MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Ninyi watu hebu tutumie akili kwa kina kutazama katika hili tusifikiri juu juu, tunapolilia katiba mpya ilihali ambaye anatakiwa kuusimamia mchakato wake Mh Rais amesema kua kwake sio kipaumbele tutegemee nini?
Anyway, tuseme ndio amekubali, mnafikiri kama bunge tu la jamhuri ya Muungano limedhibitiwa itawezekanaje wakashindwa kudhibiti kitaasisi kidogo tu cha kusimamia mchakato huu? Mnafikiri hata jaji warioba akirudi kuusimamia mchakato upya ataongea kitu gani? atabadili kitu gani?
Yaani wajumbe wa tume ya kukusanya naoni wanateuliwa na Rais,wajumbe wa bunge la katiba wanateuliwa na Rais, mwenye maamuzi ya mwisho ya katiba iweje ni Rais mtegemee tupate katiba ya wananchi kweli yenye sura ipi?
Hapa yalitakiwa maridhiano ya kitaifa kuhusisha sehemu zote za uwakilishi wa wananchi,watu watumie busara kukamilisha kupanga taswira ya taifa letu la baadae na vizazi vijavyo. Bila ya hivyo tukitaka kumlazimisha Mh Rais juu ya katiba mpya haitasaidia kitu.
Inashangaza sana kama kuna hata viongozi wa dini wanatoka hadharani kuutangazia umma kua hakuna haja ya katiba ilihali wanaona kabisa kua hali si shwari ni hatari sana, hawa viongozi wa dini ni wa kukemewa kabisa tena wanatakiwa wapumzike huwahudumia kondoo wao kwa maana akili zao zimekwisha choka. Hawa ni lazima tuwaone kama wasaliti wa kiimani
Tanzania ya viwanda, kwa katiba hii iliyo na mfumo wa kizamani wa katiba haiwezi kufikiwa kamwe, tutazame sasa ni miaka miwili ya utawala huu wa awamu ya 5 kuna kipi kikubwa zaidi ya ugumu wa maisha kwa raia wasiojua hili wala lile? Viwanda vinavyosemwa vimeongezeka iko wapi impact yake? Vinatengeneza nini? Vinavyotengenezwa vinauzwa nchi gani? Tuweni maskini sana tunakoelekea kunatia shaka sana.
Washauri wetu wa masula ya kijamii,kiuchumi na kisiasa wametugeuka! Wanatazama mahitaji yao binafsi wanaongopa kuusema ukweli wa mambo wanasubiri tu tuharibikiwe ndio wazungumze pengine.
Anyway, tuseme ndio amekubali, mnafikiri kama bunge tu la jamhuri ya Muungano limedhibitiwa itawezekanaje wakashindwa kudhibiti kitaasisi kidogo tu cha kusimamia mchakato huu? Mnafikiri hata jaji warioba akirudi kuusimamia mchakato upya ataongea kitu gani? atabadili kitu gani?
Yaani wajumbe wa tume ya kukusanya naoni wanateuliwa na Rais,wajumbe wa bunge la katiba wanateuliwa na Rais, mwenye maamuzi ya mwisho ya katiba iweje ni Rais mtegemee tupate katiba ya wananchi kweli yenye sura ipi?
Hapa yalitakiwa maridhiano ya kitaifa kuhusisha sehemu zote za uwakilishi wa wananchi,watu watumie busara kukamilisha kupanga taswira ya taifa letu la baadae na vizazi vijavyo. Bila ya hivyo tukitaka kumlazimisha Mh Rais juu ya katiba mpya haitasaidia kitu.
Inashangaza sana kama kuna hata viongozi wa dini wanatoka hadharani kuutangazia umma kua hakuna haja ya katiba ilihali wanaona kabisa kua hali si shwari ni hatari sana, hawa viongozi wa dini ni wa kukemewa kabisa tena wanatakiwa wapumzike huwahudumia kondoo wao kwa maana akili zao zimekwisha choka. Hawa ni lazima tuwaone kama wasaliti wa kiimani
Tanzania ya viwanda, kwa katiba hii iliyo na mfumo wa kizamani wa katiba haiwezi kufikiwa kamwe, tutazame sasa ni miaka miwili ya utawala huu wa awamu ya 5 kuna kipi kikubwa zaidi ya ugumu wa maisha kwa raia wasiojua hili wala lile? Viwanda vinavyosemwa vimeongezeka iko wapi impact yake? Vinatengeneza nini? Vinavyotengenezwa vinauzwa nchi gani? Tuweni maskini sana tunakoelekea kunatia shaka sana.
Washauri wetu wa masula ya kijamii,kiuchumi na kisiasa wametugeuka! Wanatazama mahitaji yao binafsi wanaongopa kuusema ukweli wa mambo wanasubiri tu tuharibikiwe ndio wazungumze pengine.