samirnasri
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 1,388
- 213
Juzi nilikutana na rafiki yangu mmoja ambaye ni msomi wa shahada ya uzamili kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam na ni mzaliwa wa Singida Mashariki, jimbo linaloongozwa na Lissu. Tukiwa safarini tulianza kusimuliana mambo mbalimbali yaliyokuwa yamejiri bungeni jana yeke. Nilimsimulia rafiki yangu juu ya muongozo uliokuwa umeombwa na Lissu kwa spika baada ya spika kubatilisha hoja ya zitto kabla hoja hiyo haijafika mezani kwake. Nilimsifu Lissu nikasema yule jamaa ni JEMBE kweli.
Jamaa yangu aliniambia kweli Lissu ni jembe lakini haoneshi u-jembe wake jimboni kwake. Nilishtuka na kumwambia aache utani akaniambia habari ndo hiyo kwamba Lissu amekuwa moto bungeni lakini jimboni kwake ameshindwa kutimiza ahadi zake alizozitoa wakati wa kampeni. Nilimuomba anithibitishie maneno hayo kwani sikuamini kama Lissu angewasaliti wapiga kura wake. Jamaa akaniambia wakati wa kampeni Lissu aliahidi visima 12 endapo angechaguliwa kuwa mbunge na kwamba chama chake cha CHADEMA kiliahidi kumuonezea nguvu ya kujenga visima hivyo, lakini takribani miaka miwili sasa Lissu hajachimba kisima hata kimoja na kwamba wananchi wengi wamekata tamaa na wameahidi kumuhukumu katika uchaguzi mkuu ujao kama hatatimiza ahadi zake.
Zaidi ya hapo niliambiwa kitu ambacho Lissu amefanya ni kuwakingia kifua wananchi wake wasichangishwe michango mbalimbali kitu ambacho kimechangia halmashauri pia kukwamisha miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni kwake kwa madai kwamba wananchi wake hawachangii kuwezesha kukamilika kwa miradi hiyo. Kilichowaumiza na kuwasikitisha zaidi wananchi wa singida mashariki ni pale Joshua Nassari alipoanza kuchimba visima siku moja tu baada ya kutangazwa mshindi wa jimbo la arumeru mashariki.
Nilisikitika sana baada ya kusikia habari hizo kwa kuwa mimi binafsi namuamini sana Lissu na uwepo wake bungeni una mchango mkubwa sana kwa ustawi wa upinzani na kwa kuiweka serikali katika msitari mnyoofu. Nililazimika kuziamini habari hizo kwa kuwa mtoa habari ni mfuasi wa mageuzi na kwa kuwa na mimi napenda harakati za CDM katika kulikomboa taifa nimeona ni vyema niliweke suala hili jamvini ili wahusika walione na wachukuwe hatua stahiki jimbo lisije likarudi kwa chama cha magamba mwaka 2015.
Najua bado Lissu ana zaidi ya miaka miwili mbele ya kuweza kusimamia ahadi zake kwani ahadi ni deni. Wananchi wanahoji kama chadema walimwambia watamsaidia ajenge visima mbona mpaka leo hawajatimiza ahadi kama walivyofanya Arumeru mashariki? au kwa kuwa singida ni ngome ya CCM? Naomba chadema kama chama wachukuwe hatua kuhakikisha baadhi ya ahadi hizo zinatimizwa ili kulinda hadhi ya chama kuelekea mwaka 2015.
Chadema wakumbuke kwamba singida na kanda ha kati kwa ujumla imekuwa ngome ya CCM kwa miaka mingi hivyo hawapaswi kuchezea bahati waliyoipata huko singida mashariki bali wanatakiwa watumie jimbo hilo kama chachu ya kupata mjimbo mengi zaidi mwaka 2015. Singida mashariki iwe mfano kwa majimbo mengine ya ukanda huo ili wananchi washawishike kuchagua chadema katika uchaguzi ujao. Daima mtu anayekupenda atakwambia ukweli.
Nategemea michango yenye kujenga na sio kejeli wale kubeza, najua wengi tuna mapenzi binafsi na Lissu lakini kwenye ukweli lazima tuuseme kwa manufaa ya upinzani ambao naamini wengi tunaupenda.
Jamaa yangu aliniambia kweli Lissu ni jembe lakini haoneshi u-jembe wake jimboni kwake. Nilishtuka na kumwambia aache utani akaniambia habari ndo hiyo kwamba Lissu amekuwa moto bungeni lakini jimboni kwake ameshindwa kutimiza ahadi zake alizozitoa wakati wa kampeni. Nilimuomba anithibitishie maneno hayo kwani sikuamini kama Lissu angewasaliti wapiga kura wake. Jamaa akaniambia wakati wa kampeni Lissu aliahidi visima 12 endapo angechaguliwa kuwa mbunge na kwamba chama chake cha CHADEMA kiliahidi kumuonezea nguvu ya kujenga visima hivyo, lakini takribani miaka miwili sasa Lissu hajachimba kisima hata kimoja na kwamba wananchi wengi wamekata tamaa na wameahidi kumuhukumu katika uchaguzi mkuu ujao kama hatatimiza ahadi zake.
Zaidi ya hapo niliambiwa kitu ambacho Lissu amefanya ni kuwakingia kifua wananchi wake wasichangishwe michango mbalimbali kitu ambacho kimechangia halmashauri pia kukwamisha miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni kwake kwa madai kwamba wananchi wake hawachangii kuwezesha kukamilika kwa miradi hiyo. Kilichowaumiza na kuwasikitisha zaidi wananchi wa singida mashariki ni pale Joshua Nassari alipoanza kuchimba visima siku moja tu baada ya kutangazwa mshindi wa jimbo la arumeru mashariki.
Nilisikitika sana baada ya kusikia habari hizo kwa kuwa mimi binafsi namuamini sana Lissu na uwepo wake bungeni una mchango mkubwa sana kwa ustawi wa upinzani na kwa kuiweka serikali katika msitari mnyoofu. Nililazimika kuziamini habari hizo kwa kuwa mtoa habari ni mfuasi wa mageuzi na kwa kuwa na mimi napenda harakati za CDM katika kulikomboa taifa nimeona ni vyema niliweke suala hili jamvini ili wahusika walione na wachukuwe hatua stahiki jimbo lisije likarudi kwa chama cha magamba mwaka 2015.
Najua bado Lissu ana zaidi ya miaka miwili mbele ya kuweza kusimamia ahadi zake kwani ahadi ni deni. Wananchi wanahoji kama chadema walimwambia watamsaidia ajenge visima mbona mpaka leo hawajatimiza ahadi kama walivyofanya Arumeru mashariki? au kwa kuwa singida ni ngome ya CCM? Naomba chadema kama chama wachukuwe hatua kuhakikisha baadhi ya ahadi hizo zinatimizwa ili kulinda hadhi ya chama kuelekea mwaka 2015.
Chadema wakumbuke kwamba singida na kanda ha kati kwa ujumla imekuwa ngome ya CCM kwa miaka mingi hivyo hawapaswi kuchezea bahati waliyoipata huko singida mashariki bali wanatakiwa watumie jimbo hilo kama chachu ya kupata mjimbo mengi zaidi mwaka 2015. Singida mashariki iwe mfano kwa majimbo mengine ya ukanda huo ili wananchi washawishike kuchagua chadema katika uchaguzi ujao. Daima mtu anayekupenda atakwambia ukweli.
Nategemea michango yenye kujenga na sio kejeli wale kubeza, najua wengi tuna mapenzi binafsi na Lissu lakini kwenye ukweli lazima tuuseme kwa manufaa ya upinzani ambao naamini wengi tunaupenda.