Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Kwa wale wanaojua masuala ya uhandisi wa ndege pamoja na kuzitunza, wataelewa kwamba hakuna kitu chenye gharama kubwa kama kupaki ndege bila kuitumia. Unapokuwa na ndege ni lazima itumike karibu kila wakati. Gharama za kuitunza ndege iliyopaki ni kubwa sana.
Tulikuwa na shamrashamra za kununua ndege ambapo tuliambiwa sasa ndege za ATCL zimefikia zaidi ya 10. Hatukutarajia kukumbwa na blaa la Corona lililozuia usafiri hasa wa kimataifa na kiasi wa ndani ya nchi.
Sasa kama wananchi wenye uchungu na kodi zetu, tungependa kufahamishwa gharama za kila mwezi tunazoingia kwa kupaki ndege za ATCL kutokana na ugonjwa wa Corona.
Na pia tungependa kujua tangu tatizo hili liikumbe dunia, ATCL imeingia gharama na hasara za kiasi gani kwa kupaki ndege zake.
Tulikuwa na shamrashamra za kununua ndege ambapo tuliambiwa sasa ndege za ATCL zimefikia zaidi ya 10. Hatukutarajia kukumbwa na blaa la Corona lililozuia usafiri hasa wa kimataifa na kiasi wa ndani ya nchi.
Sasa kama wananchi wenye uchungu na kodi zetu, tungependa kufahamishwa gharama za kila mwezi tunazoingia kwa kupaki ndege za ATCL kutokana na ugonjwa wa Corona.
Na pia tungependa kujua tangu tatizo hili liikumbe dunia, ATCL imeingia gharama na hasara za kiasi gani kwa kupaki ndege zake.