Tunapingia 2017:Ujumbe wa Martin Luther Jr(AUDIO attcmnt) na maoni yangu kwa Mtu Mweusi Wa Tanzania

MSEZA MKULU

JF-Expert Member
Jul 22, 2011
3,752
5,497
Miongoni mwa Jamii ya watu walionyanyasika na kupitia hali ngumu hapa duniani ni Mtu Mweusi.
Mtu mweusi alikusanywa kama kumbikumbi kutoka moyoni mwa Afrika na kupelewa kutumikishwa Marekani.

Mwaka 1619- Meli kubwa liltia nanga amerika likiwa limejaza Mabibi na Mababu zetu kwenda kutumiwa kama vifaa na sio binadamu wa kuheshimiwa kwa Muda wa miaka 244.

Baadae Mtu mweusi akapitia miaka mingine 100 ya kubaguliwa na kutumikishwa kifikra kama kitu duni, kisicho na akili na tegemezi, Namshukuru Mungu Kwa wazee wetu wakiongozwa na Nyerere walikabidhiwa taifa hili ili angalau tuanze kujisimamia 1961 na hii ilikuwa ni changamoto kubwa kwa mtu mweusi wa Tanzania. Lakini Machozi ya Mtu Mweusi yaliendelea Kumwagika kusini mwa Afrika, Ashukuliwa Mungu kwa Mandera Wakapata nafuu.


Sasa Changamoto inakuja kwa Mtu Mweusi, Pamoja na Watu kama Martin Luther Jr, Malcom x, Mandela, Nyerere na wengine kutoa maisha yao kwa ajili ya mtu mweusi, Bado tukiwa huru ni Wazembe,wavivu, Tunachukiana na kuoneana wivu, tunabaguana, Ubinafsi,Tunahujumiana, tunatesana,Tunauzana na hata tumeamua kuwa tegemezi kwa kodi za binadamu wenzetu ulaya.

FURSA Tanzania zilifunguliwa rasmi 1961 na baadae 1964. tunaenda mwaka wa 56 bado tunajivuta na kujikongoja kama mtu anayeogelea kwenye bwawa la gundi ya maji.

Mwaka huu unaokuja uwe ni Mwaka wa kila mkazi wa Tanzania na Wanajamiiforum wenzangu Tujitafakari na kutumia Fursa zilizopo Kutoka huku tuliko kwama. Hebu dini,siasa,makabila,Matabaka ya kiuchumi yageuzwe kuwa kichocheo cha maendeleo na sio Kamba zinazotuvuta nyuma kwenye dimbwi la chuki,husuda,umasikini na ufukara.

Tukusanye nguvu zetu,zote mmoja mmoja kupambana kwa uwezo wake wote kujikwamua na kukwamua taifa hili, Yawezekana kuna wakati 2017 itakuhitaji usilale siku nzima ili kitu fulani kiende, KESHA. Tulete michango ya kibunifu kwenye familia,vijiji, mikoa na taifa letu. Tujiheshimu na Kuheshimu wengine, Upendo utamalaki miongoni mwetu, Tuushinde ubaya kwa Wema.Dunia inamwaga fursa maelfu mwaka 2017 maelfu zaidi wenda kuliko miaka yote, Usikubali kubaki nyuma Kimbia kwa spidi kuliko aliye mbele yako kielimu,kifedha,kisiasa,kimaendelea fanya kitu kwa Tanzania yako.

Matakwa ya kihistoria hayamuhitaji Mtu mweusi wa tanzania kuangalia nyuma na kutupa lawama kwa Nyerere,Babu yake,Jk,Mwinyi,JPM,Wazazi, Bali chochote tukifanyacho Tufanye kwa bidii zote kana kwamba hutapata Fursa tena. Ni fursa kubwa sana kwa mwanadamu Kuzaliwa Tanzania, na sisi kama watanzania tunapaswa kufanya kazi sio kwa bidii tu (WORK HARD) bali zaidi Kwa Umaridadi (WORK SMART).

Kama ikikuhitaji Graduate Kuuza Vitumbua kutokana na milango ya ajira kufungwa, Uza vitumbua Kwa umakini na bidii kana kwamba hakuna muuza vitumbua mwingine duniani ila wewe.

Wenu
Mseza Mkulu
Katika Kujitafakari Kijijni KIBBUTZ
 

Attachments

  • martin-luther-king-jr-the-dilemma-and-the-challenge (1).mp3
    19.5 MB · Views: 26
Nadhani haina haja ya kuwa na fikra ya utu weusi au kijana. Mawazo hayo ukiyapa kipaumbele ndio yanakuwa visingizio kila mara kwanini tuko nyuma na hatufanikiwi. Bila kujali rangi jambo la msingi ni kufanya kazi kwa bidii na ufanisi. Vile vile ili kuwa na uchumi unaoeleweka kila mmoja afanye kazi kwa kujiajiri au kuajiriwa. Kwa kufanya hivyo uzalishaji na uchumi kwa ujumla (gdp) unakuwa mkubwa na hivyo hata purchasing power inakuwa kubwa hii inavutia wawekezaji zaidi na kuongeza ajira zaidi na mapato ya nchi yanaongezeka na huduma za jamii zinakuwa bora zaidi na hadhi ya maisha inapanda na mambo mengine kama umri wa kuishi afya, furaha n.k.

Tuwaige wa asia kwa kuwa na nidhamu ya kufanya kazi sio kutwa kubeti au kutembea na bahasha kutafuta kazi ilihali kuna fursa kibao.
Heri ya mwaka ujao mwema....

kizazi hiki cha internet tunakila sababu ya kuwa na mafanikio kuliko vizazi vilivyopita...leo wawezajifunza hata kupika mkate kwenye simu yako tu...enzi hizo usingeweza.

Hebu tufunguke tanzania nadhani inaongoza kutumia mitandao ya kijamii afrika lakini zaidi kwa mambo yasiyo na faida wakati jirani zetu wanaongoza kwa kuitumia kwa namna chanya.
 
Sina uhakika kama mtu mweusi ndiye aliyeteswa na mwanadamu mwenzie kuliko wote, labda kwenye modern history...
Zamani watu walikuwa ni monsters wote tu, weupe waliteswa na wenzao, wakafanywa watumwa na kuuwawa kinyama
Wayahudi wameteswa na kupitia shurba nyingi mno
 
Sina uhakika kama mtu mweusi ndiye aliyeteswa na mwanadamu mwenzie kuliko wote, labda kwenye modern history...
Zamani watu walikuwa ni monsters wote tu, weupe waliteswa na wenzao, wakafanywa watumwa na kuuwawa kinyama
Wayahudi wameteswa na kupitia shurba nyingi mno
Umenena vyema lakini nadhani point ya msingi ya mwandishi suluba kubwa aliyoipata mtu mweusi na fedhena kubwa nadhini ni ile kutumikishwa kama mtumwa (slavery) manaake of all things jambo hili lili~undermine sana human dignity to a larger extent
 
Umenena vyema lakini nadhani point ya msingi ya mwandishi suluba kubwa aliyoipata mtu mweusi na fedhena kubwa nadhini ni ile kutumikishwa kama mtumwa (slavery) manaake of all things jambo hili lili~undermine sana human dignity to a larger extent
slaves walikuwepo kabla hata ya wakoloni na waarabu kuja Africa, Enzi za utawala wa Rumi utumwa wa kinyama ulikuwepo sana tu..kati ya weupe kwa weupe
Sema blacks wana tatizo la attitude na kujiona wameonewa kuliko yoyote
 
slaves walikuwepo kabla hata ya wakoloni na waarabu kuja Africa, Enzi za utawala wa Rumi utumwa wa kinyama ulikuwepo sana tu..kati ya weupe kwa weupe
Sema blacks wana tatizo la attitude na kujiona wameonewa kuliko yoyote
Ujue slavery as a mode kwa Africans ilikuwa so extreme na Africans tuache masihara watumikishwa balaa
 
Back
Top Bottom