Tunashabikia UEFA Champions League lakini pesa anayolipwa bingwa wa EPL ni kubwa zaidi

.
mkuu samahani embu fafanua kidogo hapa,,fainali ya play off championship ni ya kumtafta mshindi wa 3 atakaepanda ligi kuu pamoja na bingwa na mshndi wa 2,sasa anapataje hela nyngi kulko bingwa wa epl!??? je mshindi wa 2 na bingwa wa championship?
Huyu jamaa kajichanganya.
 
Hoja hapa ni bingwa wa uefa kulamba pesa ndogo
Hiyo ni kopy tu kuonyesha chelsea alipotwaa ubingwa msimu uliopita alipata pesa ndefu kuliko ile ya leicester pauni million 93 kutokana na wadhamini kuongezeka
Vipi bingwa wa UEFA anapata pesa ndogo hivyo ?
Nilitegemea awe anakunja ndefu kwa kuwa ni michuano pia inayotazamwa duniani kote
Kwani mshindi wa UEFA analipwa sh ngapi wewe mbona hutoi mchanganuo wa bingwa wa UEFA anakusanya sh ngapi???
 
Mbona fainal ya play off ya championship ya uingereza bingwa anapata pesa nyingi kuliko bingwa wa EPL na UCL?

Stoke city wakiwa mabingwa hawawezi kupewa pesa atakazopewa United hata kama wakiwa nafasi ya 10.
Hapana sio kweli EPL wana utaratibu team zote league ikiwa inaanza team zote mgao sawa bila kujali position, mfano Milion 100, sasa pesa inazidi kutokana na position % fulani lakini kubwa team ambayo itakuwa kwenye live games nyingi pesa ina add kila mechi unaweza kukuta team ya pili inapata zaidi ya bingwa. Hii ilitokea wakati wa kina Suarez walikuwa wa pili lakini sababu walikuwa team ina burudisha na ilikuwa top pick katika live games wakapata pesa nyingi zaidi ya City. Tofauti ya Spain wakubwa wanajadili mkataba wao maana ndio wanauza zaidi ila kwa sasa wanataka kubadili wawe kama EPL. hii ndio sababu ya EPL teams kuwa tajiri.
 
Mabingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL), Chelsea wanatarajiwa kulamba kitita cha bilioni 434 za Kitanzania kutoka kwa wasimamizi wa ligi hiyo inayotarajiwa kumalizika wikiendi hii.

Fedha hizo ambazo ni sehemu ya zawadi ya kutwaa ubingwa pamoja na haki ya matangazo ya luninga, Chelsea imejikusanyia pesa nyingi paundi mil 150, tofauti ya bingwa wa msimu wa uliopita Leicester City aliyepata paundi 93.

Hii inafuatia kuongezeka dau la udhamini kwenye matangazo ya ndani kwenye mkataba mpya wa EPL dhidi ya warusha matangazo SkySport na BT Sports wanaorusha jumla ya michezo 168 ya ligi hiyo moja kwa moja.

Mkataba mpya wa EPL na wenye haki ya kuonyesha michezo hiyo unaonyesha kila mechi moja ni sawa na paundi mil 10.19 sawa na fedha za kitanzania bil 2.7 kwa mchezo.

Mgawanyo wa fedha hizo unaonyesha mshindi wa pili anapata paundi milioni 144, mshindi wa tatu paunid milioni 142, mgao huo unaendelea kwa timu zote na timu ya mwisho inaambulia paundi mil 97
Hivi ni Chelsea gani hapo unayoiongelea hapo na kwa kipindi gani?
 
Mabingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL), Chelsea wanatarajiwa kulamba kitita cha bilioni 434 za Kitanzania kutoka kwa wasimamizi wa ligi hiyo inayotarajiwa kumalizika wikiendi hii.

Fedha hizo ambazo ni sehemu ya zawadi ya kutwaa ubingwa pamoja na haki ya matangazo ya luninga, Chelsea imejikusanyia pesa nyingi paundi mil 150, tofauti ya bingwa wa msimu wa uliopita Leicester City aliyepata paundi 93.

Hii inafuatia kuongezeka dau la udhamini kwenye matangazo ya ndani kwenye mkataba mpya wa EPL dhidi ya warusha matangazo SkySport na BT Sports wanaorusha jumla ya michezo 168 ya ligi hiyo moja kwa moja.

Mkataba mpya wa EPL na wenye haki ya kuonyesha michezo hiyo unaonyesha kila mechi moja ni sawa na paundi mil 10.19 sawa na fedha za kitanzania bil 2.7 kwa mchezo.

Mgawanyo wa fedha hizo unaonyesha mshindi wa pili anapata paundi milioni 144, mshindi wa tatu paunid milioni 142, mgao huo unaendelea kwa timu zote na timu ya mwisho inaambulia paundi mil 97
Bingwa msimu huu 2017/2018 ni man city Chelsea ni wa tano huo ubingwa kauchukulia wapi
 
.
mkuu samahani embu fafanua kidogo hapa,,fainali ya play off championship ni ya kumtafta mshindi wa 3 atakaepanda ligi kuu pamoja na bingwa na mshndi wa 2,sasa anapataje hela nyngi kulko bingwa wa epl!??? je mshindi wa 2 na bingwa wa championship?
Championships ina timu 24. Mbili zinapanda daraja moja kwa moja. Hawa ni bingwa na mshindi wa pili. Mshindi wa 3,4,5,na 6 wanacheza play off kupata timu ya 3 itakayopanda daraja kucheza EPL.

Baada ya kucheza zinabaki mbili. Fainal inapigwa pale Wembley. Mshindi wa hii vame ndio anapata pesa nyingi kuliko yule bingwa wa UCL na Epl.

Kwa kuongeza. Kwenye mashindani yote ngazi za club barani ulaya fainal ya championship bingwa ndio anapata pesa nyingi kuliko mabingwa wa makombe mengine barani ulaya. Iwe laliga, Serie A, Ligue 1 na hata Bundasliga...
 
Hapana sio kweli EPL wana utaratibu team zote league ikiwa inaanza team zote mgao sawa bila kujali position, mfano Milion 100, sasa pesa inazidi kutokana na position % fulani lakini kubwa team ambayo itakuwa kwenye live games nyingi pesa ina add kila mechi unaweza kukuta team ya pili inapata zaidi ya bingwa. Hii ilitokea wakati wa kina Suarez walikuwa wa pili lakini sababu walikuwa team ina burudisha na ilikuwa top pick katika live games wakapata pesa nyingi zaidi ya City. Tofauti ya Spain wakubwa wanajadili mkataba wao maana ndio wanauza zaidi ila kwa sasa wanataka kubadili wawe kama EPL. hii ndio sababu ya EPL teams kuwa tajiri.
Upo sawa. Vp kwenye fainal ya championship?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom