Tunashindwa makubwa, hata hili lituhinde?

Dangire

JF-Expert Member
Oct 5, 2011
221
68
dakika chache zijazo ntatoka ofisini(mitaa ya mwenge dsm) kuelekea hom, mawazo yamenijaa ni jinsi gani nitapata gari za mbagala. shida ni kubwa sana kupata usafiri. tatizo kubwa zaidi ni jinsi gani nitaweza kupanda kwenye gari bila kashkash? hata lini tutaendelea na hii ''survival for the fittest?" ........serikali kweli inashindwa kuiongoza jamii kuwa na utaratibu wa kupanga foleni (kila mtu anapofika kituo cha anakoelekea)?

hivi hii si ingesaidia watu wote kuuona usafiri wa daladala kuwa ni usafiri bora na ni wa kila mtu? hivi hata wenye magari binafsi wanaoongeza foleni njiani si wangethubutu kuyaacha magari yao na kupanda daladla? lakini kwa hali hii......hakuna atakayesema aache kwenda mjini na 'private car' yake eti kwa kutegemea daladala. usafiri wa daladala hizi hapa jijini umekuwa ni moja ya kero zinazowakumba wakaazi wa dar.

hebu fikiria, mtoto (wanafunzi) anapataje nafasi kwenye gari kwa hali hii?
je, walemavu watapandaje usafiri huu katika hali hii?
je, wanawake wanawezaje kustahimili hali hii?

serikali ikumbuke kuwa wakaazi wa dar nao wana haki ya kusafiri kwa heshima (utu wao ulindwe). Ni lazima serikali iwajali watu wao....sio kweli kwamba watz tumezoea shida....huu ni uzembe tu wa watendaji kuhakikisha hata matatizo haya madogo madogo yanatatuliwa. yaani....badala ya kufurahia kuishi bongo, tunajikuta tunavumilia kuishi hapa. ukiamka asubuhi unawaza ni namna gani utapata usafiri....na jioni nayo tunaanza kuwaza namna ya kufika hom....kweli?

chonde chonde serikali na watendaji wote wa jiji tujengeeni ustaarabu wakazi wa dar ili tufurahie maisha.........
 
Pole sana mm ushauri wangu tafuta kazi ingine huko Mbagala na sio lazima ufanye kazi Mwenge
tafuta kazi yako ya kujiajiri huko Mbagala na achana na kazi za kuajiriwa huko Mwenge au hamia Mwenge km bado utapenda kuajiriwa na watu wengine.
Ungehama Dar -es-salaam ukaja huku bush kuna Jamii Forum, umeme haukatwi wala hakuna daladala
Ule mpango wa kuweka miji mingine ndani ya Dar naona bado
hivyo nunua kigari chako mwenyewe kwa kuomba Mkopo hapo ulikoajiriwa
Soooory km nimejibu tofauti na
samahani km nimekuudhi nilidhani ushauri wangu ungekusaidia kero ya KUFANYA KAZI MWENGE NA KUISHI MBAGALA NA UNASAFIRI KWA DALADALA
 
Pole ase mi huo mkoa hapo ndo panchoshaga na hali ya hewa, hiyo concetration inazidi afu eneo dogo.

Karibu Arusha.
 
jani mupendweje wakai wa dar acheni lawama , kana kwamba huoni jitihada za mwakyembe na dt pombe kwenye mradi wa mabasi yaendayo kasi
 
Usije mjini kama hupawezi...Dar sio kama Singida kuwa utapanda punda
 
Back
Top Bottom