Tundu Lissu anafaa kugombea kuwa Rais wa JMT 2020

Major

JF-Expert Member
Dec 20, 2007
1,865
2,439
Binafsi sijawahi kuwa Mwanachama wa chama Chochote Cha Siasa. Yeyote anayefanya vizuri Mimi ni Mfuasi wake kwa Maslahi ya Tanzania.

Nawashauri CHADEMA waanze kumwandaa Tundu Lisu Kuanzia Sasa ili aje kuwa Mgombea wa Uraisi 2020.Huyu ni Mwanasheria Nguli Na ni Mtu anayejitambua sana. Kwa taaluma yake ya Sheria Nina Imani ataheshimu haki za kila mtu, na ataendesha Nchi Kwa mujibu wa Taratibu tulizojiwekea.

Nasema hivi kwa sababu naliona Anguko Kubwa sana kwa Chama kilichopo Madarakani kwa sasa. Kwa kawaida hulka. Mimi ni mtu ninayependa sana ushindani, tena uwe wa aina yoyote ile.hata ktk timu za mpira Mimi sinaga ushabiki wa timu moja, kila mwaka lazima nibadidili Timu. Kitendo cha kutawaliwa na chama kimoja tangu Nizaliwe kimenichosha sana, nataka kuona watu wengine tena wakitawala, hata Kama ni Cuf au Act Au NCCR, wherever. Ninachohitaji ni Mabadiliko ya uongozi.

Hata president aliyepo sasa, angeweza kufanya makubwa zaidi ikiwa angekuwa Raisi nje Ya CCM. Hata Mzee Kingunge aliwahi kusema. CCM Kimeishiwa Pumzi. Sasa sisi tunachongangana nacho nini?!

Ifikapo Mwaka 2020, Chama hiki cha Mababu zetu, kitakuwa kimekata pumzi Kabisa, kiasi kwamba Mgombea yeyote wa upinzani akiandaliwa vizuri na mapema, njia ni nyeupe State House. Huyu Tundu Lisu anao uelewa mkubwa, Siyo mla Rushwa, ni Very Strong leader, hafanani na Dr Slaa, Lipumba,Zito na wengine wa Namna hiyo. Nina Imani huyu Lisu angekuwa mla Rushwa CCM wangeshampa kiasi chochote anachotaka. Na wanajua ktk Chama hiki kikuu cha Upinzani, ukimtoa Lisu Na mbowe, chama kimekwenda na Maji.

Natoa with kwa wapinzani Muanze kujipanga sasa hivi na hakuna sababu ya kuchelewa Mtangazeni mapema ili Kama Ana matatizo yoyote muwape Muda watu wa kumchambua mapema. God bless you Tundu Lisu
 
Hahaha hiki ni kioja cha karne, uliza kwanza Jimboni kwake Tundu alipita kwa kura ngapi, kabla ya kuleta upupu wako hapa, huyo Tundu 2020 kama akipita hata kwenye Ubunge Singida sijui!
Mtu ambaye hata anakotoka hawamtaki ndo aje kuwa Raisi JMTZ? Utamkampenia vipi Tundu kwa Watanzania, kwanza hata hatumjui, ukiondoa JF?
 
Tundu Lissu mm namfananisha na Julius Malema wa South Africa wao wanaamini ktk matumizi makubwa ya UFAHAMU kuliko AKILI

UFAHAMU= NI mkusanyiko wa ujuzi na habari ambazo mtu anaupata kupitia uzoefu
au Elimu

AKILI= Ni uwezo wa mtu kutumia maarifa vizuri(matumizi sahihi ya ufahamu)

Sasa bhasi Lissu na mwenzie Malema wanatumia Ufahamu tu si akili

Dunia ya sasa inaitaji Smart thinker si Great thinker

Great thinker ni wale wanaongonzwa na (Ufahamu)

Smart thinker ni wale wanaongozwa na( Akili )
 
Hahaha hiki ni kioja cha karne, uliza kwanza Jimboni kwake Tundu alipita kwa kura ngapi, kabla ya kuleta upupu wako hapa, huyo Tundu 2020 kama akipita hata kwenye Ubunge Singida sijui!
Mtu ambaye hata anakotoka hawamtaki ndo aje kuwa Raisi JMTZ? Utamkampenia vipi Tundu kwa Watanzania, kwanza hata hatumjui, ukiondoa JF?
Jimbo la lisu lipo vijijini lakini bado anashinda pamoja na fitina zote anazochezewa.hata hivyo lisu akienda jimbo lolote ndani ya tz ni lazima ashinde
 
Hahaha hiki ni kioja cha karne, uliza kwanza Jimboni kwake Tundu alipita kwa kura ngapi, kabla ya kuleta upupu wako hapa, huyo Tundu 2020 kama akipita hata kwenye Ubunge Singida sijui!
Mtu ambaye hata anakotoka hawamtaki ndo aje kuwa Raisi JMTZ? Utamkampenia vipi Tundu kwa Watanzania, kwanza hata hatumjui, ukiondoa JF?

Wewe mama, Tundu Lisu ameoa hataweza kukufanya mke wa pili.
 
Hahaha hiki ni kioja cha karne, uliza kwanza Jimboni kwake Tundu alipita kwa kura ngapi, kabla ya kuleta upupu wako hapa, huyo Tundu 2020 kama akipita hata kwenye Ubunge Singida sijui!
Mtu ambaye hata anakotoka hawamtaki ndo aje kuwa Raisi JMTZ? Utamkampenia vipi Tundu kwa Watanzania, kwanza hata hatumjui, ukiondoa JF?
Hivi unajua tabu za kuwa mpinzani Tz au unapanuapanua tu mdomo?

Mpinzani gani aliye tangazwa mshindi bila mshikeli?

Budget allocation tu kwa Tz ni Politically based!! T. Lissu yuko na kesi kibao kuwatetea msiojitambua kama ww!!

Hivi unadhani Tanganyika Law Society kupitisha jina la T. Lissu kuwania uenyekiti wamekosa watu?
Yule kijana ni Thinking Tanks ya Tz tukiweka siasa kando.
 
Hivi unajua tabu za kuwa mpinzani Tz au unapanuapanua tu mdomo?

Mpinzani gani aliye tangazwa mshindi bila mshikeli?

Budget allocation tu kwa Tz ni Politically based!! T. Lissu yuko na kesi kibao kuwatetea msiojitambua kama ww!!

Hivi unadhani Tanganyika Law Society kupitisha jina la T. Lissu kuwania uenyekiti wamekosa watu?
Yule kijana ni Thinking Tanks ya Tz tukiweka siasa kando.
Mkuu hii Nchi Ina mazuzu wengi sana, wanaojitambua ni wachache sana
 
Back
Top Bottom