Tunatekeleza-boom kwa wanafunzi wa vyuo nchi nzima limeshatua kwenye akaunti za vyuo

jingalao

JF-Expert Member
Oct 12, 2011
35,052
28,242
Toka Rais Magufuli aingie madarakani sijasikia maandamano ya wanavyuo kuelekea HELSB kudai fedha za mikopo ya elimu ya juu.

Hii ilikuwa ni kero kuu iliyokuwa inapelekea kuibua migomo ya mara kwa mara vyuoni.

Imesimamiwa na kupatiwa ufumbuzi.

Leo ninapoanzisha thread hii nimejiridhisha kupitia msemaji wa serikali ,wahasibu wa vyuo na baadhi ya wanafunzi wa vyuo vikuu nchini kuwa ule mzigo unaosubiriwaga kwa hamu kubwa hasa hasa kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza yaani kwa jina maarufu unaitwa "BOOM" umeingia rasmi kwenye akaunti za vyuo.

Hata hivyo kuna tetesi ya kuwa vipo baadhi ya vyuo vinataka kufanya figisu figisu kwa kujaribu kukatakata hilo boom la wanafunzi kwa sababu mbalimbali zisizo na mashiko ...ni vyema wakaacha kwani katika hili Serikali ya jembe John P Magufuli haitamuacha mtu salama pindi anapochezea haki ya mnyonge.

Wito wangu kwa vijana ambao miezi michache iliyopita walikuwa humu jamvini tukijumuika nao kwa raha na shari na sasa wako kwenye mishemishe za kusaini boom ...wazitunze fedha wanazopata na kuzitumia kwa manufaa ya kielimu zaidi.

Katika kampeni za kuomba kura Rais Magufuli aliahidi kutoa elimu bure hadi sekondari na kwa sasa shule zinapatiwa moja kwa moja fedha za elimu bure.

Vile vile Magufuli aliwaahidi wanafunzi wa elimu ya juu kupata mikopo kwa wakati na kurekebisha utendaji wa HELSB na taasisi nyingine zinazohusiana na elimu ya juu.

Nihitimishe kwa maneno ya Dr Abbas kwamba" Serikali ni Tajiri Sana "

Na hivyo tunaweza kushuhudia Bombardier zikinunuliwa ,Reli ikijengwa,miradi mbalimbali ikitekelezwa kwa fedha za ndani huku wanafunzi wetu wakiwezeshwa kusoma bila vikwazo.

Basi kwa wanavyuo wote njooni hapa tupeane mrejesho wa boom na yanayojiri....


KWA HISANI YA WATU WA TANZANIA!
 
Ni kweli kabisa tangu j5 ya wiki iliopita walio kuwa wamesain walianza kuingiziwa pesa yao na mpaka sasa wanaoendelea kusain wanaingiziwa pesa yao

Kwa hili na mshukuru na kumpongeza mweshimiqa raid JPM
 
Sawa ndugu,..pongez kwa mheshimiwa rais..ntamuunga mkono zaid akipandisha madaraja na nyongeza yetu ya mshahara
Ahadi ni deni mkuu...tuendelee kumuombea siha njema ili aendelee kuinyoosha mifumo iliyopinda.
 
Hongera kwake...
tumejifunza sababu za maandamano ya Bumu enzi hizo zilikuwa zinatengenezwa na wabinafsi wachache kwa maslahi yao.
Kuna mtu mmoja niliwahi kuzungumza naye maeneo ya Upanga na kuniuliza sababu iliyokuwa inachagiza migomo kipindi kile...nilimueleza kwa uwazi kwamba ni kweli wanafunzi wanadai haki zao ambazo pamoja na udogo wake zilikuwa zinacheleweshwa kwa maslahi ya PANYA wachache.

Nashukuru Serikali hii ya magufuli imeweza kuwashughulikia vilivyo panya hao.
 
Hongera kwake...
tumejifunza sababu za maandamano ya Bumu enzi hizo zilikuwa zinatengenezwa na wabinafsi wachache kwa maslahi yao.
Kuna mtu mmoja niliwahi kuzungumza naye maeneo ya Upanga na kuniuliza sababu iliyokuwa inachagiza migomo kipindi kile...nilimueleza kwa uwazi kwamba ni kweli wanafunzi wanadai haki zao ambazo pamoja na udogo wake zilikuwa zinacheleweshwa kwa maslahi ya PANYA wachache.

Nashukuru Serikali hii ya magufuli imeweza kuwashughulikia vilivyo panya hao.
 
Vile vile Magufuli aliwaahidi wanafunzi wa elimu ya juu kupata mikopo kwa wakati na kurekebisha utendaji wa HELSB na taasisi nyingine zinazohusiana na elimu ya juu.

Nihitimishe kwa maneno ya Dr Abbas kwamba" Serikali ni Tajiri Sana "

Na hivyo tunaweza kushuhudia Bombardier zikinunuliwa ,Reli ikijengwa,miradi mbalimbali ikitekelezwa kwa fedha za ndani huku wanafunzi wetu wakiwezeshwa kusoma bila vikwazo.
Taarifa hizi nzuri kwako wapelekee wale baadhi ya 30000 ambao mikopo wanaisikia kwenye bomba tu, na wao wanavigezo vya kupata mkopo lakini serikali hii tajiri (kama usemavyo wewe na Abbas) imewachinjia baharini kwani imewaona hawana uhitaji.
 
kuna ukweli katika andishi lako. ila tatizo lipo hasa ukizingatia waliopewa mkopo kwa mwaka wa kwanza ukilinganisha na idadi ya walioomba mkopo huo. serikali itoe mkopo kwa wanachuo wote waliopata vyuo na waliomba bodi mikopo....
 
Siamini katika haya mambo! Mkopo si kitu cha kushabikia ingalikuwa ni ruzuku sawa. Mkopo unatakiwa urejeshwe ni deni si hisani.
 
Unajua kuna vijana karibu 30000 hawajapata mkopo? unajua rais aliahidi akiwa rais kila mwanafunzi atapata mkopo?? sasa hao 30000 sio wanafunzi au???

Sjilingi imeshuka, umeme wa mgao, mikopo mnazingua kutoa!! alikua anabip kuomba urais ... ina maana alikua hajajiandaa!! Hahahaha wa bongo bana...kuongoza nchi sio sawa na kuswaga ng'ombe wa chato!!
 
Toka Rais Magufuli aingie madarakani sijasikia maandamano ya wanavyuo kuelekea HELSB kudai fedha za mikopo ya elimu ya juu.

Hii ilikuwa ni kero kuu iliyokuwa inapelekea kuibua migomo ya mara kwa mara vyuoni.

Imesimamiwa na kupatiwa ufumbuzi.

Leo ninapoanzisha thread hii nimejiridhisha kupitia msemaji wa serikali ,wahasibu wa vyuo na baadhi ya wanafunzi wa vyuo vikuu nchini kuwa ule mzigo unaosubiriwaga kwa hamu kubwa hasa hasa kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza yaani kwa jina maarufu unaitwa "BOOM" umeingia rasmi kwenye akaunti za vyuo.

Hata hivyo kuna tetesi ya kuwa vipo baadhi ya vyuo vinataka kufanya figisu figisu kwa kujaribu kukatakata hilo boom la wanafunzi kwa sababu mbalimbali zisizo na mashiko ...ni vyema wakaacha kwani katika hili Serikali ya jembe John P Magufuli haitamuacha mtu salama pindi anapochezea haki ya mnyonge.

Wito wangu kwa vijana ambao miezi michache iliyopita walikuwa humu jamvini tukijumuika nao kwa raha na shari na sasa wako kwenye mishemishe za kusaini boom ...wazitunze fedha wanazopata na kuzitumia kwa manufaa ya kielimu zaidi.

Katika kampeni za kuomba kura Rais Magufuli aliahidi kutoa elimu bure hadi sekondari na kwa sasa shule zinapatiwa moja kwa moja fedha za elimu bure.

Vile vile Magufuli aliwaahidi wanafunzi wa elimu ya juu kupata mikopo kwa wakati na kurekebisha utendaji wa HELSB na taasisi nyingine zinazohusiana na elimu ya juu.

Nihitimishe kwa maneno ya Dr Abbas kwamba" Serikali ni Tajiri Sana "

Na hivyo tunaweza kushuhudia Bombardier zikinunuliwa ,Reli ikijengwa,miradi mbalimbali ikitekelezwa kwa fedha za ndani huku wanafunzi wetu wakiwezeshwa kusoma bila vikwazo.

Basi kwa wanavyuo wote njooni hapa tupeane mrejesho wa boom na yanayojiri....


KWA HISANI YA WATU WA TANZANIA!


Kwa hili Magu tunampongeza...migomo mingi hutokea semister ya 2...ndio Boom hucheleweshwa....Ngoja tusubiri semister ya 2...hii ya kwanza mambo Good
 
Taarifa hizi nzuri kwako wapelekee wale baadhi ya 30000 ambao mikopo wanaisikia kwenye bomba tu, na wao wanavigezo vya kupata mkopo lakini serikali hii tajiri (kama usemavyo wewe na Abbas) imewachinjia baharini kwani imewaona hawana uhitaji.
Siamini kama kuna mwenye vigezo amekosa mkopo.
 
Back
Top Bottom