GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Mimi ni mwana CCM, Tundu Lissu anachotufanyia sio sahihi kabisa, Sasa anatuchezesha segere ya kujibu hoja zake ambazo kwenye TV hazionyeshwi na hazijibiki.
Yale maelfu ya watu wanaomfuata wanatoka wapi?
Taarifa zake zinaenea kwa style ipi mpaka viongozi wa ccm wanazipata na kuzijibu?
William Lukuvi aliwahi kutamka kuwa Tundu lissu anatumia Ngekewa au kamzizi wakati wa Bunge la Katiba kushawishi wajumbe wamsikilize na wengi kukubaliana na hoja zake, Kauli ya lukuvi ilitokana na Tundu lissu kuwazidi kwa hoja za mambo ya muungano na uwezo wa kushawishi wajumbe
Je, kwa haya yanayoendelea kwenye kampeni kwa umati unaomfuata na kusababisha kila mtu kumfuatilia ni Ngekewa au kamzizi?
Siamini katika ndumba lakini hizi video zinajieleza
Kama watu wameamua tu kumfuata bila ndumba au kamzizi basi ccm chama changu kinapaswa kubadili mbinu
Facebook huko imewekwa hoja ya Majimbo watu wanaisifia na kuponda chama cha mapinduzi vibaya sana na hii ndio imepelekea mimi kuandika hii mada hapa JF
Nashauri chama changu mbinu ya kumaliza hizi hoja ni kutekeleza mambo yafuatayo kuelekea oktoba 2020
Mosi, Kushusha kodi ya pay as you earn kwa asilimia mbili
Pili, Kurudisha riba ya mikopo ya wanafunzi mpaka kumi asilimia au nane
Tatu, Kuwaomba radhi wale ambao bado wana hasira na chama hasa baadhi ya wafanyabiashara na wakulima
Nne, Kundi kubwa la CCM linaonyesha litapiga kura za hasira hivyo linahitaji kuwa nalo makini,Hawa wanashangilia lakini ni dhahiri watakiadhibu chama kwenye sanduku la kura,Tuwe nao watu hawa makini kwenye kampeni
Yale maelfu ya watu wanaomfuata wanatoka wapi?
Taarifa zake zinaenea kwa style ipi mpaka viongozi wa ccm wanazipata na kuzijibu?
William Lukuvi aliwahi kutamka kuwa Tundu lissu anatumia Ngekewa au kamzizi wakati wa Bunge la Katiba kushawishi wajumbe wamsikilize na wengi kukubaliana na hoja zake, Kauli ya lukuvi ilitokana na Tundu lissu kuwazidi kwa hoja za mambo ya muungano na uwezo wa kushawishi wajumbe
Je, kwa haya yanayoendelea kwenye kampeni kwa umati unaomfuata na kusababisha kila mtu kumfuatilia ni Ngekewa au kamzizi?
Siamini katika ndumba lakini hizi video zinajieleza
Kama watu wameamua tu kumfuata bila ndumba au kamzizi basi ccm chama changu kinapaswa kubadili mbinu
Facebook huko imewekwa hoja ya Majimbo watu wanaisifia na kuponda chama cha mapinduzi vibaya sana na hii ndio imepelekea mimi kuandika hii mada hapa JF
Nashauri chama changu mbinu ya kumaliza hizi hoja ni kutekeleza mambo yafuatayo kuelekea oktoba 2020
Mosi, Kushusha kodi ya pay as you earn kwa asilimia mbili
Pili, Kurudisha riba ya mikopo ya wanafunzi mpaka kumi asilimia au nane
Tatu, Kuwaomba radhi wale ambao bado wana hasira na chama hasa baadhi ya wafanyabiashara na wakulima
Nne, Kundi kubwa la CCM linaonyesha litapiga kura za hasira hivyo linahitaji kuwa nalo makini,Hawa wanashangilia lakini ni dhahiri watakiadhibu chama kwenye sanduku la kura,Tuwe nao watu hawa makini kwenye kampeni