Tunawashukuru sana Marekani kwa kukikata meno kikosi cha Wasiojulikana!

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Marekani walijua kabisa kwamba kulikuwa na kikosi kilichobatizwa jina la "Wasiojulikana" hapa nchini, kikosi ambacho kilijikita katika kuteka watu na hata kuua. Na Marekani waliona wazi kwamba wahanga wa kikosi hiki cha Wasiojulikana walikuwa ni kutoka vyama vya upinzani pamoja na waandishi wa habari na wananchi kwa ujumla walioikosoa serikali. Pia kulikuwa na wafanya biashara wakubwa ambao walionekana kutenda kinyume na matakwa ya serikali,

Na jambo jingine Marekani waliloona wazi ni kwamba siku zote Polisi hawakuonyesha nia ya dhati ya kushughulikia na kupepeleza kesi au matukio yaliyofanywa na hiki kikosi cha Wasiojulikana. Mara nyingone Polisi walitoa matamko ya kuwalaghai na kuwapoteza lengo wananchi pale ilipohusu matukio ya Wasiojulikana.

Ndipo Marekani wakaamua kuingilia na kuwaokoa watanzania walioendelea kuwa wahanga wa kikosi hiki cha Wasiojulikana. Wakatuma ujumbe. Wakatoa onyo.

Tunawashukuru sana Marekani kwa jambo hili. Ni wazi kuingilia kwenu kumeokoa maisha ya Watanzania wengi na kutoa ahueni kubwa. Tunajua watu wegi walikuwa kwenye "hit list" ya hiki kikosi cha Wasiojulikana na kama sio kuingilia kwenu wengi wangeumizwa au kutoweshwa. Lakini bado tunaomba mwende mbali zaidi na kufunua wazi nani waliohusika na kikosi cha Wasiojulikana, na kiliundwa kwa amri ya nani. Damu za waliopota zinatulilia tuwafanyie hilo.
 
Marekani walijua kabisa kwamba kulikuwa na kikosi kilichobatizwa jina la "Wasiojulikana" hapa nchini, kikosi ambacho kilijikita katika kuteka watu na hata kuua. Na Marekani waliona wazi kwamba wahanga wa kikosi hiki cha Wasiojulikana walikuwa ni kutoka vyama vya upinzani pamoja na waandishi na wananchi kwa ujumla walioikosoa serikali. Pia kulikuwa na wafanya biashara wakubwa ambao walionekana kutenda kinyume na matakwa ya serikali,

Na jambo jingine Marekani waliloona wazi ni kwamba siku zote Polisi hawakuonyesha nia ya dhati ya kushughulikia na kupepeleza kesi au matukio yaliyofanywa na hiki kikosi cha Wasiojulikana. Mara nyingone POlisi walitoa matamko ya kuwalaghai wanachi pale ilipohusu matukio ya Wasiojulikana.

Ndipo Marekani wakaamua kuingilia na kuwaokoa watanzania walioendelea kuwa wahanga wa kikosi hiki cha Wasiojulikana. Wakatuma ujumbe. Wakatoa onyo.

Tunawashukuru sana Marekani kwa jambo hili. Ni wazi kuingilia kwenu kumeokoa maisha ya Watanzania wengi na kutoa ahueni kubwa. Tunajua watu wegi walikuwa kwenye "hit list" ya hiki kikosi cha Wasiojulikana na kama sio kuingilia kwenu wengi wangeumizwa au kutoweshwa. Lakini bado tunaomba mwende mbali zaidi na kufunua wazi nani waliohusika na kikosi cha Wasiojulikana, na kiliundwa kwa amri ya nani. Damu za waliopota zinatulilia tuwafanyie hilo.
Mbona hujaongelea waliokuwa wanavamia misafara ya askari wetu na kuwapora silaha na kuwahua? Mbona ujaongelea genge LA wezi na majambazi wa kuvamia mabenk? Sasa hivi wapo?
 
Pompeo lile linakasrika mashoga yakiguswa halijui chochote kuhusu mambo mengine

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa hili hilo li "Pompeo" limewafyata mkia barabara. Hamna hata fyoo. kujibu. Halafu kama hujagundua, hadi wakuu wamekuwa wapole siku hizi.

Cha kucheesha ni kwamba siku hizi serikali inakimbia kujieleza kwa Marekani hata kabla hawajaulizwa! Unacheza na Pompeo wewe!
 
Marekani walijua kabisa kwamba kulikuwa na kikosi kilichobatizwa jina la "Wasiojulikana" hapa nchini, kikosi ambacho kilijikita katika kuteka watu na hata kuua. Na Marekani waliona wazi kwamba wahanga wa kikosi hiki cha Wasiojulikana walikuwa ni kutoka vyama vya upinzani pamoja na waandishi na wananchi kwa ujumla walioikosoa serikali. Pia kulikuwa na wafanya biashara wakubwa ambao walionekana kutenda kinyume na matakwa ya serikali,

Na jambo jingine Marekani waliloona wazi ni kwamba siku zote Polisi hawakuonyesha nia ya dhati ya kushughulikia na kupepeleza kesi au matukio yaliyofanywa na hiki kikosi cha Wasiojulikana. Mara nyingone Polisi walitoa matamko ya kuwalaghai na kuwapoteza lengo wananchi pale ilipohusu matukio ya Wasiojulikana.

Ndipo Marekani wakaamua kuingilia na kuwaokoa watanzania walioendelea kuwa wahanga wa kikosi hiki cha Wasiojulikana. Wakatuma ujumbe. Wakatoa onyo.

Tunawashukuru sana Marekani kwa jambo hili. Ni wazi kuingilia kwenu kumeokoa maisha ya Watanzania wengi na kutoa ahueni kubwa. Tunajua watu wegi walikuwa kwenye "hit list" ya hiki kikosi cha Wasiojulikana na kama sio kuingilia kwenu wengi wangeumizwa au kutoweshwa. Lakini bado tunaomba mwende mbali zaidi na kufunua wazi nani waliohusika na kikosi cha Wasiojulikana, na kiliundwa kwa amri ya nani. Damu za waliopota zinatulilia tuwafanyie hilo.
Hapo unapoandika nahakika kuna watu wanajua upo wapi na upuuzi wako wanakucheki tu. Ila kwa uungwana tu wanaamua kukuacha.Maana hata wakidili na wewe ni kupoteza muda.
 
Yaani unataka kusema sisi watanzania hatukuweza kupambana na hao wasaliti wasiojulikana hadi mmarekani alipoingilia kati No kumbuka mabaraza ya viongozi wadini ndio walioanza kukemea then wakafuta wanachi wengine na wapinzani wakapiga kelele sana akiwemo Tundu Lisu ndio wamarekani nao wakaongeza nguvu kwahiyo wanaotakiwa kushukuriwa sio wamarekani peke yao.
 
Yaani unataka kusema sisi watanzania hatukuweza kupambana na hao wasaliti wasiojulikana hadi mmarekani alipoingilia kati No kumbuka mabaraza ya viongozi wadini ndio walioanza kukemea then wakafuta wanachi wengine na wapinzani wakapiga kelele sana akiwemo Tundu Lisu ndio wamarekani nao wakaongeza nguvu kwahiyo wanaotakiwa kushukuriwa sio wamarekani peke yao.
Ni wazi kelelle za Watanzania hazikufua dafu hadi Marekani alipoingilia. Wasiojulikana walikuwa na kiburi cha ajabu sana
 
Back
Top Bottom