Tunapoambiwa kuwa Tanzania inakuwa 'Rebranded' ni vyema pia tukaambiwa nani 'aliichafua', lini na kwa manufaa gani

RAIS MAGUFULI ALIMWEKA "JELA" MAKAMU WAKE SAMIA SULUHU HASSAN

Na Bollen Ngetti

MWANAMUZIKI Ndanda Kosovo aliwahi kuimba, "Jela..jela ni mbaya, jela..jela ni mateso". Ndanda hakukosea. Aliimba uzoefu alioupata jela hapo Ukonga. Ninamuunga mkono Ndanda kwa uzoefu nilioupata nikiwa jela Keko na Segerea. Jela ni mbaya. Ukiwa jela umezungukwa kuta nene ndefu huwezi kuona nje kwa kifupi unakuwa umenyimwa uhuru wako.

Hata hivyo hakuna jela mbaya duniani kuliko hata Gwantanamo kama jela ya fikra. Yani jela ambapo huwezi kutoa mawazo yako hadharani. Hii ni jela mbaya inayojengwa na shetani tu.

Niliwahi kudokezwa huko nyuma lakini sikuandika maana nilikosa ushahidi kwamba kuna wakati Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan alitaka kujiuzulu nafasi ya Umakamu kujiondoa kwenye gereza la fikra lakini wenye hekma na busara walimshauri asifanye hivyo.

Kwa namna Rais Samia Suluhu Hassan alivyoongoza nchi hii kwa siku 100 ni dhahiri alikuwa jela la fikra. Ni ukweli kwamba hakukubaliana na mambo mengi ya Rais Magufuli hata kama leo anasema "Mimi na Magufuli ni kitu kimoja" lakini matendo ni tofauti.

Mama Samia hakukubaliana na uendeshaji wa demokrasia nchini. Alikuwa jela na ilimtesa ndio maana amechukua njia tofauti kuendesha dhana nzima ya demokrasia. Hakuwa na jinsi wala namna. Bila shaka alilia kimya kimya gerezani.

Mama yetu Samia hakupenda uminyaji wa Uhuru wa Habari. Ilimtesa ndio maana "Fundi" alipomwondoa duniani Pombe naye kuchukua hatamu waandishi wa habari wakashangweka. Akaruhusu Uhuru wa Habari na dunia imeshuhudia maana enzi hizo za jela hata andiko hili lisingetoka maana ningekwenda jela la majengo.

Mama Samia hakufurahishwa na kesi za kubumba. Ilimtesa, ilikuwa ni jela kwake ndio maana alipoingia madarakani akafyatua kesi 147 zilizobumbwa na TAKUKURU. Hali hii ilimtesa. Lakini kuachiwa kwa viongozi wa dini wa Uamsho waliosota kwa miaka 9 jela nayo ilimweka jela kisaikolojia Samia. Hakupenda uonevu.

Huyu mama ni swala 5. Ni Muislamu Safi. Hapendi mali za dhulma iwe ni kwa mtu binafsi au Serikali. Hakupenda fedha za dhulma zilizotokana na kesi za kubumba za uhujumu uchumi na ML ndio maana tunaendelea kushuhudia watuhumiwa wakichomolewa magerezani kwa makundi. Lilimuumiza lakini hakuwa na lakufanya maana hakuwa Mkuu wa Maamuzi, Rais. Kitendo cha Mahakama Kuu kuamuru Serikali kurudisha fedha za dhulma kwa kina Mbowe ni ishara nyingine ya kuwa mama yetu aliumia sana kwa matendo hayo. Alikuwa jela.

Makamu wa Rais Samia (sasa Rais) hakupenda watu kuishi kwa hofu na woga. Alitamani watu wawe huru ndani ya nchi yao ila waheshimu Sheria za nchi. Ndio maana leo hata mama lishe, bodaboda nakadhalika wanakwambia, "nchi inafunguka". Wanahisi uhuru walioukosa miaka 5 tuliyoipa kisogo.

Kumbe hata mradi wa Bandari ya Bagamoyo (BEZ) iliyopigwa vita na Pombe ilimkera. Ilimweka jela la kifikra. Hakupenda lakini leo ameamua tufanye mazungumzo mradi ufanyike.

Ndugu zangu, tumuunge mkono Samia kuondokana na gereza la kifikra ili tulisongeshe mbele gurudumu la maendeleo ya nchi.

Binafsi nimejitoa sadaka kumlinda na kumtetea Mama yetu Rais Samia Suluhu Hassan. Mniunge mkono.

Bollen@2021
#MguseMamaNinuke
Wala hustahili kujitokeza kumsemea mhusika, ajitokeze yeye binafsi katika hili hakuna atakayekuunga mkono kwa kuwa wanajamvi na wananchi kwa ujumkla wana uelewa mkubwa tu.

Hilo eneo kuanzia chuo cha Mbegani, Zinga kwa Mtoro, Pande na Kiromo inasemekana watu wameanza kujisajili kulipwa fidia mara mbili. Wamasai na Wamang'ati wanaoishi kwenye pori hilo wanatishiwa kila siku kwamba wahame haraka vinginevyo watachomewa vijumba vya na mifugo-hofu imetanda.

Kuna kitu kimejificha kwenye mradi wa Bagamoyo sio bure mtathibisha hivi karibuni maana wako tayari kutumia nguvu kuuanzisha bila kuzingatia shuku ya dhuluma iliyokuwepo.
 
Aliyejiuzulu katangulia mbele za haki lakini kaacha mambo mengi yanayoongea kwa niaba yake na ndiyo watu wanayoyatumia kumjadili.

Kama makamu alikuwa msaidizi tu ingawa aliona na alibariki kila kitu kwa usaidizi.

Kufanya uchaguzi baada ya rais kutangulia ingekuwa ngumu sana kumbuka gharama za uchaguzi mkuu kwa nchi moja ya afrika.
Katiba imempa yeye nafasi ya urais na limekuwa jambo lilotupitisha vyema kipindi kile kigumu.
Hapo sikubaliani na wewe kabisa, juzi waziri mmoja wa uiengereza amejiuzulu nafasi hiyo baada ya kuenda kinyume na maelekezo ya udhibiti wa UVIKO sembuse makamu? Nyerere alijiuzulu uwaziri mkuu mwaka 1960 kwa kuona alikuwa kwenye nafasi kama kinyago tu.

Hana 'moral authority' ya kuwa 'critic' kwa mtangulizi wake la sivyo laana itamtafuna mpaka mifupa. Kwanini hajaitengua sheria iliyomwingiza makamu wa rais, waziri mkuu, jaji mkuu na spika wa bunge kutoshitakiwa kama kwenli ni mtenda haki?
 
Kwangu mimi Kassim ndio alitakiwa kuwa mtu wa kwanza kujiuzulu huyu ndio mtendaji mkuu wa serikali wa kila siku iweje asiwe anajua kweli? Makamu wa Rais bongo ni "cheo picha" tu

Naungana na wewe 100/100
Kassim Majaliwa angelinda heshma yake kwa kujiuzulu.
Ali fokea Umma.... kuwa Rais yupo busy kazi nyingi,ati tulitaka tumwome anatembea Kariakoo....n.k.
 
Hiyo bado sikuielewa ,

Yaani watanzania tumegeuka bidhaa??

Inawezekana lakini, maana ukute tushauzwa kitambo na hatufahamu Hilo.
 
Naungana na wewe 100/100
Kassim Majaliwa angelinda heshma yake kwa kujiuzulu.
Ali fokea Umma.... kuwa Rais yupo busy kazi nyingi,ati tulitaka tumwome anatembea Kariakoo....n.k.
Hata makamu naye ambaye kwa sasa ndiye mwenye kiti kikuu alifanya ziara Tanga ya siku sita wakati akijua bosi wake anaumwa tena akasema Rais anawasalimu na kwamba waendelee kuchapa kazi wakati akijua sio kweli.
 
Haya ndio maeneo nnayotamani kuona hiyo re-branding itayagusaje?

1. Elimu
2. Uongozi
3. Ulinzi na usalama
4. Afya
5. Ajira

Yapo mambo madogo madogo pia kama Nembo ya Taifa, Rangi za Taifa, vazi la Taifa, Maadili ya kijamii nk.

Kama wadaawa wengine walivyosema. Re-branding ni jambo pana sana na linahitaji watu wa kada mbalimbali kulifanikisha hilo

NAKUPENDA SANA TANZANIA
 
Hapo sikubaliani na wewe kabisa, juzi waziri mmoja wa uiengereza amejiuzulu nafasi hiyo baada ya kuenda kinyume na maelekezo ya udhibiti wa UVIKO sembuse makamu? Nyerere alijiuzulu uwaziri mkuu mwaka 1960 kwa kuona alikuwa kwenye nafasi kama kinyago tu.

Hana 'moral authority' ya kuwa 'critic' kwa mtangulizi wake la sivyo laana itamtafuna mpaka mifupa. Kwanini hajaitengua sheria iliyomwingiza makamu wa rais, waziri mkuu, jaji mkuu na spika wa bunge kutoshitakiwa kama kwenli ni mtenda haki?
Unaumia sana yeye kuwa Rais baada ya JPM kufariki?.

Moral authority anayo na ndio inayomuwezesha kuongea na kufanya anayoyafanya.

Anakuwa critic kwa faida ya Tanzania sio ya mtu mmoja au wawili.

Swali la kwanini hakujiuzulu ni zito sana, hakuna aliyejua kuwa JPM angefariki march 2021 ni mipango ya Mungu.
 
Usilete dharau zako za kijima. Wewe ndio mwenye akili sio na kwamba ndiye unayefahamu kila kitu kilichopo Tanzania na nje ya nchi?

Tafadhali tusikoseani adabu, mind your business if you feel you can't swallow the versatile pill. Respect other's opinions as yours do.
Naona Dawa imekuingia eeeh? Safi sana
 
Unaumia sana yeye kuwa Rais baada ya JPM kufariki?.

Moral authority anayo na ndio inayomuwezesha kuongea na kufanya anayoyafanya.

Anakuwa critic kwa faida ya Tanzania sio ya mtu mmoja au wawili.

Swali la kwanini hakujiuzulu ni zito sana, hakuna aliyejua kuwa JPM angefariki march 2021 ni mipango ya Mungu.
Acha kujipendekeza wewe, unaijua kesho kweli?

Nasisitiza tena hana hiyo 'moral authority' na tafadhali heshimu maoni ya mtu mwingine usilazimishe wengine kukubaliana na hoja yako butu kisa ni mnufaika wake.

Both internal and external resistance will cluster around the beef very soon until the landmark is resumed on track.
 
Acha kujipendekeza wewe, unaijua kesho kweli?

Nasisitiza tena hana hiyo 'moral authority' na tafadhali heshimu maoni ya mtu mwingine usilazimishe wengine kukubaliana na hoja yako butu kisa ni mnufaika wake.

Both internal and external resistance will cluster around the beef very soon until the landmark is resumed on track.
Samia na Magufuli ni kitu kimoja huo ndio ukweli. Wanatekeleza sera zile zile za Chama kile kile.

Ukinasa katika mtego wa personalities utawatenganisha wawili hao ukiutazama mustakabali mzima wa nchi hii hutazifikiria tofauti zao.

Better change your mindset as it is your downfall when it comes to realizing that the fate of our Tanzania is in the hands of this lady at Magogoni and Chamwino.
 
mimi sieliwi tuliambiwa Tanzania imepanda na kufika uchumi wa kati, leo tunaambiwa shuhuli zote zisubiri kwanza tujenge uchumi 🤣 🤣 🤣
 
Leo GENTAMYCINE natoa angalizo kwa wale ambao huko maofisini au katika maeneo mengine mnapokuwa na vyeo vya manaibu (makamu) wa ubosi mkiona wakubwa zenu wanakosea au wanaharibu muwe mnasema mapema au mnaachia ngazi kuliko kuendelea kuwa nao kiutendaji.

Halafu, ama wakistaafu kazi au wakifa ndiyo mnakuja kutuonyesha 'kimafumbo' kuwa mlikuwa hamkubaliani 'kimaamuzi' kwani wenye akili kubwa tutawatafsiri nyie si tu ni wanafiki bali pia mna 'vielementi' vya uchawi pamoja na vya ufitini pia.

Ninaamini message sent and delivered.

Ninachojua rebranding ilianza wakati wa "bonge la kaka".
 
Leo GENTAMYCINE natoa angalizo kwa wale ambao huko maofisini au katika maeneo mengine mnapokuwa na vyeo vya manaibu (makamu) wa ubosi mkiona wakubwa zenu wanakosea au wanaharibu muwe mnasema mapema au mnaachia ngazi kuliko kuendelea kuwa nao kiutendaji.

Halafu, ama wakistaafu kazi au wakifa ndiyo mnakuja kutuonyesha 'kimafumbo' kuwa mlikuwa hamkubaliani 'kimaamuzi' kwani wenye akili kubwa tutawatafsiri nyie si tu ni wanafiki bali pia mna 'vielementi' vya uchawi pamoja na vya ufitini pia.

Ninaamini message sent and delivered.
hata mama samia akimaliza mda wake ajiandae tu kwa maneno kama haya!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom