Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Sanamu inaweza kuwa ni picha, kinyago,kikaragosi au kitu tuu kinachofurahisha, kukonga moyo na hata kujenga imani ambayo huwa ni vigumu kubadilika.
Nawaangalia Watanzania wengi waliopoteza haki yao ya kuwa huru kwa kusujudu sanamu na kufurahia uzuri wa sura iliyokonga mioyo yao, kiasi cha kusujudu na kuamini kila sarufi, kiambishi, kiunganishi, kivumishi, neno, ahadi na hata tungo zilizojaa matumaini ya bandia zilizotoka kinywani kwa huyu anayeabudiwa na kusujudiwa.
Yawezekana ni limbwata au ulevi wa gongo, mirungi au kule kuelea baada ya kupata msokoto wa bangi ambako hufikia mtu kufanya mambo yasiyoeleweka kwa watu wenye akili zao timamu na hivyo hisia kuwa huyu aliyelewa au kupumbazwa hanazo huongezeka.
Lakini, waliolewa kilevi ni wasomi, wenye taaluma, upeo na uwezo wa kukokotoa kati ya shayiri na mtama. Na ni hawa ambao huwapa tumaini butu na bubu wale wengi ambao elimu yao ya haki zao kikatiba imefunikwa na gamba la furukombe nao huishia kushangilia kulishwa makombo na kutolea zaka sanamu.
Inastaajabisha na kushangaza wimbi na wingu la wanaosujudu Sanamu na kuitolea Zaka wanavyopiga vifua vyao makonde ya kujenga hisia chanya za mapenzi yasiyo na kikomo, kuwa sasa Amani na utimilizi wa njozi zao unatimia. Hata machozi ya furaha na makamasi yanawatoka kwa kurukwa na fahamu za kufurahia uzuri wa taswira na umaridadi wa kinyago wanachokiabudu na kukitukuza.
Tena kwa nyenzo za hali ya juu, kwa hali na mali kwa ushirika wamekubali na kuenzi Sanamu na kuiabudu, kuisujudu wakiipigia magori na wakiwa tayari kutoa uhai wao kuitetea sanamu. Wanahubiri uzuri wa sanamu yao, kusifia ilivyo na haiba ya kutamanisha na jinsi inavyowafurahisha mithili ya kikaragosi kinachoutwa kamba na kunyanya mabega na kifua na kupumbaza watu na kuwa kichekesho.
Kwa udi na vumba hawa ndugu wamesujudu na kutukuza Sanamu na kuifanya Mungu wao. Wanapita kila kona ya himaya wakihubiri habari za kusifia sanamu yao na kuipamba kwa manukato na mafuta ya uto.
Wala si kwa masikhara, ni wakali mno wakiitetea Sanamu yao na kuibeba juu na ukikataa kuisujudu, nafsi yako hupigwa mhuri wa kuwa msaliti na mchokozi usiyependa Kushikamana na nduguzo ambao kwao wao, Sanamu ni tumaini la maisha mema.
Utulivu wao huja kwa kuirembesha Sanamu na kuipa uhai bandia ambao wanautembeza kila mtaa na kona na kudai kila mtu aisujudu Sanamu ili neema ijae katika Maisha ya mtazamaji na mwabudu sanamu naye kugeuka kuwa muumini Bora.
Lakini wanasahau, sanamu ni sanamu, haina uwezo wa kuwa na fahamu, imechongwa, imependezeshwa lakini haina uhai binafsi wa kujirembesha wala kujiuza. Imechongwa na aliyepata maono na kuona haja ya kuuza Sanamu hii kama Imani.
Sanamu hii inayosujudiwa, si Mungu, bali inalazimishwa iabudiwe kuwa Mungu ambaye aliumba dunia kutokana na kazi yake na uwezo wake wa kufikiri na uumbaji. Lakini wanayoipenda Sanamu na hata kudiriki kudai wao ni wamiliki, wanashurtisha kila mtu apige goti, atoe zaka na kuahidi kula kiapo cha utii kuisujudu na kuitumikia Sanamu, ilhali Sanamu imekaa kama mlima au kifusi cha mchanga kisicho na uhai wowote.
Ajabu, hawa wanaoipaka manukato Sanamu hii ili inukie na kuvutia, wameshindwa kuoonyesha mazao ya kweli ya sadaka na sala zao za maombi kutoka kwa Sanamu. Wanaamini tukiendelea kuitazama Sanamu kwa kukazia macho kwa nguvu na kuendelea kuisujudu kwa kasi, basi ari ya kuwa na wokovu itatimia na hovyo wote tunapaswa kuamini wanachokiamini.
Najiuliza, ni ulevi gani huu wa kupindukia wa kuamini kuwa Sanamu yaweza leta uhai? Je hata ikirembwa namna gani, si bado ni Sanamu na kamwe haiwezi yenyewe kuwa na Uhai wa kweli wa kuamsha mioyo na kuihamasisha?
Sasa kwa nini kama yule mlevi wa pombe ya Pingu tulazimike kuishangilia, kuiabudu na kuipigia magoti kama si kuanguka kifudifudi kuitukuza na kuisujudu Sanamu huku tukitoa zaka za haki yetu kuifanya Sanamu Mungu?
Kuna dhambi gani kuikataa Sanamu au kukataa kuburuzwa na makuhani wanaolazimisha Ibada ya kafara na kuisujudu Sanamu?
Nawaangalia Watanzania wengi waliopoteza haki yao ya kuwa huru kwa kusujudu sanamu na kufurahia uzuri wa sura iliyokonga mioyo yao, kiasi cha kusujudu na kuamini kila sarufi, kiambishi, kiunganishi, kivumishi, neno, ahadi na hata tungo zilizojaa matumaini ya bandia zilizotoka kinywani kwa huyu anayeabudiwa na kusujudiwa.
Yawezekana ni limbwata au ulevi wa gongo, mirungi au kule kuelea baada ya kupata msokoto wa bangi ambako hufikia mtu kufanya mambo yasiyoeleweka kwa watu wenye akili zao timamu na hivyo hisia kuwa huyu aliyelewa au kupumbazwa hanazo huongezeka.
Lakini, waliolewa kilevi ni wasomi, wenye taaluma, upeo na uwezo wa kukokotoa kati ya shayiri na mtama. Na ni hawa ambao huwapa tumaini butu na bubu wale wengi ambao elimu yao ya haki zao kikatiba imefunikwa na gamba la furukombe nao huishia kushangilia kulishwa makombo na kutolea zaka sanamu.
Inastaajabisha na kushangaza wimbi na wingu la wanaosujudu Sanamu na kuitolea Zaka wanavyopiga vifua vyao makonde ya kujenga hisia chanya za mapenzi yasiyo na kikomo, kuwa sasa Amani na utimilizi wa njozi zao unatimia. Hata machozi ya furaha na makamasi yanawatoka kwa kurukwa na fahamu za kufurahia uzuri wa taswira na umaridadi wa kinyago wanachokiabudu na kukitukuza.
Tena kwa nyenzo za hali ya juu, kwa hali na mali kwa ushirika wamekubali na kuenzi Sanamu na kuiabudu, kuisujudu wakiipigia magori na wakiwa tayari kutoa uhai wao kuitetea sanamu. Wanahubiri uzuri wa sanamu yao, kusifia ilivyo na haiba ya kutamanisha na jinsi inavyowafurahisha mithili ya kikaragosi kinachoutwa kamba na kunyanya mabega na kifua na kupumbaza watu na kuwa kichekesho.
Kwa udi na vumba hawa ndugu wamesujudu na kutukuza Sanamu na kuifanya Mungu wao. Wanapita kila kona ya himaya wakihubiri habari za kusifia sanamu yao na kuipamba kwa manukato na mafuta ya uto.
Wala si kwa masikhara, ni wakali mno wakiitetea Sanamu yao na kuibeba juu na ukikataa kuisujudu, nafsi yako hupigwa mhuri wa kuwa msaliti na mchokozi usiyependa Kushikamana na nduguzo ambao kwao wao, Sanamu ni tumaini la maisha mema.
Utulivu wao huja kwa kuirembesha Sanamu na kuipa uhai bandia ambao wanautembeza kila mtaa na kona na kudai kila mtu aisujudu Sanamu ili neema ijae katika Maisha ya mtazamaji na mwabudu sanamu naye kugeuka kuwa muumini Bora.
Lakini wanasahau, sanamu ni sanamu, haina uwezo wa kuwa na fahamu, imechongwa, imependezeshwa lakini haina uhai binafsi wa kujirembesha wala kujiuza. Imechongwa na aliyepata maono na kuona haja ya kuuza Sanamu hii kama Imani.
Sanamu hii inayosujudiwa, si Mungu, bali inalazimishwa iabudiwe kuwa Mungu ambaye aliumba dunia kutokana na kazi yake na uwezo wake wa kufikiri na uumbaji. Lakini wanayoipenda Sanamu na hata kudiriki kudai wao ni wamiliki, wanashurtisha kila mtu apige goti, atoe zaka na kuahidi kula kiapo cha utii kuisujudu na kuitumikia Sanamu, ilhali Sanamu imekaa kama mlima au kifusi cha mchanga kisicho na uhai wowote.
Ajabu, hawa wanaoipaka manukato Sanamu hii ili inukie na kuvutia, wameshindwa kuoonyesha mazao ya kweli ya sadaka na sala zao za maombi kutoka kwa Sanamu. Wanaamini tukiendelea kuitazama Sanamu kwa kukazia macho kwa nguvu na kuendelea kuisujudu kwa kasi, basi ari ya kuwa na wokovu itatimia na hovyo wote tunapaswa kuamini wanachokiamini.
Najiuliza, ni ulevi gani huu wa kupindukia wa kuamini kuwa Sanamu yaweza leta uhai? Je hata ikirembwa namna gani, si bado ni Sanamu na kamwe haiwezi yenyewe kuwa na Uhai wa kweli wa kuamsha mioyo na kuihamasisha?
Sasa kwa nini kama yule mlevi wa pombe ya Pingu tulazimike kuishangilia, kuiabudu na kuipigia magoti kama si kuanguka kifudifudi kuitukuza na kuisujudu Sanamu huku tukitoa zaka za haki yetu kuifanya Sanamu Mungu?
Kuna dhambi gani kuikataa Sanamu au kukataa kuburuzwa na makuhani wanaolazimisha Ibada ya kafara na kuisujudu Sanamu?