Tunasubiri Nchi Wahisani Waje WATUAMURU Hatua za Kuchukua Kwenye Wizi?

Huo wizi uko wapi, mnabwabwaja na kuhororoja wakati hakuna mahali panapoonesha pameibiwa.

Mlitaka umeme wa bure?
Wewe ni wa kutukanwa matusi yote, hao waliokutuma wamezoea kukufanya wewe ni mtu wa kufunuliwa na kutolewa ufahamu, huna lolote, wewe ni chakula cha hao wezi na ipo siku yako,hata huruma hauna!
 
Watanzaniaaaaaaa vichekesho kwelikweli kama hadithiiiii sasa hao waliolipwa fedha ni zawadi kwa lipi au wao ndo wazalisha umeme?
 
Huo wizi uko wapi, mnabwabwaja na kuhororoja wakati hakuna mahali panapoonesha pameibiwa.

Mlitaka umeme wa bure?
haa haa kwa hiyo Chenge, tibaijuka, askofu kilaini na kina ngeleja, walianza lini kuuza umeme kwa tanesco? Mpaka wakagawana mapesa pale mkombozi benki?
 
Wewe wacha porojo, fedha za IPTL zilikuwa zinapelkwa account ya escrow kuanzia mwaka 2004 na msimamizi wa shughuli hizo wakati wa mgogoro wa IPTL na TANESCO alikuwa ni RITA, sijuwi ni nini usichokielewa hapo?
haa haa, kwa nini zipelekwe escrow badala ya IPTL?MAMA umepata ngapi kutoka pale mkombozi benki? Kweli njaa mbaya sana!
 
Kwa CCM hata ukiwa taahira unapewa ubunge! Yule Mama, Lusinde na Chombo kuna nuts zimamiss vichwani mwao!

Hawa wabunge wa aina hiyo Serikali imesimamishiwa hiyo budget support hawana hata moja la kuishauri nini cha kufanya. Jee wakijitoa kabisa kwa ajili ya huo ujinga wao wana njia gani mbadala kushauri serikali? Kweli nchi yetu imefikia mahali tuna wabunge maarufu ambao mpaka mwingine anatoa muda wake wa mchango ili aongee kwani yeye ni bingwa wa mipasho?
Aibu gani hii? Nenda tuu hapo Kenya, wabunge aina hiyo ya Lusinde sio tuu hawaongei bali hawapo kabisa.
Ni aibu kesho au kesho kutwa tuje tuambiwe na mashika ya misaada MWONDOE YULE NA YULE NI WEZI LA SIVYO HATUTOI PESA ZETU.
 
Mi nadhani nchi wahisani wafunge bomba la misaada for some 2 years then nadhani serikali itakuwa makini na rasilimali za nchi. Inasikitisha sana kupata kumbusho hili kutoka kwa wahisani.
 
Huo wizi uko wapi, mnabwabwaja na kuhororoja wakati hakuna mahali panapoonesha pameibiwa.

Mlitaka umeme wa bure?

Huu sijui nikuite nawe msaka tonge ww hakuna anaetaka umeme wa bure.
Swali kubwa kuwa account ya Escrow ilifunguliwa kwa nia gani? Jibu rahisi sana ilikuwa amana kwa ajili ya kuja kulipa IPTL mgogoro ukiisha na si kwamba kupeleka hela escrow ilikuwa ndio wanalipa hapana ndio maana walikuwa hawapewi objectivity yoyote as a payment( I mean kama walikuwa wanalipa it means walipaswa kupewa receipts) tuletee document yoyote iliyokuwa inatoka IPTL kama kukubali matokeo.
Achana na kutumika jali maslahi mapana na si unafiki unakufanya uonekane mjinga
 
Imefikia wakati serikali inaona ni sawa mtumishi wa umma kupewa rushwa na supplier ni sawa ,halafu the very same mtumishi ni part ya waliotengeneza mkataba wa kumpa kazi supplier, huu ni uwendawazimu
Hawa pccb naona wana deal na vihakimu na walimu rushwa kubwa zote ni sawa kwao
 
Mkuu nadhani huyu FF ni yule mbunge mmama mwalimu wa msingi anayesema kamati ya Zitto PAC ni ya wapinzani kavaa mipete kama mganga wa kienyeji

Yaani kabla hajasema kaz yake ni ipi nilikuwa najiuliza huyu mama ana elimu gani ndo baadae nikajua ni mwalimu wa upe. Mjinga sana yule mmama.
 
Yaani kabla hajasema kaz yake ni ipi nilikuwa najiuliza huyu mama ana elimu gani ndo baadae nikajua ni mwalimu wa upe. Mjinga sana yule mmama.

Lakini uliona jinsi wabunge wa CCM walivyokuwa wanamshangilia akiwepo Membe? Mie nadhani yule mama aweza kuwa mjinga ila mjinga zaidi ni wale waliokuwa wakimpongeza akiwepo huyo mtaka Urais asiyejitambua.
 
Hivi kama wakiona yaliyotokea jana na kuamua kuendelea kutu puuza na kukaa kimya na hela zao tutafanya ni i na ndio hivyo tena ndugu zetu wanaendelea kufa kwa kukosa dawa?
 
Hivi kama wakiona yaliyotokea jana na kuamua kuendelea kutu puuza na kukaa kimya na hela zao tutafanya ni i na ndio hivyo tena ndugu zetu wanaendelea kufa kwa kukosa dawa?
Wanafahamu vizuri sana kila kinachoendelea.
 
Mkakati wa CCM wa kuwaokoa wezi katika sakata hili la akaunti ya Escrow utatuaibisha kama taifa huko tuendako. Wahisani walisitisha misaada yao ya Kibajeti kwa Tanzania hadi scandal hii ishughulikiwe. Hii inamaana hata ukweli wanaujua ila hatua za kuchukua ni juu ya Bunge na serikali yetu wenyewe
Sasa nafasi hiyo imepatikana lakini kwa mastajabu ya wengi ni kuwa sasa kuna mkakati wa kuwatetea wahusika. Tunajua wazi kuwa hizo fedha za wahisani ni kodi za watu wao sasa kama tunalia shida lakini fedha zetu zinatafunwa tunachekelea basi watakuja na option mbaya sana kwetu kwamba kama hamchukui hatua kwa huyu na yule basi hamna sababu ya kuwapa misaada hii na ile. JEE HILI NDIO WATANZANIA TUMEWATUMA WABUNGE WETU? KWAMBA KUCHUKUA HATUA MPAKA TUSHINIKIZWE NA WAHISANI

Ndugu najuuuta kuzaliwa tz.
 
Ndugu najuuuta kuzaliwa tz.

No no no! Huna sababu ya kujuta kuzaliwa nchi kama hii yenye neema. Juta kwa nini wewe na wengine (yaani sisi wote) hatuchukui hatua? Hivi unadhani kama kwa yale ya jana tuu leo watu kama elfu tatu hivi pale Dodoma wangejitokeza na mabango yao kuja Bungeni na kulaani kinachoendelea unadhani kuna Mbunge angebwabwaja ujinga tena? Au wanafunzi wa UDOM na St Johns University waliokosa mikopo wange vamia pale Bungeni japo kwa dakika tano tuu ambazo zingetosha kuleta attention ya media na wabunge wenyewe lazima wangekuwa na woga na kauli za ajabu.
Lakini wakiangalia wanaona sisi wote ni Business as usual
 
Watanzaniaaaaaaa vichekesho kwelikweli kama hadithiiiii sasa hao waliolipwa fedha ni zawadi kwa lipi au wao ndo wazalisha umeme?
Hilo swali hata Ikulu wameshindwa kujibu mpaka leo na ripoti ya PAC ndio hiyo imefungiwa kabatini. Ni kweli kuwa lazima tuje tufundishwe jinsi ya kuchukulia hatua wezi.
 
Tangu sakata la ESCROW lilipohitimishwa kwa kusubiria hadi Januari 2015, habari za siasa kwa sasa hazina zimepooza.

Wananchi watasahau.Kisha upepo kimbunga wa ESCROW uliovuma sana utapita.Maisha mengine yataendelea.Tumezoea....
 
Back
Top Bottom