Tundu Lissu alonga mambo mhimu na makubwa juu ya yaliyotokea Kenya

chuuma

JF-Expert Member
May 19, 2015
363
557
Mahakama ya Juu ya Kenya imetengua matokeo ya Uchaguzi wa Rais wa nchi hiyo na kuamuru urudiwe ndani ya siku 60.

Sisi wa CHADEMA tulimuunga mkono Uhuru Kenyatta na chama chake cha Jubilee, ambaye alitangazwa mshindi kwenye Uchaguzi huo.

Hata hivyo, uamuzi wa Supreme Court ya Kenya ni ushindi mkubwa kwa wapigania demokrasia kila mahali duniani na kwetu pia.

Uamuzi huo umetokana na Kenya kuwa na Mahakama iliyo huru na isiyokuwa na hofu, woga wala upendeleo katika utendaji wake wa haki.

Mahakama hiyo huru imetokana na Kenya kuwa na Katiba Mpya ya kidemokrasia ya mwaka 2010.

Katiba hiyo ilipunguza na au kudhibiti mamlaka ya Rais wa Kenya, na ilimaliza utawala wa kiimla uliodumu Kenya kwa karibu nusu karne.

Kwetu sisi uamuzi huu ni fundisho kubwa sana.

Tunahitaji demokrasia itakayoondoa utawala wa kidikteta katika Tanzania pia.

Tunahitaji Katiba Mpya itakayolinda haki za binadamu, kuleta utawala wa sheria na kuondoa utawala wa amri za majukwaani na bomoa bomoa.

Ili kupatikana kwa demokrasia hiyo, tunahitaji Katiba Mpya.

Katiba Mpya itakayopunguza na kudhibiti Urais wa Kifalme ambao umekuwa 'organizing principle' ya Katiba yetu tangu mwaka 1962.

Katiba Mpya itakayoiweka huru Mahakama ya Tanzania, ambayo leo haina hata Jaji Mkuu, na kuwatoa hofu majaji wetu.

Katiba Mpya itakayowawezesha watawaliwa kuwadhibiti na kuwaadabisha watawala, wanaojigeuza miungu watu mara wakishaingia madarakani.

Kwa hiyo, pamoja na kuwa urais uliotenguliwa ni wa mgombea tuliyemuunga mkono, hatuna budi kushangilia ushindi huu wa utawala wa sheria na uhuru wa mahakama.

Na, bora zaidi, hatuna budi kuyafanyia kazi mafundisho ya demokrasia ya Kenya: Katiba Mpya na ya kidemokrasia.

Katiba Mpya ya Kenya haikujileta. Ililetwa kwa jitihada, jasho na damu ya waKenya. Katiba Mpya ilipiganiwa, ilidaiwa na, baada ya kupatikana, imelindwa.

Na kwetu lazima iwe hivyo hivyo. Haitapatikana kwa kuombewa makanisani au misikitini tu. Itapatikana kwa kudaiwa mitaani na barabarani na Mahakamani na kila mahali.

Haitapatikana kwa vigelegele na vicheko. Itapatikana kwa vilio vya wanaodai haki na wanaokandamizwa.

Hebu na tujielekeze katika kazi ngumu na muhimu iliyoko mbele yetu. Kazi ya kudai Katiba Mpya.
 
Hivi Lissu sio wewe unayeshinda case mahakamani dhidi ya jamhuri kila leo? Huo sio uhuru unao ulilia?
Mbona hujasema mtazamo wako juu ya neno tume huru ya uchaguzi na maamuzi ya mahakama juu ya dosari na makosa ya IBEC ya kenya?
 
Mahakama ya Juu ya Kenya imetengua matokeo ya Uchaguzi wa Rais wa nchi hiyo na kuamuru urudiwe ndani ya siku 60.

Sisi wa CHADEMA tulimuunga mkono Uhuru Kenyatta na chama chake cha Jubilee, ambaye alitangazwa mshindi kwenye Uchaguzi huo.

Hata hivyo, uamuzi wa Supreme Court ya Kenya ni ushindi mkubwa kwa wapigania demokrasia kila mahali duniani na kwetu pia.

Uamuzi huo umetokana na Kenya kuwa na Mahakama iliyo huru na isiyokuwa na hofu, woga wala upendeleo katika utendaji wake wa haki.

Mahakama hiyo huru imetokana na Kenya kuwa na Katiba Mpya ya kidemokrasia ya mwaka 2010.

Katiba hiyo ilipunguza na au kudhibiti mamlaka ya Rais wa Kenya, na ilimaliza utawala wa kiimla uliodumu Kenya kwa karibu nusu karne.

Kwetu sisi uamuzi huu ni fundisho kubwa sana.

Tunahitaji demokrasia itakayoondoa utawala wa kidikteta katika Tanzania pia.

Tunahitaji Katiba Mpya itakayolinda haki za binadamu, kuleta utawala wa sheria na kuondoa utawala wa amri za majukwaani na bomoa bomoa.

Ili kupatikana kwa demokrasia hiyo, tunahitaji Katiba Mpya.

Katiba Mpya itakayopunguza na kudhibiti Urais wa Kifalme ambao umekuwa 'organizing principle' ya Katiba yetu tangu mwaka 1962.

Katiba Mpya itakayoiweka huru Mahakama ya Tanzania, ambayo leo haina hata Jaji Mkuu, na kuwatoa hofu majaji wetu.

Katiba Mpya itakayowawezesha watawaliwa kuwadhibiti na kuwaadabisha watawala, wanaojigeuza miungu watu mara wakishaingia madarakani.

Kwa hiyo, pamoja na kuwa urais uliotenguliwa ni wa mgombea tuliyemuunga mkono, hatuna budi kushangilia ushindi huu wa utawala wa sheria na uhuru wa mahakama.

Na, bora zaidi, hatuna budi kuyafanyia kazi mafundisho ya demokrasia ya Kenya: Katiba Mpya na ya kidemokrasia.

Katiba Mpya ya Kenya haikujileta. Ililetwa kwa jitihada, jasho na damu ya waKenya. Katiba Mpya ilipiganiwa, ilidaiwa na, baada ya kupatikana, imelindwa.

Na kwetu lazima iwe hivyo hivyo. Haitapatikana kwa kuombewa makanisani au misikitini tu. Itapatikana kwa kudaiwa mitaani na barabarani na Mahakamani na kila mahali.

Haitapatikana kwa vigelegele na vicheko. Itapatikana kwa vilio vya wanaodai haki na wanaokandamizwa.

Hebu na tujielekeze katika kazi ngumu na muhimu iliyoko mbele yetu. Kazi ya kudai Katiba Mpya.
Upepo umegeuka, kutoka kudai demokrasia na mikutano sasa wameibukia kwenye katiba. Katiba ambayo waliikimbia kuijadili au walau kuikataa bungeni wakaamua kulala mbele.. Wanataka katiba ambayo Lowassa boss wao akiwa CCM aliikataa.. Je, Lowassa ataitaka tena hiyo katiba aliyotumia gharama zake na ushawishi ndani ya CCM kuikataa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ni mpya!

Hizi hoja za kudai katiba ni upepo tu wa kisiasa kwa sababu walipiga sana kabla Lowassa hajaibuka ndani ya CHADEMA lakini alipoibuka wakaanza kusema kushinda uchaguzi sio lazima ubadilishe katiba bali ulinde kura.

Leo CHADEMA wanashangilia mahakama kumpiga stop Uhuru Kenyatta ambaye wameshirikiana naye kuharibu uchaguzi!

Viongozi wa CHADEMA wanachofanya kwa sasa ni sawa na Unapelekwa mahakamani halafu ukishindwa unaanza kushangilia! Mtu mwenye akili timamu lazima awashangae sana.

Tundu Lissu anafanya propaganda za kitoto na kijinga.

Kabla ya maamuzi ya mahakama walikuwa wanatuambia uchaguzi umefanyika katika hali huru na haki halafu leo wanatuambia tofauti ili kwenda na upepo wa kisiasa.

Nchi ya Kenya inaingia gharama nyingine ya mabilioni ya shilingi katika uchaguzi kwa sababu ya ushirikiano wa CHADEMA na Uhuru Kenyatta ambao umesababisha uchaguzi kurudiwa.

Hii inaonyesha ni jinsi gani CHADEMA na baadhi ya viongozi wake hawana msimamo dhabiti.

CHADEMA walituambia tuige mfano wa tume ya uchaguzi ya Kenya. Leo mahakama imesema tume ilisaidia ushindi feki wa Kenyatta. Kwa sasa Tundu Lissu anatuambia tena tuige Mahakama ya Kenya ! This is fun to say the least!

Siwezi kushangaa sana kwa sababu ni hawa hawa kina Tundu Lissu kwa zaidi ya miaka minane walituaminisha kuwa Lowassa ni fisadi papa na hafai hata kupewa fomu ya kugombea Urais achilia mbali kupitishwa kuwa mgombea. Kwa sasa wamekuwa wabeba mikoba ya Lowassa.

CHADEMA please! You can't have two incompatible things!

In other way, You can't have your cake and eat it!

Ama kweli, “If you don't stand for something, you will fall for anything.”
 
Tundu Lissu ....hatuhitaji elimu ya umuhimu wa katiba mpya ...tunataka tuone Chadema inao mkakati huo na jinsi mnavyoutekeleza ....tatizo lenu mnafanya siasa za matukio ....hata hili la Kenya mtalifanya kama tukio then mtaendelea na maigizo yenu ya kila siku yasiyo na tija ...
 
Back
Top Bottom