fyddell
JF-Expert Member
- Dec 19, 2011
- 11,108
- 19,985
Hivi viatu ni vizito kwakweli. Mungu ana maana yake ya kutomchukua Lissu katika shambulio lile la kikatili.Wasalaam wapendwa!
Kila mara humu mtu ukisoma vizuri comments za kila mada huwezi kupita bila kukutana na neno UNAFKI. Hili neno linasemwa kulingana na sisi wenyewe tulivyo na vitabia vyetu.
Hivi Tundu Lissu kabla haijapigwa risasi akachungulia kaburi na kurudi tuwahi kusikia akiitwa msaliti na nani?
Hebu vaa viatu vyake chukulia kua wewe ni tundu Lissu,
1. Upigwe risasi 16 saa 7 mchana kweupe na mpaka leo hii wasijulikane waliotenda tukio hilo
2. Chukulia wewe ndio Tundu Lissu unyimwe gharama za matibabu yako kama mbunge bila sababu yeyote ya msingi
3. Chukulia wewe ndio Tundu Lissu mpaka leo unyimwe nafsi yako ya ubunge na stahiki ziingine
4. Chukulia hii wewe ni Tundu Lissu unaporwa ubunge wako hadharani bila sababu ya msingi
6. Chukulia wewe ndio yeye unapata matatizo watu wanazuiwa hata kukusanyika kukuombea kwa Mola upone
6. Chukulia wewe ni Tundu Lissu unaarifiwa na vyanzo vya ndani ya mfumo kama asemavyo yeye kua ilitolewa amri kua shughuli ilitakiwa imalizike mapema kisha apumzishwe haraka kijijini kwao mapema bila kuagwa, hivi kwa maneno haya upendo utoke wapi?
Tunaomwita Lissu mtumwa wa Mabeberu hebu mfikirieni na yeye kwa vyote aliyofikia nayo. Mbona hatukumwita msaliti kabla? Hivi yeye si binadamu na asinune wala kuchukua ana moyo wa chuma?