Tundu Lissu ametega kitendawili cha bunge na katiba ya Jamhuri

Lissu katufungua macho,na mwenye macho haambiwi tazama!Tuchukulie mfano mdogo-kikao cha BAJETI kinajadili bajeti ya wizara isiyohusika na muungano-wanashiriki wabunge toka bara na visiwani.Kushiriki kwao kunawahalalishia kulipwa posho za ushiriki ambazo zinatokana na kodi yangu mimi na wewe mbara mwenzangu! tujiulize ushiriki wa huyu mwakilishi toka Znz una tija gani mpaka ahalalishiwe kukamua kodi yangu mie ninayeendelea kunyauka kwa ugumu wa maisha? yaani yeye akamue vikao vya bunge bara na vya uwakilishi znz kwa kodi zetu? Kuna haja ya wanajamii forum mlio na upembuzi mpana zaidi wa maswala haya mtupembulie ili wabara wengi tuone umuhimu wa kudai haki sawa ktk katiba ijayo.Kwa katiba ya sasa wabara ndo wanakamuliwa zaidi ili wa visiwani ndo mabingwa wa kulalamika kuonewa na kupunjwa! wana jf tafadhali fanyeni kazi ya ziada ya kupembua mambo bila ushabiki wa kivyama!

Hayo ndiyo tunayotaka, maana kodi zetu zinatumika hadi visiwani na pengine wengine kung'ang'ania kushika uongozi wa kamati za bunge wakati mengi yanayojadiliwa yanawahusu wabara. Wanachong'ang'ania wavisiwani ni ulaji huu tu, ebu mbara atie pua visiwani utadhani ametenda kosa la jinai wakati anatoa huduma halali.
 
Hili la visiwa vya Unguja na Pemba kwamba ni independent state halipingiki lakini not free state kwa vile wanafungwa na katiba ya Muungano katika masuala ya kimataifa. Tunachojadili hapa ni mambo yaliyomo ndani ya Muungano huu ambayo hayatendewe kwa haki, na hili la Wabunge wa visiwani kupigia kura mambo ambayo yanawahusu wabara tu ni kasoro ambayo inatakiwa kufanyiwa kazi katika katiba mpya ijayo.

Kuna ule msemo unaosema upo na sisi au haupo na sisi its as simple as that. Bunge la muungano ndio bunge kuu TZ, hapa ndio sheria zetu zinatungwa, hela inapojadiliwa in short its where the national democracy is practised. Wewe unaona sawa kweli kusema wengine wasiingie na mustakabali wao unajadiliwa pia. hivyo amna namna na wao ni kushiriki tu kwanza kuna hathari kubwa wao kutoshiriki katika hii mijada na
maslahi yao kuliko kwetu.Dawa ni simple upinzani labda uongeze wabunge huko hili wabalance lakini kuwazuia isnt an option at all.
 
Kuna ule msemo unaosema upo na sisi au haupo na sisi its as simple as that. Bunge la muungano ndio bunge kuu TZ, hapa ndio sheria zetu zinatungwa, hela inapojadiliwa in short its where the national democracy is practised. Wewe unaona sawa kweli kusema wengine wasiingie na mustakabali wao unajadiliwa pia. hivyo amna namna na wao ni kushiriki tu kwanza kuna hathari kubwa wao kutoshiriki katika hii mijada na
maslahi yao kuliko kwetu.Dawa ni simple upinzani labda uongeze wabunge huko hili wabalance lakini kuwazuia isnt an option at all.

Ni wizara chache sana ndani ya Muungano ambazo zinahusu Muungano, kwa hiyo wabunge wa visiwani wanahitajika katika mijadala hiyo na inapoisha bunge linaanza mjadala wa masuala yanayohusu Bara, vinginevyo ile ajenda ya kuwa na bunge la Tanganyika ndilo lingetoa utata huu. Na kama bunge la Tanganyika likianzishwa kutakuwa na bunge dogo sana la Muungano ambalo litahusika katika masuala ya muungano tu na hapo kuokoa pesa ambazo zinaelekewa kwa wabunge wa visiwani wanapokaa miezi miwili kujadili mambo ya wabara.
 
Ni wizara chache sana ndani ya Muungano ambazo zinahusu Muungano, kwa hiyo wabunge wa visiwani wanahitajika katika mijadala hiyo na inapoisha bunge linaanza mjadala wa masuala yanayohusu Bara, vinginevyo ile ajenda ya kuwa na bunge la Tanganyika ndilo lingetoa utata huu. Na kama bunge la Tanganyika likianzishwa kutakuwa na bunge dogo sana la Muungano ambalo litahusika katika masuala ya muungano tu na hapo kuokoa pesa ambazo zinaelekewa kwa wabunge wa visiwani wanapokaa miezi miwili kujadili mambo ya wabara.
Wao wanamawaziri wangapi na budget yao inatoka wapi na sera zao zinaelekezwa na nani kwa upande mkubwa?
 
Wao wanamawaziri wangapi na budget yao inatoka wapi na sera zao zinaelekezwa na nani kwa upande mkubwa?

Kwa nini tangu Tundu lisu apasue jipu bungeni wiki hii wabunge wa kutoka Visiwani wamekuwa wakali kutetea hoja dhidi ya Lisu, jambo ambalo ni mara ya kwanz akutokea. Kumbe wavisiwani wanalalamikia yanayowakera wao tu, na wanapogeuziwa kibao wanavyofaidi ya kutoka bara wanakuwa wakali kutetea Muungano.
 
Kwa nini tangu Tundu lisu apasue jipu bungeni wiki hii wabunge wa kutoka Visiwani wamekuwa wakali kutetea hoja dhidi ya Lisu, jambo ambalo ni mara ya kwanz akutokea. Kumbe wavisiwani wanalalamikia yanayowakera wao tu, na wanapogeuziwa kibao wanavyofaidi ya kutoka bara wanakuwa wakali kutetea Muungano.

Kuna usemi usemao "UJANJA MWINGI MBELE KIZA" Wakati ule watanganyika walitumia mivutano ya wazanzibari kuimeza zanzibar na hapo ndipo Tanganyika ilipo potezwa kwa lengo la kuifanya Tanzania kua nchi moja ambayo nikinyume na makubaliano ya muungano.

Watanganyika walizigeuza ofice zao na idara zote na kuziita za Muungano,leo wazanzibari kua kitu kimoja na kukataa kuuza nchi yao imekua shida?

Na wengine wanadhani katiba ikiundwa mpya yatamaliza
Katiba hata ikiundwa mpya haitaweza kukidhi haja kama Tanganyika haitakuapo na wizara za tanganyika zikawekwa wazi na zile za Tanzania(MUUNGANO) zikawekwa wazi.
 
Yaliyopita mpaka hapa tulipo sasa basi, ila tunataka kizazi hiki cha sasa kiridhie muungano kwa taratibu zenye maslahi kila upande bila upande mmoja kuelemewa na mzigo wa mwingine. Tunaongelea Tanzania ya leo si ya Nyerere na Karume.
 
Birth certificte ya Mtanganyika imeandikwa Jamhuri ya muungano wa Tanzania....ile ya Mzanzibari inaandikwa jamhuri ya Zanzibar!Hii tafsiri yake ni kuwa Mzanzibari sio MTANZANIA?
 
Birth certificte ya Mtanganyika imeandikwa Jamhuri ya muungano wa Tanzania....ile ya Mzanzibari inaandikwa jamhuri ya Zanzibar!Hii tafsiri yake ni kuwa Mzanzibari sio MTANZANIA?

Mzanzibari huzaliwa akiwa Mzanzibari ila anapopewa passport ndio anakua Mtanzania.
Kipo kipengele cha sheria kinachosema zanzibar ni nchi ndani ya Tanzania ila sio nchi nnje ya Tanzania.Hapa ndio maana nikakuambia hadi akipewa pass kwa matumizi ya nnje ndio huwa Mtanzania.

Pale Zenji mtu akijaza fomu yoyote inayotaka kujua uraiya huzema Mzanzibari isipokua kwenye form za kuomba pass ndio husema mtanzania,na hata vitambulisho (ID) zao hakuna neno Tanzania.
 
Birth certificte ya Mtanganyika imeandikwa Jamhuri ya muungano wa Tanzania....ile ya Mzanzibari inaandikwa jamhuri ya Zanzibar!Hii tafsiri yake ni kuwa Mzanzibari sio MTANZANIA?

Kwa hili utaambiwa mchochezi, acha kuchokonoa mambo yalivyo:peace:
 
Birth certificte ya Mtanganyika imeandikwa Jamhuri ya muungano wa Tanzania....ile ya Mzanzibari inaandikwa jamhuri ya Zanzibar!Hii tafsiri yake ni kuwa Mzanzibari sio MTANZANIA?

Mzanzibari huzaliwa akiwa Mzanzibari ila anapopewa passport ndio anakua Mtanzania.
Kipo kipengele cha sheria kinachosema zanzibar ni nchi ndani ya Tanzania ila sio nchi nnje ya Tanzania.Hapa ndio maana nikakuambia hadi akipewa pass kwa matumizi ya nnje ndio huwa Mtanzania.

Pale Zenji mtu akijaza fomu yoyote inayotaka kujua uraiya huzema Mzanzibari isipokua kwenye form za kuomba pass ndio husema mtanzania,na hata vitambulisho (ID) zao hakuna neno Tanzania.

Una maana raia wa visiwani wanaopewa passport za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni dua citizenship?
 
Lissu katufungua macho,na mwenye macho haambiwi tazama!Tuchukulie mfano mdogo-kikao cha BAJETI kinajadili bajeti ya wizara isiyohusika na muungano-wanashiriki wabunge toka bara na visiwani.Kushiriki kwao kunawahalalishia kulipwa posho za ushiriki ambazo zinatokana na kodi yangu mimi na wewe mbara mwenzangu! tujiulize ushiriki wa huyu mwakilishi toka Znz una tija gani mpaka ahalalishiwe kukamua kodi yangu mie ninayeendelea kunyauka kwa ugumu wa maisha? yaani yeye akamue vikao vya bunge bara na vya uwakilishi znz kwa kodi zetu? Kuna haja ya wanajamii forum mlio na upembuzi mpana zaidi wa maswala haya mtupembulie ili wabara wengi tuone umuhimu wa kudai haki sawa ktk katiba ijayo.Kwa katiba ya sasa wabara ndo wanakamuliwa zaidi ili wa visiwani ndo mabingwa wa kulalamika kuonewa na kupunjwa! wana jf tafadhali fanyeni kazi ya ziada ya kupembua mambo bila ushabiki wa kivyama!
Una point muhimu sana. Kwa mtu anayetaka kuelewa hili jambo vizuri ajibu swali lifuatalo. Mbunge ana kazi gani? Mbunge kazi yake kubwa ni kuwawakilisha wananchi katika kutunga sheria. Unawawakilisha wananchi waliokutuma jimboni au kama viti maalum. Sasa wabunge wa Znz wanamwakilisha nani katika mambo yasiyohusu muungano? Hawamwakilishi yeyote. Hii inakinzana kabisa na dhana ya uwakilishi. Mbunge wa znz anapojadili mambo haya ni sawa tu na wewe umeenda kuwa mbunge kenya hutakuwa umetumwa au unamwakilisha mtu yeyote.

Mfano, nilimsikia mbunge wa Znz anasema mahakama ya kadhi isipoanzishwa atahamasisha waislam waandamane. Sasa Znz wana mahakama ya kadhi? Hao waislamu waliomtuma bungeni akatetee mahakama ya kadhi ni akina nani? Znz au wana jimbo lake wana tatizo la mahakama ya kadhi?
 
Tungekuwa bold ili kupunguza matumizi, wabunge wa bara wakutane wazungumze ya bara, zanzibar wajadili ya znz. Hallafu wawe na session ya kujadili mambo ya muungano yaani mabunge haya mawili. Hivyo znz hakuna sababu ya kuwa na mbunge na mwakilishi tunaingia gharama za bure. Hata Nyerere aliliona hili katika hotunba zake alisema wanachofanya znz ni kusema changu changu chako chetu. Wabara tuamke jamani tutanyonywa hadi lini?
 
Una maana raia wa visiwani wanaopewa passport za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni dua citizenship?

Nakumbuka mara ya mwisho kuisikia hii hoja dual citizenship ilikuwa mwaka jana kwenye bunge la bajeti, iliongelewa kwa sana na bernard membe.

Nakumbuka hadi sasa tanzania hatujawa na sheria ya dual citizensship, sasa hawa wazanzibari wao tayari wana dual citizenship, wanatumia sheria gani kuhalalisha huo u-dual citizenship? just curious!
 
Birth certificte ya Mtanganyika imeandikwa Jamhuri ya muungano wa Tanzania....ile ya Mzanzibari inaandikwa jamhuri ya Zanzibar!Hii tafsiri yake ni kuwa Mzanzibari sio MTANZANIA?<br />
<br />
Mzanzibari huzaliwa akiwa Mzanzibari ila anapopewa passport ndio anakua Mtanzania.<br />
Kipo kipengele cha sheria kinachosema zanzibar ni nchi ndani ya Tanzania ila sio nchi nnje ya Tanzania.Hapa ndio maana nikakuambia hadi akipewa pass kwa matumizi ya nnje ndio huwa Mtanzania.<br />
<br />
Pale Zenji mtu akijaza fomu yoyote inayotaka kujua uraiya huzema Mzanzibari isipokua kwenye form za kuomba pass ndio husema mtanzania,na hata vitambulisho (ID) zao hakuna neno Tanzania.
<br />
<br />
Huu ni upuuzi...Muungano wa kishenzi kabisa!Yaani haya ndo walikaa na kukubaliana 1964?mbona ni utoto mtupu...yaani wenzetu visiwani wamebaki na kila kitu chao.,sisi huku ndo mazuzu kabisa!
 
Kwa hili utaambiwa mchochezi, acha kuchokonoa mambo yalivyo<img src="/images/styles/JamiiForums/smilies/peace.gif" border="0" alt="" title="Peace" smilieid="238" class="inlineimg" />
<br />
<br />
mkuu hakuna haja ya kufichaficha haya mambo tena!NAITAKA TANGANYIKA YETU.
 
Nimeona niwafafanulie tena,<br />
<br />
Katiba iliopo ni ya Jamuhuri ya muungano sasa vipi mzanzibari asishiriki mambo yote wakati yuko katika muungano?<br />
<br />
Kama itakua iko katiba ya Tanganyika Hapo haitakua haki wazanzibari kushiriki.Hii nikama ilivyo kwa zanzibar Wabara Hawawezi kushiriki kutokana na kua serekali na katiba ya zanzibar haviwahusu wabara.<br />
<br />
Sasa chakufanya nyinyi undeni katiba inayohusu Tanganyika muone kama hata nnzi kutoka zanzibar atatua hapo.<br />
<br />
alioyasema Lisu yengekua sawa kama wakati anasema hivyo iko serekali inayohusu Tanganyika tu.au katika katiba hii hii ya sasa yako mambo yalioainishwa na katiba kua haya sio ya muungano.<br />
<br />
Kwamfano katiba ya Zanzibar inatamka wazi kua ulinzi yani jeshi na polisi ni wamuungano.lakini niatamka pia mambo yasio ya muungano mfano Magereza sio wa muungano.<br />
<br />
au vyeti vyakuzaliwa vya zanzibar haviandikwi kua neno muungano lakini vyeti vya Tanzania vyote vinaandikwa ni vya jamuhuri ya muungano wa Tanzania.<br />
<br />
suali linakuja ni jambo lipi kwenu sio la muungano? Maana document za serekali zote zimeandikwa za jamuhuri ya muungano,hebu niambieni hapo utaweza vipi kumtenga mbunge kutoka zanzibar wakati nyinyi wenyewe hamuko tayari kutenganisha mambo ya muungano na yasio ya muungano?
<br />
<br />
hapo unapoint.
Na ndio sababu TL anapiga kelele na kupaza sauti ya namna tutakavyofikia win-to-win situation.
 
Tungekuwa bold ili kupunguza matumizi, wabunge wa bara wakutane wazungumze ya bara, zanzibar wajadili ya znz. Hallafu wawe na session ya kujadili mambo ya muungano yaani mabunge haya mawili. Hivyo znz hakuna sababu ya kuwa na mbunge na mwakilishi tunaingia gharama za bure. Hata Nyerere aliliona hili katika hotunba zake alisema wanachofanya znz ni kusema changu changu chako chetu. Wabara tuamke jamani tutanyonywa hadi lini?

Nakubaliana na maoni yako, sioni sababu ya utitiri wa wabunge bungeni kwa miezi karibu mitatu kujadili bajeti ya bara, huku wengine wakiwa ni wahudhuriaji ambao hawaathiriwi na bajeti hiyo wakati huo huo wakiwa wanapigia kura na kupata posho. Kwa nini kusiundwe utaratibu kama wa bunge la east afrika ambalo hujadili mambo ya jumuiya tu na ambalo lingekuwa bunge dogo tu kutokana na majumu waliyoaminishwa?
 
Nawaomba wabunge wanaokerwa na muundo wa muungano waanze kuhoji mambo haya. Kwa mfano, wa znz walioko bungeni wanakaribia mia moja. Ukiangalia posho, mishahara na mashangingi wanayochukua ni in terms of billions. Je, serikali ya smz inachangia kiasi gani katika kuendesha bunge la JMT?
 
Back
Top Bottom