Tunapenda sana kukuza mambo, naona kabisa hii kesi Mama hakuwa na details nayo. Haijui!

Prof Koboko

JF-Expert Member
Aug 15, 2020
350
2,549
Hey, asalaam alaykm! Kwema kabisa comrades na makamanda humu?

Kwa jicho langu lenye uoni wa mbali naona kabisa Mama hakua na details na hii kesi inayomkabili mwanasiasa mkubwa na mkongwe nchini Kamanda Mbowe na wenzake. Kwa alivyokua akihojiwa na BBC, majibu aliyoyatoa kwa haraka haraka unaona kabisa kua yeye alikua mtu wa kusimuliwa tu lakini siyo kwamba alikua anajua nature na source ya hii kesi. Naona kabisa master minds wa hii kesi ni watendaji ambao kimsingi walianza maandalizi toka 2020 ambapo yawezekana yeye alikua hajui kabisa.

Kwa ushahidi unaotolewa mpaka sasa kwa Mama alivyo na huruma kama mwanamke, inaonekana kabisa haifurahii hii kesi lakini anafungwa na kitu kimoja tu cha kwamba ule ni mhimili mwingine yeye hana maamuzi nao, anachosubiri ni kuona mahakama inatenda haki.Hata yeye kama muumini safi wa dini ya Kiislam naamini anajua kabisa hii kesi ni ya kutunga yenye lengo la kumkomoa mtu.

Mtihani mkubwa ni kwa DPP aliyepo ambaye kwangu mimi mpaka sasa naamini ni mtu anayependa haki, naye naona hakua anaijua hii kesi chanzo chake ameamua naye kuitazama mwenendo wake hadi mwisho na ndiyo maana amejali muda kwa kuipeleka mahakamani haraka ili maamuzi yafanyike na haki ya mtu ipatikane. Ukitaka kujua kua hata yeye DPP ameistukia hii kesi, angalia kuna ushahidi wa madawa ya kulevya lakini hayapo kwenye hati ya mashtaka.

Huu mzigo inaonekana kabisa ni wa kina Kingai,DCI Mstaafu na timu yake na hawa inaonekana wanajua kabisa hii kitu ni wapi inaanzia. Haiwezekani kuna watu wanaotajwa kama viungo kwenye hii kesi kina Sabaya,Kaaya na ASP Jumanne mpaka sasa wana walishakumbwa na tuhuma za utovu wa nidhamu na tuhuma za unyang'anyi tena wengine wanashughulikia vifungo. Hawa wote niliowataja watatu walitajwa kua walikua na shutuma za utapeli.

Walishindwa nini kutengeneza kesi za uongo? DCI mstaafu, Kingai na wengine nani atawaamini? Ushahidi wanaoutoa mahakamani unatofautiana kwa kiasi kikubwa sana, haihitaji digirii kujua kua hii kesi ni ya kuchonga.

Ninachoomba na ndicho pekee cha muhimu, Mahakama itende haki pasina kumuonea wala kumuogopa Mtu. Hii kesi ni maarufu, ikihukumiwa kwa misukumo flani yenye hisia za kisiasa madhara yake ni makubwa nchini mno.

Tunafahamu Sekeseke la Masheikh la uamsho lilivyoitesa serikali, Mbowe si mtu mdogo,ukitaka kulijua hilo fika mahakamani uone ni kina nani wanahudhuria kusikiliza kesi yake.

Sina sababu ya kumlaumu na kumshambulia Mama kwenye hii kesi. Wakutazamwa na kulaumiwa ni watendaji wa chini yake akiwemo IGP hawezi pia kukwepa lawama hizi na hata akistaafu Mbowe akiwa gerezani lawama hazitamuacha salama.
 
Kama hakuwa na details kwanini akaenda BBC kwenye ile interview na kusema wana ushahidi wa kutosha kumfunga Mbowe?

Au baada ya kuona amepotoshwa akapotea ndio akaamua kumzawadia yule jaji cheo ili amsaidie kufukia mashimo yake aliyotengeneza kwenye ile interview?

Kama hilo hapo juu sio kweli, anajiamini kwa alichosema kwenye ile interview na ana waamini wasaidizi wake waliomwambia wana ushahidi wa kumfunga Mbowe, kwanini asingesubiri yule jaji amalize kusikiliza ile kesi ndio ampe zawadi ya cheo?

Naona hapa Rais alikubali amepotoshwa na akapotea, ndio maana akawahi kujitengenezea njia kwa kutoa cheo ili asiaibike siku ya hukumu, lakini bado haitoshi, aibu hii itamuandama tu, kwa ushahidi ule unaotolewa na mashahidi wa jamhuri unaonesha dhahiri hakuna kesi pale, wanalazimisha tu.
 
Kila nikitafakari nahisi Kingai na Mahita sio watu wakawaida. Nadhani ni vizazi vya laana. Ila Hakuna jiwe litakalosimama. Daima. Kila jiwe litaangushwa. Kwasasa kina Kingai wanajiona salama japo mioyo inawauma ila malipo yapo tu na ni hapa hapa ulimwenguni.

Kingine kama Kina Mbowe kama watakuwa na kesi ya kujibu na ndivyo itakavyokuwa kutokana na mwenendo wa Jaji, basi IGP ajiandae kutoa ushahidi wake na hili jambo litamshusha sana credit yake kuliko hata hapa alipo.
 
Rais hapaswi kua mropokaji. Alishindwa nini kukataa kujibu swali hilo na kusema tuu liko mahakani na tuiachie mahakama?.

Yeye ni zao la mfumo onevuu na kandamizii, anajua kabisaa jinsi chama chake na serikali vinavyo onea watu, alishindwa nini kua na subra ili ajue ukweli wote ndio atoe kauli?.

Manafiki.
 
Kama hakuwa na details kwanini akaenda BBC kwenye ile interview na kusema wana ushahidi wa kutosha kumfunga Mbowe?

Au baada ya kuona amepotoshwa akapotea ndio akaamua kumzawadia yule jaji cheo ili amsaidie kufukia mashimo yake aliyotengeneza kwenye ile interview?

Kama hilo hapo juu sio kweli, anajiamini kwa alichosema kwenye ile interview na ana waamini wasaidizi wake waliomwambia wana ushahidi wa kumfunga Mbowe, kwanini asingesubiri yule jaji amalize kusikiliza ile kesi ndio ampe zawadi ya cheo?

Naona hapa Rais alikubali amepotoshwa na akapotea, ndio maana akawahi kujitengenezea njia kwa kutoa cheo ili asiaibike siku ya hukumu, lakini bado haitoshi, aibu hii itamuandama tu, kwa ushahidi ule unaotolewa na mashahidi wa jamhuri unaonesha dhahiri hakuna kesi pale, wanalazimisha tu.
Hivi unaelewa maana ya taarifa za kuandaliwa? Alichozungumza ni hicho alichambiwa kuhusu kesi. I'm sure 100% alitegemea swali kama hilo toka BBC
 
Rais hapaswi kua mropokaji. Alishindwa nini kukataa kujibu swali hilo na kusema tuu liko mahakani na tuiachie mahakama?.

Yeye ni zao la mfumo onevuu na kandamizii, anajua kabisaa jinsi chama chake na serikali vinavyo onea watu, alishindwa nini kua na subra ili ajue ukweli wote ndio atoe kauli?.

Manafiki.
Angekataaje kujibu swali wakati alikua na majibu hata kama si ya kuridhisha?
 
Hivi unaelewa maana ya taarifa za kuandaliwa? Alichozungumza ni hicho alichambiwa kuhusu kesi. I'm sure 100% alitegemea swali kama hilo toka BBC
Naona nawe unakubali alipotoshwa akapotoka, sasa kwanini Rais asijiridhishe na majibu anayopewa na wasaidizi wake kwanza kabla hajaenda kuongea public halafu baadae yanamletea shida?

Matokeo yake anajikuta anatoa rushwa ya cheo ili afichiwe aibu wakati nae akisimama majukwaani anasema rushwa ni adui wa haki.

#Hafai.
 
Kimsingi wakati wa utawala wa Magu watendaji wengi na hasa upande wa vyombo vya ulinzi na usalama waliwafanyia waTz mambo mengi sana ambayo siyo ya kiutu, hivyo mashaka yao ni kwamba wangeacha haki za kiraia, kisiasa na kidemokrasia zitawale uovu wao ungewekwa hadharani na pengine kutakiwa kuwajibishwa kwa waliyoyafanya na hili nadhani ndilo lililotufikisha hapa tulipo sasa.

Mama naye kwenye mahojiano ya BBC alichemka, hivyo anaona shida kula matapishi yake mwenyewe , na hivyo naona amechagua bora nchi igawanyike kuliko kuifuta hii kesi ya kutunga.

Huwa nafuatilia hutuba za mama , ukisoma saikolojia ya mama na body language wakati anahutubia unaona anamhukumu Mbowe kwa kumkosea adabu au kuonyesha kutotambua/kuheshimu mamalaka aliyo nayo na hivyo kutuma signal kwa Mbowe na wengine kwamba nafasi ile inaweza kukufanya chochote inachotaka kupitia vyombo vyake na usifanye chochote.

Nafasi hii ya uraisi inataka mtu aliyejaa hekima, busara na hofu ya mungu (katika kutenda na siyo kwa kuongea tu kama yule kiongozi wa malaika) vinginevyo mateso katika taifa hili hayatakuja kuisha.
 
Nakazia Mahita jr na Kingai ni vizazi vya laana na huyo Mahita mpaka kufikia hapo ni kwa kubebwa na juhudi za ushawishi alizonazo Mahita sn kwenye hilo jeshi ovu

Na ndo ule usemi kuwa jeshi limejaa watoto wa kota hii ndo maana yake halisi
 
Kifupi mama mwenyewe anataka Mbowe afungwe jela ili yeye apite kiulaini 2025, maana uwepo wa Mbowe uraiani utachochea madai ya katiba mpya na tume huru ya uchaguzi. Kitu ambacho mama anajua ni hatari kwake. Kama Magufuli mwenyewe na umaarufu wake wote hakushinda kwenye chaguzi zote 2, mama ndo hatoboi kabisa. Ukiangalia trend ya mambo ya tozo,kupanda mafuta, machinga ...mama anazidi kuchukiwa hasa.

Uchaguzi wa 2025 upinzani utashinda kwa kishindo kuliko muda wowote. Watapata kura zaidi ya 65% Kitu kitakachoendelea ni matumizi makubwa ya dola na uporaji wa waziwazi. Mipango ni mama akishaapishwa tena, baada ya hali ya hewa kutulia ndo atoe "msamaha" kwa Mbowe. Au Mbowe aachiwe "ashinde" kesi yake ya rufaa wakati huo uchaguzi ulishapita na mama ameapishwa kimazabe. Tunza hii hii msg yangu kichwani. You will see
 
Yaani sikusoma hadi mwisho kwa hasira, iweje umtoe jwa kusema eti mama hawezi kuingilia kwani ni mhimili mwingine?
Hiyo kesi sio ya Mahakama bali ni ya serikali (DPP) na huyo yuko katika mamlaka ya Executive yaani chini ya Rais hivyo alikuwa na uwezo wa kuagiza aondoe mashtaka hayo ya kubumba badala ya kumuacha Mbowe aendelee kutaabika eti mahakama itauona ukweli!
Hawa ndio kesho mambo yakiwageukia wao wanabaki kuomba huruma.
Au anadhani yeye atahutumiwa kwa jinsia yake?
 
Yaani sikusoma hadi mwisho kwa hasira, iweje umtoe jwa kusema eti mama hawezi kuingilia kwani ni mhimili mwingine?
Hiyo kesi sio ya Mahakama bali ni ya serikali (DPP) na huyo yuko katika mamlaka ya Executive yaani chini ya Rais hivyo alikuwa na uwezo wa kuagiza aondoe mashtaka hayo ya kubumba badala ya kumuacha Mbowe aendelee kutaabika eti mahakama itauona ukweli!
Hawa ndio kesho mambo yakiwageukia wao wanabaki kuomba huruma.
Au anadhani yeye atahutumiwa kwa jinsia yake?
Ww subiri ,hukumu itoke .Unapoanza kutoa hukumu ,wakati kesi bado,unatupeka kwenye hisia zako.Acha kesi ilindime ndugu.
 
29 Reactions
Reply
Back
Top Bottom