Tunataka Rais Mwanamke Pia, acheni danganya toto

Gerad2008

JF-Expert Member
Jun 9, 2009
583
287
Makamba asiwaone watanzania watoto wadogo. Ni kweli kwamba tangu uhuru mihimili hii mitatu yaani Bunge ,Serikali na Mahakama hazijawahi ongozwa na mwana mama. Kwa lengo jema hilohilo aliloonyesha kuwa wakati umefika kwa bunge kuongozwa na mwanamke basi na Mwaka 2015 wamteue mgombea urais wa CCM mwanamke. Kama wataona huko ni mbali basi watupatiea basi hata Waziri Mkuu mwanamke ili kuonyesha wanajali sana usawa wa kijinsia.

Sababu nyepesi alizotoa Makamba ni janja ya CCM kumpitisha aliyependekezwa na wenye nchi yaani MAFISADI kwa lengo la kulinda masalahi ya wenye Chama kwa sasa yaani MAFISADI tena. Habari kwamba Anna Makinda alishauriwa na MAFISADI kuchukua fomu kumtoa Bosi wake ziliandikwa kabla ya tukio la Jana na hii inanifanya niamini kwamba kuna mpango mahsusi ulioandaliwa na MAFISADI kutwaa nchi yetu.

Njaa za viongozi wa CCM ambao Elimu zao zinatia shaka ndizo zinataka kuifikisha nchi yetu nzuri pabaya. Nchi ipo mikononi mwa walevi wa madaraka, wezi, na waporaji ambao wanataka kutunyonya hadi tone la mwisho.

Kutugeresha watanzania eti wakati umefika wa kuwa na spika mwanamke ni uchuro ambao kwetu sisi wenye kuona mbali tunajua ni yale yale ya kumwona mtanzania Mbumbumbu na mazezeta. Hili goli hutufungi mgosi tumeliona na kulidaka na tunarudia kusema"WATANZANIA HATUDANGANYIKI TENA". Hatua zote mnazopiga za kutaka kutufanyia ubaradhuli na ufedhuli kwa sababu mtu mnataka kukata ya tamaa zenu mbaya za mali tumeziona na tuko macho tukizifuatilia. Tumeanza asubuhi hii 2010 na ikifika jioni 2015, tutakuwa tumewazunguka na hamtakwenda mahali lazima tuwabwage Mafisadi na chama chenu cha kifisadi ambacho kamwe hakimtaki yeyote aliye safi bali wachafuzi wa hali ya hewa ya uchumi wa nchi yetu.

Mnachofanya sasa hivi ni kuboresha hali ya umaskini wa mtanzania kwa kunyanganya hata ile rasilimali kidogo aliyopewa na muumba wetu kupitia mikataba mibovu ya madini, kuuza mali asili ya nchi yetu kwa waarabu kwa lugha inayonuka ya uwekezaji. Laana mnayopata kutokana na machozi ya watanzania waliohamishwa maeneo waliyozaliwa tangu mababu kwa kisingizio cha kupisha wawekezaji zitakuwa juu ya watoto wenu na vizazi vyenu. Mtatafuta wala hamtaridhika na mtakula hamtashiba na mwisho wa siku tunairudisha nchi mikononi mwa watanzania wenye nia na dhamira njema na nchi yao.

Watanzania tujipange kwa mwaka 2015, tuhakikishe tumemaliza uzia kwa mustakabali wa watanzania woote.
 
Wakimaliza usawa wa kijinsia wawakumbuke walemavu. Tunataka Spika ALBINO mwaka 2015. Waziri Mkuu asiyeona mwaka 2020 na Rais kiziwi mwaka 2025.
 
Wakimaliza usawa wa kijinsia wawakumbuke walemavu. Tunataka Spika ALBINO mwaka 2015. Waziri Mkuu asiyeona mwaka 2020 na Rais kiziwi mwaka 2025.

Mbona viongozi wengi wa CCM ni walemavu!
Katibu mkuu wao ni mlemavu wa mdomo. kila linalomjia huropoka tu.
 
Makamba asiwaone watanzania watoto wadogo. Ni kweli kwamba tangu uhuru mihimili hii mitatu yaani Bunge ,Serikali na Mahakama hazijawahi ongozwa na mwana mama. Kwa lengo jema hilohilo aliloonyesha kuwa wakati umefika kwa bunge kuongozwa na mwanamke basi na Mwaka 2015 wamteue mgombea urais wa CCM mwanamke. Kama wataona huko ni mbali basi watupatiea basi hata Waziri Mkuu mwanamke ili kuonyesha wanajali sana usawa wa kijinsia.

Sababu nyepesi alizotoa Makamba ni janja ya CCM kumpitisha aliyependekezwa na wenye nchi yaani MAFISADI kwa lengo la kulinda masalahi ya wenye Chama kwa sasa yaani MAFISADI tena. Habari kwamba Anna Makinda alishauriwa na MAFISADI kuchukua fomu kumtoa Bosi wake ziliandikwa kabla ya tukio la Jana na hii inanifanya niamini kwamba kuna mpango mahsusi ulioandaliwa na MAFISADI kutwaa nchi yetu.

Njaa za viongozi wa CCM ambao Elimu zao zinatia shaka ndizo zinataka kuifikisha nchi yetu nzuri pabaya. Nchi ipo mikononi mwa walevi wa madaraka, wezi, na waporaji ambao wanataka kutunyonya hadi tone la mwisho.

Kutugeresha watanzania eti wakati umefika wa kuwa na spika mwanamke ni uchuro ambao kwetu sisi wenye kuona mbali tunajua ni yale yale ya kumwona mtanzania Mbumbumbu na mazezeta. Hili goli hutufungi mgosi tumeliona na kulidaka na tunarudia kusema"WATANZANIA HATUDANGANYIKI TENA". Hatua zote mnazopiga za kutaka kutufanyia ubaradhuli na ufedhuli kwa sababu mtu mnataka kukata ya tamaa zenu mbaya za mali tumeziona na tuko macho tukizifuatilia. Tumeanza asubuhi hii 2010 na ikifika jioni 2015, tutakuwa tumewazunguka na hamtakwenda mahali lazima tuwabwage Mafisadi na chama chenu cha kifisadi ambacho kamwe hakimtaki yeyote aliye safi bali wachafuzi wa hali ya hewa ya uchumi wa nchi yetu.

Mnachofanya sasa hivi ni kuboresha hali ya umaskini wa mtanzania kwa kunyanganya hata ile rasilimali kidogo aliyopewa na muumba wetu kupitia mikataba mibovu ya madini, kuuza mali asili ya nchi yetu kwa waarabu kwa lugha inayonuka ya uwekezaji. Laana mnayopata kutokana na machozi ya watanzania waliohamishwa maeneo waliyozaliwa tangu mababu kwa kisingizio cha kupisha wawekezaji zitakuwa juu ya watoto wenu na vizazi vyenu. Mtatafuta wala hamtaridhika na mtakula hamtashiba na mwisho wa siku tunairudisha nchi mikononi mwa watanzania wenye nia na dhamira njema na nchi yao.

Watanzania tujipange kwa mwaka 2015, tuhakikishe tumemaliza uzia kwa mustakabali wa watanzania woote.
Makamba ni mjinga. Tulitegemea hila hizi wanazotumia ili waingize kipenzi chao Anna Makinda kwenye uspika wangezitumia pia kuingiza wanawake wengi kupitia sanduku la kura. Lakini badala yake waliwaengua na kusubiri wawaingize kwa huruma za viti maalum.
Makamba na kundi la majambazi wa ccm sikilizeni, sisi hatuhitaji kuwa na spika basing on a gender reason lakini tunahitaji Spika mwenye uwezo wa kuwa Spika muadilifu. Whether ni mwanamke au mwanaume. Kwani Spika muadilifu ni yule tu ambaye hatakuwa na makundi wala hatapendelea chama chake kama kina uovu lakini yuko tayari kulitetea taifa kwanza na si chama kwanza.
 
Hahahaaaa nimeipenda hii ya ULEMAVU wa Viongozi wa CCM,Katibu mlemavu wa mdomo, M/kiti mlemavu wa miguu na wanawake maana kila saa anaanguka na kuwaangukia wanawake, Kinana mlemavu wa kichwa maana hana hata nywele na akili ni nywele :tape:
 
"WATANZANIA HATUDANGANYIKI TENA".

endelea kuwaelimisha waTZ wanaoishi mikoa ya pwani (waislam?) ili nao wasiendelee kudanganyika na thithiem.
 
Back
Top Bottom