Tunaweza kuona tuna msimamo imara suala la Corona lakini mwishoni gharama yake inaweza kuwa Tanzania kukosa heshima na kupoteza urafiki na nchi jirani

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Sikatai kwa nchi hata Tanzania kutokuwa na msimamo na kukubali kuyumbishwa ndani na nje ya nchi. Ninachowaambia ni kwamba katika masuala ya mahusiano, ndani na nje ya nchi, tunapaswa tujue namna ya ku balance kati ya kuwa na msimamo, kutoyumbishwa na udiplomasia. Kuwa na msimamo haina maana kukosana na watu ndani na nje ya nchi. Huo sio msimamo, ni kujimwambafai ambako mbele ya safari matokeo yake huwa ni mabaya. Tumefikia mahali Corona inatuvuruga kisiasa ndani na nje ya nchi, ni wazi tuna tatizo na yatupasa tukiri hilo.

Angalia suala la Corona na msimamo wetu dhidi ya nchi jirani na hadi za SADC. Tumeshughulikia suala hili kama vile tuna ugomvi (confrontation) na nchi hizi na mara nyingine hili limeleta hata migongano katika ngazi za chini za madereva wetu au raia mipakani. Kuna wakati tumefanya mambo kama vile kulipiza kisasi na kusababisha migongano na uwezekano wa kukorofishana na jirani zetu kutia ndani Rwanda, Uganda, Zambia na Kenya. Pale ambapo tumealikwa na viongozi wa nchi jirani kujadili masuala ya Corona tumepuuza - kwa kuona hawana la kutuambia sisi tuna msimamo wetu juu ya jinsi tutakavyoshughulika na Corona. Hicho ni kiburi na hakitatusaidia.

Kuna mambo ambayo wala hatukuhitaji kuutangazia ulimwengu lakini tumeona sisi tunajua zaidi na kuitangazia dunia vitu kama mapapai kuonekana na Corona. Kwa nini lakini? Hata viongozi wa nchi jirani ambao inajulikana ni rafiki zetu tumeamua kuwapuuza wanapojaribu kufanya mawasiliano nasi.

Ndani ya nchi Corona imefanya tutukanane viongozi kwa viongozi, na hadi Bungeni kuanza kuitana fulani mbunge wa ovyo na hatarudi Bungeni. Imefikia tunafukuzana hata uanachama au kutumbuana kwa vikosa vidogo na kusahau mazuri watu waliyofanya huko nyuma. Kisa cha yote haya Corona tu?

NI vizuri kuwa na msimamo, lakini haina maana tuonyeshe kuwa na msimamo kwa kuharibu uhusiano na jirani zetu, au hata ndugu zetu ndani ya nchi. Tujifunze namna ya kuwa na msimamo imara lakini kuuonyesha kidiplomasia, sio kujifanya vijogoo vinavyojua kuwika na kuku wa jirani kusikia. Corona inaweza kupita, lakini hawa jirani watakuwapo siku zote. Hivyo basi tuepuke kufanya mambo kwa namna ambapo Corona inabadilisha urafiki uliopo na nchi jirani na kusababisha kutoelewana na hata uadui. Tusikubali kufanya mambo kwa namna ambayo Corona itapoteza heshima ya taifa letu hapo mbele.

Tumkumbuke Nyerere - alikuwa na misimamo mikali lakini bado alikuwa mwanadiplomasia mzuri sana, kiasi kwamba kupinga na kuzishutumu nchi kama Marekani, Uingereza, USA nk hakukusababisha tukosane nao. Aliwashutumu na bado akabaki rafiki yao sana tu na wakamheshimu sana. Awamu hii ya tano ina jambo kubwa la kujifunza kwa Nyerere kuhusiana na mahusiano na nchi na mashirika ya kimataifa, la sivyo Tanzania kama taifa na uongozi wa juu utaishia kudharauliwa na nchi, jumuia za kimataifa na viongozi wa nchi za nje.
 
Wataalamu wa afya kutoka shirika la afya duniani wanasema corona haiondoki leo wala kesho

Hao majirani zetu watajifungia mpaka December ? Km Wazungu wamefungiwa mwezi tu wameanza kuandamana

Corona ni mafua tu Sema kuna watu walijazwa uwoga na media za Mabeberu
 
Wataalamu wa afya kutoka shirika la afya duniani wanasema corona haiondoki leo wala kesho

Hao majirani zetu watajifungia mpaka December ? Km Wazungu wamefungiwa mwezi tu wameanza kuandamana

Corona ni mafua tu Sema kuna watu walijazwa uwoga na media za Mabeberu
Basi yatupasa kukumbuka kuna maisha beyond Corona!
 
Wataalamu wa afya kutoka shirika la afya duniani wanasema corona haiondoki leo wala kesho

Hao majirani zetu watajifungia mpaka December ? Km Wazungu wamefungiwa mwezi tu wameanza kuandamana

Corona ni mafua tu Sema kuna watu walijazwa uwoga na media za Mabeberu

Ni media ipi haijasema kuwa corona ni homa kali ya mfumo wa kupumua inayoweza kuua ba duniani zaidi ya watu 315,000 wamepoteza maisha???

Kubali jambo moja, kuna watu wamechagua uhai kwanza uchumi baadae, wengine uchumi kwanza na uhai baadae, na wengine wamekataa hata kukubali corona ni ugonjwa hatari kama unavosemwa. Kila nchi ilo katika moja ya makundi hayo matatu!!
 
Ni media ipi haijasema kuwa corona ni homa kali ya mfumo wa kupumua inayoweza kuua ba duniani zaidi ya watu 315,000 wamepoteza maisha???

Kubali jambo moja, kuna watu wamechagua uhai kwanza uchumi baadae, wengine uchumi kwanza na uhai baadae, na wengine wamekataa hata kukubali corona ni ugonjwa hatari kama unavosemwa. Kila nchi ilo katika moja ya makundi hayo matatu!!
Kulingana na mambo yanavyoendelea suala la uhai kwanza kukabiliana na Corona kiuchumi haliko sustainable. Kwa hiyo suala la uhai kwanza limeshapita halipo tena, kwa sasa dunia inachukua msimamo wa uchumi kwanza.

Soma hii thread;

Mtazamo mpya wa dunia kuhusu Corona ni kuwa dunia imefikia breaking point; vizuizi vitaondolewa, watakaokufa watakufa, watakaopona watapona
 
Wataalamu wa afya kutoka shirika la afya duniani wanasema corona haiondoki leo wala kesho

Hao majirani zetu watajifungia mpaka December ? Km Wazungu wamefungiwa mwezi tu wameanza kuandamana

Corona ni mafua tu Sema kuna watu walijazwa uwoga na media za Mabeberu
Hata kama gonjwa hili halitaondoka leo ama kesho, lkn isiwe sababu ya kukwepa kutambua ukubwa na uhalisia wa tatizo kwa hapa nchini. Kama nchi nyingine zinafanya jitihada za makusudi ili kupambana na maambukizi mapya, ni lazima na sisi pia tuonyeshe jitihada kama hizo zenye mashiko ya kisayansi.

Wanasiasa wakwepe kuwavunja moyo na kuwakatisha tamaa wataalamu mbalimbali wa afya. Nasema hivyo kwa kuwa tumeshuhudia wenye mamlaka wakija na "promo" za nguvu za tiba mbadala, huku pia wakitoa kasoro, kubeza na hata kuelezea hadharani mashaka yao juu ya "efficacy of previous laboratory tests" na hatimaye vipimo vikaacha kufanyika na "updates" ya visa vipya kuacha kutolewa.

Ni mapema sana kuanza kuchukulia poa gonjwa hili. Sijui huu ujasiri wa viongozi wetu kutaka kutangaza ushindi dhidi yake hata unatoka wapi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sikatai kwa nchi hata Tanzania kutokuwa na msimamo na kukubali kuyumbishwa ndani na nje ya nchi. Ninachowaambia ni kwamba katika masuala ya mahusiano, ndani na nje ya nchi, tunapaswa tujue namna ya ku balance kati ya kuwa na msimamo, kutoyumbishwa na udiplomasia. Kuwa na msimamo haina maana kukosana na watu ndani na nje ya nchi. Huo sio msimamo, ni kujimwambafai ambako mbele ya safari matokeo yake huwa ni mabaya. Tumefikia mahali Corona inatuvuruga kisiasa ndani na nje ya nchi, ni wazi tuna tatizo na yatupasa tukiri hilo.

Angalia suala la Corona na msimamo wetu dhidi ya nchi jirani na hadi za SADC. Tumeshughulikia suala hili kama vile tuna ugomvi (confrontation) na nchi hizi na mara nyingine hili limeleta hata migongano katika ngazi za chini za madereva wetu au raia mipakani. Kuna wakati tumefanya mambo kama vile kulipiza kisasi na kusababisha migongano na uwezekano wa kukorofishana na jirani zetu kutia ndani Rwanda, Uganda, Zambia na Kenya. Pale ambapo tumealikwa na viongozi wa nchi jirani kujadili masuala ya Corona tumepuuza - kwa kuona hawana la kutuambia sisi tuna msimamo wetu juu ya jinsi tutakavyoshughulika na Corona. Hicho ni kiburi na hakitatusaidia.

Kuna mambo ambayo wala hatukuhitaji kuutangazia ulimwengu lakini tumeona sisi tunajua zaidi na kuitangazia dunia vitu kama mapapai kuonekana na Corona. Kwa nini lakini? Hata viongozi wa nchi jirani ambao inajulikana ni rafiki zetu tumeamua kuwapuuza wanapojaribu kufanya mawasiliano nasi.

Ndani ya nchi Corona imefanya tutukanane viongozi kwa viongozi, na hadi Bungeni kuanza kuitana fulani mbunge wa ovyo na hatarudi Bungeni. Imefikia tunafukuzana hata uanachama au kutumbuana kwa vikosa vidogo na kusahau mazuri watu waliyofanya huko nyuma. Kisa cha yote haya Corona tu?

NI vizuri kuwa na msimamo, lakini haina maana tuonyeshe kuwa na msimamo kwa kuharibu uhusiano na jirani zetu, au hata ndugu zetu ndani ya nchi. Tujifunze namna ya kuwa na msimamo imara lakini kuuonyesha kidiplomasia, sio kujifanya vijogoo vinavyojua kuwika na kuku wa jirani kusikia. Corona inaweza kupita, lakini hawa jirani watakuwapo siku zote. Hivyo basi tuepuke kufanya mambo kwa namna ambapo Corona inabadilisha urafiki uliopo na nchi jirani na kusababisha kutoelewana na hata uadui. Tusikubali kufanya mambo kwa namna ambayo Corona itapoteza heshima ya taifa letu hapo mbele.
Corona kwa Afrika imeshindwa ,labda watengeneze formula kwa upya kwa ajili ya Afrka tu,kwa jinsi inavyouwa na matarajio yao imekua tofauti kabisa .
Waangalie wajerumani wanavyosema kuhusu covid 19

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Corona itapoteza heshima ya taifa letu hapo mbele.

The hell with "heshima ya taifa letu"

Unyoronyoro hauwezi kukupa heshime ever

Misimamo ilifanya Tanzania ya Nyerere ikaheshimika

Sycophantic foreign relations of Membe and Kikwete out the window!
 
Hata kama gonjwa hili halitaondoka leo ama kesho, lkn isiwe sababu ya kukwepa kutambua ukubwa na uhalisia wa tatizo kwa hapa nchini. Kama nchi nyingine zinafanya jitihada za makusudi ili kupambana na maambukizi mapya, ni lazima na sisi pia tuonyeshe jitihada kama hizo zenye mashiko ya kisayansi.

Wanasiasa wakwepe kuwavunja moyo na kuwakatisha tamaa wataalamu mbalimbali wa afya. Nasema hivyo kwa kuwa tumeshuhudia wenye mamlaka wakija na "promo" za nguvu za tiba mbadala, huku pia wakitoa kasoro, kubeza na hata kuelezea hadharani mashaka yao juu ya "efficacy of previous laboratory tests" na hatimaye vipimo vikaacha kufanyika na "updates" ya visa vipya kuacha kutolewa.

Ni mapema sana kuanza kuchukulia poa gonjwa hili. Sijui huu ujasiri wa viongozi wetu kutaka kutangaza ushindi dhidi yake hata unatoka wapi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Well said

MÊmENtO HoMO
 
Corona kwa Afrika imeshindwa ,labda watengeneze formula kwa upya kwa ajili ya Afrka tu,kwa jinsi inavyouwa na matarajio yao imekua tofauti kabisa .
Waangalie wajerumani wanavyosema kuhusu covid 19

Sent using Jamii Forums mobile app
Naona kama mada ni kumaintain diplomacy hata kama mitazamo yetu ni tofauti kuhusu Covid-19, na sio kuonesha umwamba na kiburi.

Tunaomba mada irudi kwenye reli tafadhali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
The hell with "heshima ya taifa letu"

Unyoronyoro hauwezi kukupa heshime ever

Misimamo ilifanya Tanzania ya Nyerere ikaheshimika

Sycophantic foreign relations of Membe and Kikwete out the window!
Tofauti na sasa, Nyerere alikuwa na msimamo na udiplomasia - aliwasimanga Waingereza na Marekani na bado akawa kipenzi chao!

Alivunja uhusiano na Uingereza na West Germany - na bado wakamfuata kuomba urudishwe.

Hebu iambie awamu ya tano leo hii iseme inavunja uhusiano na Marekani uone kama watatufuata kutubembeleza tuurudishe!
 
Wataalamu wa afya kutoka shirika la afya duniani wanasema corona haiondoki leo wala kesho

Hao majirani zetu watajifungia mpaka December ? Km Wazungu wamefungiwa mwezi tu wameanza kuandamana

Corona ni mafua tu Sema kuna watu walijazwa uwoga na media za Mabeberu
Yaani nikisomaga thread nikakuta comment yako Basi huwa sikomenti najua unaletaga siasa kwenye mambo ya msingi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom