Mwande na Mndewa

JF-Expert Member
Feb 26, 2021
949
2,865
Kauli ya Mzee Makamba ya kusema mungu anawaua wabaya na kuwaacha wema na akawataja majina imeniumiza sana binafsi,baada ya kauli hiyo nikawakumbuka wapendwa wangu walioufa,kwa namna ya pekee nikamkumbuka Hayati Rais John Pombe Magufuli aliyekufa akilitetea Taifa kwa damu na nyama hakulala hakupumzika hakuwa na muda wakupoteza kama kiongozi wakitaifa,alifanya kazi kwa uchungu mkubwa na alitaka kuona mabadiliko yanatokea Tanzania sawa sawa na ndoto ya Hayati Baba wa Taifa,Mwalimu Julius Nyerere,nikajiuliza hivi Hayati Daktari John Pombe Magufuli alikuwa mbaya!?

Tunawaenzi mashahidi wa imani waaokufa wakitetea imani,tunawaenzi mashujaa wa Taifa letu waliokufa vita vya Kagera,nilitegemea wanaCCM wangemuenzi Mwenyekiti wao aliyekufa akiwa bado Mwenyekiti wao, Hayati Daktari John Pombe Magufuli kwa dhati ya moyo kwa kuwa Magufuli amekufa kwa sababu ya CCM kuendelea kukaa madarakani hii sio siri wala habari yakuficha Hayati Magufuli amekufa akilitetea Taifa lake chini ya sera hizi hizi za chama Chama cha Mapinduzi, Rais Magufuli amekufa akipigania kuitimiza ilani ya chama cha mapinduzi, kama tunajigamba hadharani tena kwenye mkutano Mkuu wa CCM kuwa waliokufa ni wabaya na wanaoishi ni wazuri,sijui unajaribu kupeleka taarifa gani kwa Watanzania? basi umegusa nyoyo zetu zinazowakumbuka wapendwa Baba zetu,Mama zetu,kaka zetu,dada zetu na mashujaa wetu waliotangulia mbele ya haki.

Huyu Mzee anapaswa kuomba radhi Watanzania kwa kutamka matamshi yale,kwa busara za uzee ulipaswa kujua kati ya waliokufa hivi karibuni ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Watanzania bado wanaomboleza mioyoni na kwenye akili zao,sasa kwa nini kuwakumbusha kumbusha habari za kifo,nashauri mjadala wowote wa kumdhihaki Daktari John Pombe Magufuli ufungwe,maana mjadala huo hauna afya kwa Taifa la Tanzania. China walipata bahati ya kuwa na Marais wenye akili ya ubunifu Mao Zedong na Deng Xiaoping,China ya sasa ni matokeo ya Marais hao waliokufa, lakini sijasikia Wachina waliwatukana Marais hao, leo Tanzania tunatukana waliokufa akiwemo Rais Magufuli aliyeipeleka Tanzania katika uchumi wa kati na kutamkwa na IMF na alipokufa Umoja wa Mataifa ukamuenzi kwa jambo hilo la pekee lililofanywa na Mtanzania aliyekuwa Mzalendo kwa asilimia 120% kwa nchi yake ya Tanzania,sisi tunatukana waliokufa,ni vyema kuheshimu juhudi za pekee zilizofanywa na mtu aliyekufa.

Nikiishia hapa, Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854

-Bachelor of Business Administration in International Business.

-Master of Leadership and Management.

Recent Publication;-
-Assessment on the effect of Micro-Financing on Poverty Reduction.
 
Tanzania, kuendelea inahitaji Neema ya Mungutu. Baadhi ya viongozi hawako kwa Ajili ya kuleta maendeleo Bali kujinufaisha wao na familia zao.

Huyu huyu Anaetukanwa ndie Amekuja na kufanya mambo makubwa Kwa miaka 5 Maendeleo Ambayo hata baba wa taifa hakuweza kuyaleta kwa zaidi ya miaka 20 Aliyotawala.

Huyu huyu Anaetukanwa ndie Ameweza kununua ndege Ambazo watangulizi wake walishindwa kununua hata ndege moja kwa miaka 10 waliotawala.

Huyu huyu ndie Aliyetujengea Uzalendo na kuipenda nchi yetu.

Chama cha mapinduzi kitapata laana kubwa sana maana huyu wanae mtukana ndio Aliwafanya watembee kifua mbele kwa uchapaji wake wa kazi.

Nimalizie kwa kusema. Ganda la ndizi ni dogo sana lakini linauwezo wa kuangusha Mtu mkubwa.
 
Kauli ya Mzee Makamba ya kusema mungu anawaua wabaya na kuwaacha wema na akawataja majina imeniumiza sana binafsi,baada ya kauli hiyo nikawakumbuka wapendwa wangu walioufa,kwa namna ya pekee nikamkumbuka Hayati Rais John Pombe Magufuli aliyekufa akilitetea Taifa kwa damu na nyama hakulala hakupumzika hakuwa na muda wakupoteza kama kiongozi wakitaifa,alifanya kazi kwa uchungu mkubwa na alitaka kuona mabadiliko yanatokea Tanzania sawa sawa na ndoto ya Hayati Baba wa Taifa,Mwalimu Julius Nyerere,nikajiuliza hivi Hayati Daktari John Pombe Magufuli alikuwa mbaya!?

Tunawaenzi mashahidi wa imani waaokufa wakitetea imani,tunawaenzi mashujaa wa Taifa letu waliokufa vita vya Kagera,nilitegemea wanaCCM wangemuenzi Mwenyekiti wao aliyekufa akiwa bado Mwenyekiti wao, Hayati Daktari John Pombe Magufuli kwa dhati ya moyo kwa kuwa Magufuli amekufa kwa sababu ya CCM kuendelea kukaa madarakani hii sio siri wala habari yakuficha Hayati Magufuli amekufa akilitetea Taifa lake chini ya sera hizi hizi za chama Chama cha Mapinduzi,Rais Magufuli amekufa akipigania kuitimiza ilani ya chama cha mapinduzi,kama tunajigamba hadharani tena kwenye mkutano Mkuu wa CCM kuwa waliokufa ni wabaya na wanaoishi ni wazuri,sijui unajaribu kupeleka taarifa gani kwa Watanzania? basi umegusa nyoyo zetu zinazowakumbuka wapendwa Baba zetu,Mama zetu,kaka zetu,dada zetu na mashujaa wetu waliotangulia mbele ya haki.

Huyu Mzee anapaswa kuomba radhi Watanzania kwa kutamka matamshi yale,kwa busara za uzee ulipaswa kujua kati ya waliokufa hivi karibuni ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Watanzania bado wanaomboleza mioyoni na kwenye akili zao,sasa kwa nini kuwakumbusha kumbusha habari za kifo,nashauri mjadala wowote wa kumdhihaki Daktari John Pombe Magufuli ufungwe,maana mjadala huo hauna afya kwa Taifa la Tanzania.China walipata bahati ya kuwa na Marais wenye akili ya ubunifu Mao Zedong na Deng Xiaoping,China ya sasa ni matokeo ya Marais hao waliokufa,lakini sijasikia Wachina waliwatukana Marais hao, leo Tanzania tunatukana waliokufa akiwemo Rais Magufuli aliyeipeleka Tanzania katika uchumi wa kati na kutamkwa na IMF na alipokufa Umoja wa Mataifa ukamuenzi kwa jambo hilo la pekee lililofanywa na Mtanzania aliyekuwa Mzalendo kwa asilimia 120% kwa nchi yake ya Tanzania,sisi tunatukana waliokufa,ni vyema kuheshimu juhudi za pekee zilizofanywa na mtu aliyekufa.

Nikiishia hapa, Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854

-Bachelor of Business Administration in International Business.

-Master of Leadership and Management.

Recent Publication;-
-Assessment on the effect of Micro-Financing on Poverty Reduction.
Damu za watu zisizo na hatia, Zina Dhamani kubwa kuliko maendeleo kwa sababu unaondoa Roho ya Mungu ambayo inafanya maendeleo
 
Kila nikikumbuka janga la tetemeko la Kagera alivyotutukana nguvu ya kutetea mazuri yake huwa naikoswa kabisa
 
Hivi huyu babu wa hovyo kabisa, aliwaza nini mpaka akatoa kauli mbovu kama hiyo?

Awaombe radhi watanzania na atubu kwa Mwenyezi Mungu!

Itakuwa faraja sana kwetu na Mungu atafurahi sana!

Kwa kauli yake hiyo. Kila kunapotokea msiba inatukumbusha kauli yake hiyo hiyo kwamba, na huyu aliyekufa naye siyo mwema?

Inatuumiza sana aisee
 
Hivi huyu babu wa hovyo kabisa, aliwaza nini mpaka akatoa kauli mbovu kama hiyo?

Awaombe radhi watanzania na atubu kwa Mwenyezi Mungu!

Itakuwa faraja sana kwetu na Mungu atafurahi sana!
Aisee nyie mna nongwa mbaya sana. Hizi chuki hizi mlizipata wapi? Kwann mnachukia wengine hivi?
Mlitaka mungu afanyeji dhidi ya JPM mana mnakufuru sasa inakera kweli
 
Aisee nyie mna nongwa mbaya sana. Hizi chuki hizi mlizipata wapi? Kwann mnachukia wengine hivi?
Mlitaka mungu afanyeji dhidi ya JPM mana mnakufuru sasa inakera kweli
Inakera vipi na wakati hayo yamesemwa hadharani? Wewe ulikuwa mtoto mdogo
 
Jukwaa la Siasa siku hizi limegeuka la visasi, sio tena CCM vs Upinzani, CCM wamejitafutia upinzani wao ndani kwa ndani unazidi kushika kasi, matokeo yake wapinzani wataenda kuchagua upande wa kuegemea hapo, kweli siasa zetu ni kama upepo tu.
 
Inakera vipi na wakati hayo yamesemwa hadharani? Wewe ulikuwa mtoto mdogo
Ujinga wa kihalaiki unawasumbua nyinyi sukuma gang. Aliyekufa membe nyie mnamsema makamba. Mlitaka raisi AWE NANI BAADA YA LILE CHIZI KUFA?
 
Tanzania, kuendelea inahitaji Neema ya Mungutu. Baadhi ya viongozi hawako kwa Ajili ya kuleta maendeleo Bali kujinufaisha wao na familia zao.

Huyu huyu Anaetukanwa ndie Amekuja na kufanya mambo makubwa Kwa miaka 5 Maendeleo Ambayo hata baba wa taifa hakuweza kuyaleta kwa zaidi ya miaka 20 Aliyotawala.

Huyu huyu Anaetukanwa ndie Ameweza kununua ndege Ambazo watangulizi wake walishindwa kununua hata ndege moja kwa miaka 10 waliotawala.

Huyu huyu ndie Aliyetujengea Uzalendo na kuipenda nchi yetu.

Chama cha mapinduzi kitapata laana kubwa sana maana huyu wanae mtukana ndio Aliwafanya watembee kifua mbele kwa uchapaji wake wa kazi.

Nimalizie kwa kusema. Ganda la ndizi ni dogo sana lakini linauwezo wa kuangusha Mtu mkubwa.

Ni muhimu tuangalie mambo haya katika mjadala, ili tutoe maoni yenye fikra chanya kwa mustakabali mwema wa taifa;

1. Maendeleo ni ile hali ya wananchi kutoka katika hali duni kwenda katika hali bora zaidi.
Je ni lini wananchi walio wengi walipata maendeleo?

2. Kusema wazuri hawafi haijamlenga mtu mmoja. Wamekufa wengi na wengi bado wanaishi.
Watu wabaya (waovu, majambazi, wezi, vibaka wachawi n.k maisha yao huwa shakani,hufa au huawa na wananchi wenye hasira. Yawezekana hiyo kauli ilikuwa ya jumla tu na kutafuta sifa za kisiasa).
Kwa nini tuelekeze mawazo yetu kwa mmoja?

3. Aliyoyafanya marehemu duniani, huwa mazuri na mabaya na hubaki kuwa historia inayojieleza yenyewe.
Kwa nini tusihangaike na yaliyopo na yajayo ambayo tuna uwezo wa kurekebisha?
 
Back
Top Bottom