais wa Tanzania.

Viongozi wa Dini na Kimila

Mara baada ya Kuwasili Lissu alifanyiwa maombi maalum na viongozi wote wa kidini na wale wazee wa Jadi.

Maombi hayo ni ya Kumlinda na kumkinga maadui zake hususan wale wabaya waliokula njama na kutaka kumuua.Kwamba wale wote walioshiriki ama kujua na kushindwa kuzuia waangamie kwa uovu wao.

Pia viongozi hao walimshukuru Mungu kwa jinsi alivyomkinga Lissu dhidi ya mkono wa Ibilisi.

Lissu Azungumza.

Akizungumza na halaiki hiyo ya watu Lissu aliwashukuru kwa mapokezi makubwa aliyopata kwenye Kijiji chake Cha Ikungi alikozaliwa.

Lissu amesisitiza kampeni bado hazijaanza na akasema kilichofanyika tu ni mapokezi ya kumlaki mtoto wao aliyeponywa na Mungu kwa makusudi maalum.

Lissu amewaeleza wanakijiji wenzake kwa kirefu jinsi alivyoshambuliwa na matibabu aliyopitia mpaka kupona kwake kwa miujiza.
 

Attachments

  • VID-20200809-WA0086.mp4
    9.1 MB
Jambo jema ame return to his motherland aione hata nyumba yake, familia, majirani, wapiga kura wake, viongozi wa chama chake na wananchi wenye mapenzi mema aibu kwao waliotaka kutoa uhai wake kwamba mipango yao sio mipango ya Mungu
 
Mapokezi huwa naamini ni picha za barabarani au mtu anapowasili ila hizo picha

raia mbona wamekaa wote nadhan na mgeni rasmi kashafika meza kuu katulia

ingependeza ungetuonesha picha za mapokezi ya kifalme mithili ya yesu akiingiia yerusalem

nadhani unakumbuka ingia na mapokezi ya yesu alivyokua akiingia yerusalem,picha za namna hyo sasa.
 
Back
Top Bottom