Tunapokuwa na taifa ambalao halina utawala unaofuata misingi ya sheria tutafika huko tunakoenda?

Idugunde

JF-Expert Member
May 21, 2020
6,273
6,637
Utawala wa sheria unataka viongozi na raia wa kawaida kuheshimu sheria na kuhakikisha wanafanya shughuli zao na kuishi kama sheria zinavyosema.

Ibara ya 13(3) iko wazi kabisa kwamba haki za kiraia au masuala yote yanayohusu haki na au uvunjifu wa haki yataamuriwa na mahakama.

Kama katiba ambayo ndio sheria kuu ya nchi imeamuru hivi, kwa nini mkuu wa wilaya ya Arusha alijichukulia sheria mkononi? Kwa nini mamlaka ya uteuzi iko kimya? Je huyu Dc yuko sawa?

Je, ndio kusema mtuhumiwa awe anapata mob justice hapa Tanzania? Jambo ambalo ni kinyume cha haki za binadamu!
 
Ndio umeamka? Huyo DC ni mmoja kati ya waliofanikisha kura za wizi, hivyo kanogewa kutokuheshimu sheria. Kama ameshiriki kunajisi uchaguzi, atapata shida gani kuchapa watu hadharani kinyume cha sheria?
 
Ndio umeamka? Huyo DC ni mmoja kati ya waliofanikisha kura za wizi, hivyo kanogewa kutokuheshimu sheria. Kama ameshiriki kunajisi uchaguzi, atapata shida gani kuchapa watu hadharani kinyume cha sheria?
Kuwa na heshima we kijana,mimi nilikiwa nimelala? Najua ninachosimamia.
 
Kuwa na heshima we kijana,mimi nilikiwa nimelala? Najua ninachosimamia.

Sio usingizi wa kawaida, ulikuwa usingizi wa pono, ndio maana saa hii umeamka lakini bado mawenge ya usingizi hayajaisha. Eti niwe na heshima, una heshima gani ww muhuni?
 
Sio usingizi wa kawaida, ulikuwa usingizi wa pono, ndio maana saa hii umeamka lakini bado mawenge ya usingizi hayajaisha. Eti niwe na heshima, una heshima gani ww muhuni?
Dah!
 
Kuwaona hawa DC's na Watendaji wengine wanakosea huku tukinyamazia Mmomonyoko wa Kimaadili wa Kijamii uliopo ni kutaka Kuficha tatizo.
 
Back
Top Bottom