Moringe Sokoine1
Member
- Sep 5, 2015
- 80
- 73
Inakera sana kusikia wapinzani wakibeza na kupotosha historia yetu kama taifa kuwa kwa takribani nusu karne sasa Tanzania haijafanya lolote chini ya chama tawala,CCM. Huu ni upotoshaji mkubwa wa kumbukumbu na historia ya nchi kule tulikotoka, tulipo na tuendako.Kila mtanzania mwenye,akili na masikio anayaona,anayasikia na anayasoma mambo yaliyofanywa na serikali za awamu zote nne zilizotuongoza. Nitadhibitisha kwa uchache ili kuweka mambo sawa.
Moja ya kazi kubwa na kujivunia ni Umoja,amani,ulinzi na usalama. Mambo haya yamesimamiwa vizuri sana na kama taifa tumeendelea kubaki kuwa wamoja,tunaopendana licha ya tofauti zetu za rangi.dini,makabila,mahali tulikotoka na ufuasi wa vyama vyetu. Hivyo Tanzania imeendelea kuwa kisiwa cha amani na kimbilio la wengi majirani ambao nchi zao zimepata machafuko. Hata hili tunabeza,basi watuambie wapi panatufaa zaidi.
Pili,Ni suala la kudumisha na kuimarisha muungano wetu adhimu na adimu barani Afrika. Mpaka sasa viongozi wetu wameendelea kuwa na utashi wa kisiasa katika kuona muungano unastawi vizuri zaidi kwa manufaa ya wananchi wa pande zote mbili na mpaka sasa zimebaki kero nne tu toka 13 zilizokuwepo mwaka 2005. Hata hivyo kupatikana kwa muafaka wa kisiasa kule Zanzibar kupitia kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa kumeendelea kuupa nguvu zaidi Muungano na kuwafanya wananchi kuishi kwa amani.
Tatu, Mbali na kutawaliwa kwa miaka 75 na wakoloni lakini mpaka tunapata uhuru mawasiliano nchini kwetu yalikuwa duni sana maeneo machache kupitia posta yaani unaandika barua ambayo ilichukua hadi miezi mitatu kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine. Simu za mezani ambayo nayo ilikuwa inachukua muda sana. Tulituma pesa kupitia posta au magari ambayo ilikuwa taabu kweli. Leo nusu karne tunayobezwa serikali imeweka mazingira rafiki yaliyovutia uwekezaji wa sekta binafsi katika mawasiliano na hadi sasa zaidi ya watanzania milioni 26.7 wanatumia simu za mkononi. Kuimarika kwa mawasilano nchini kumepelekea huduma nyingi sana kufanyika kupitia simu mbali na kuwasiliana, leo unatuma pesa,unanua,unauza na unalipia huduma mbalimbali kupitia simu ya mkononi popote ulipo. Unapokea taarifa za hali ya hewa,bei za mazao katika masoko mbalimbali na hata kuperuzi mitandao. Hakika ni hatua kubwa sana.
Nne,Wigo wa upatikanaji elimu nchini umeongezeka sana. Leo kumpata mfanyakazi wa ndani ni shughuli kweli kweli yote sababu ya shule za sekondari za kata. Tulipata uhuru tukiwa hatuna chuo kikuu hata kimoja. Kabla ya Serikali ya awamu ya kwanza kuamua kutumia jengo la TANU kama chuo kikuu huku wakijenga majengo ambapo ndio leo tunakiita Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam. Lakini Leo Tunavyo vyuo vikuu vikubwa na bora 11 vya umma. Wanaobeza wamepita humu humu kwenye kazi zilizofanyika. Kubwa zaidi serikali ikabuni mfumo wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu ili watoto wa watanzania maskini nao wasijekuikosa fursa hii ya elimu ya juu.
Tano, Ujenzi wa miundombinu ya barabara za lami kumeifungua sana nchi yetu; kati ya mikoa kwa mikoa,wilaya kwa wilaya na maeneo yote ya mipakani na nchi jirani. Hapa kazi kubwa ilifanyika kwani katika kutawaliwa miaka 75 na wakoloni walijenga kilomita 1300 za lami mbali na uvunaji mkubwa wa maliasili zetu lakini ndani ya nusu karne serikali imejenga barabara za lami zenye urefu wa kilomita 17,742. Kazi hii ikisimamiwa na DK.MAGUFULI ambaye leo ndiye RAIS ajaye chini ya CCM.
Mwisho, Ni kuimarika kwa uzalishaji na uboreshaji wa miundombinu ya umeme nchini. Leo serikali imewekeza katika vyanzo mbadala vya kuzalisha umeme kama vile gesi, upepo na makaa ya mawe ambapo ni muda mfupi tu ujao umeme wa uhakika tena wa gharama nafuu utakuwa umepatikana. Ujenzi wa bomba la gesi umekamilika na mitambo ya kuchakata gesi imekamilika na hata baadhi yao imeanza kuwashwa kuanza kuzalisha umeme zoezi ambalo wataalamu wa TANESCO wamesema litamalizika kabla ya mwisho wa mwezi Oktoba mwaka huu. Hapa gharama za umeme zitashuka sana kutoka dola senti 42 za kimarekani kwa uniti moja ya umeme hadi dola senti 5-8 za kimarekani. Hivyo watumiaji wa umeme sasa wanakaa mkao wa kula. Pia usambazaji wa umeme vijijini umeendelea kufanyika kwa kasi sana kwani tulipata uhuru huku 2.8% ya watanzania walikuwa wanatumia umeme leo ni 36% ya watanzania huku ilani ya CCM 2015-2020 ikieleza kuwafikishia huduma hii muhimu 60% ya watanzania waishio vijijini ifikapo 2020.
Haya ni machche tu; Hivyo nashauri kusaka kura kusiwe kisingizio cha kufuta maendeleo yaliyopatikana. Ila ifahamike kukubali mafanikio ni ustaarabu na kukiri changamoto na kueleza namna ya kuzikabili ni uongozi.
Tutafakari kabla ya kuamua. Tuepuke mihemko na ushabiki ili tuamue kwa usahihi.
Moja ya kazi kubwa na kujivunia ni Umoja,amani,ulinzi na usalama. Mambo haya yamesimamiwa vizuri sana na kama taifa tumeendelea kubaki kuwa wamoja,tunaopendana licha ya tofauti zetu za rangi.dini,makabila,mahali tulikotoka na ufuasi wa vyama vyetu. Hivyo Tanzania imeendelea kuwa kisiwa cha amani na kimbilio la wengi majirani ambao nchi zao zimepata machafuko. Hata hili tunabeza,basi watuambie wapi panatufaa zaidi.
Pili,Ni suala la kudumisha na kuimarisha muungano wetu adhimu na adimu barani Afrika. Mpaka sasa viongozi wetu wameendelea kuwa na utashi wa kisiasa katika kuona muungano unastawi vizuri zaidi kwa manufaa ya wananchi wa pande zote mbili na mpaka sasa zimebaki kero nne tu toka 13 zilizokuwepo mwaka 2005. Hata hivyo kupatikana kwa muafaka wa kisiasa kule Zanzibar kupitia kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa kumeendelea kuupa nguvu zaidi Muungano na kuwafanya wananchi kuishi kwa amani.
Tatu, Mbali na kutawaliwa kwa miaka 75 na wakoloni lakini mpaka tunapata uhuru mawasiliano nchini kwetu yalikuwa duni sana maeneo machache kupitia posta yaani unaandika barua ambayo ilichukua hadi miezi mitatu kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine. Simu za mezani ambayo nayo ilikuwa inachukua muda sana. Tulituma pesa kupitia posta au magari ambayo ilikuwa taabu kweli. Leo nusu karne tunayobezwa serikali imeweka mazingira rafiki yaliyovutia uwekezaji wa sekta binafsi katika mawasiliano na hadi sasa zaidi ya watanzania milioni 26.7 wanatumia simu za mkononi. Kuimarika kwa mawasilano nchini kumepelekea huduma nyingi sana kufanyika kupitia simu mbali na kuwasiliana, leo unatuma pesa,unanua,unauza na unalipia huduma mbalimbali kupitia simu ya mkononi popote ulipo. Unapokea taarifa za hali ya hewa,bei za mazao katika masoko mbalimbali na hata kuperuzi mitandao. Hakika ni hatua kubwa sana.
Nne,Wigo wa upatikanaji elimu nchini umeongezeka sana. Leo kumpata mfanyakazi wa ndani ni shughuli kweli kweli yote sababu ya shule za sekondari za kata. Tulipata uhuru tukiwa hatuna chuo kikuu hata kimoja. Kabla ya Serikali ya awamu ya kwanza kuamua kutumia jengo la TANU kama chuo kikuu huku wakijenga majengo ambapo ndio leo tunakiita Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam. Lakini Leo Tunavyo vyuo vikuu vikubwa na bora 11 vya umma. Wanaobeza wamepita humu humu kwenye kazi zilizofanyika. Kubwa zaidi serikali ikabuni mfumo wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu ili watoto wa watanzania maskini nao wasijekuikosa fursa hii ya elimu ya juu.
Tano, Ujenzi wa miundombinu ya barabara za lami kumeifungua sana nchi yetu; kati ya mikoa kwa mikoa,wilaya kwa wilaya na maeneo yote ya mipakani na nchi jirani. Hapa kazi kubwa ilifanyika kwani katika kutawaliwa miaka 75 na wakoloni walijenga kilomita 1300 za lami mbali na uvunaji mkubwa wa maliasili zetu lakini ndani ya nusu karne serikali imejenga barabara za lami zenye urefu wa kilomita 17,742. Kazi hii ikisimamiwa na DK.MAGUFULI ambaye leo ndiye RAIS ajaye chini ya CCM.
Mwisho, Ni kuimarika kwa uzalishaji na uboreshaji wa miundombinu ya umeme nchini. Leo serikali imewekeza katika vyanzo mbadala vya kuzalisha umeme kama vile gesi, upepo na makaa ya mawe ambapo ni muda mfupi tu ujao umeme wa uhakika tena wa gharama nafuu utakuwa umepatikana. Ujenzi wa bomba la gesi umekamilika na mitambo ya kuchakata gesi imekamilika na hata baadhi yao imeanza kuwashwa kuanza kuzalisha umeme zoezi ambalo wataalamu wa TANESCO wamesema litamalizika kabla ya mwisho wa mwezi Oktoba mwaka huu. Hapa gharama za umeme zitashuka sana kutoka dola senti 42 za kimarekani kwa uniti moja ya umeme hadi dola senti 5-8 za kimarekani. Hivyo watumiaji wa umeme sasa wanakaa mkao wa kula. Pia usambazaji wa umeme vijijini umeendelea kufanyika kwa kasi sana kwani tulipata uhuru huku 2.8% ya watanzania walikuwa wanatumia umeme leo ni 36% ya watanzania huku ilani ya CCM 2015-2020 ikieleza kuwafikishia huduma hii muhimu 60% ya watanzania waishio vijijini ifikapo 2020.
Haya ni machche tu; Hivyo nashauri kusaka kura kusiwe kisingizio cha kufuta maendeleo yaliyopatikana. Ila ifahamike kukubali mafanikio ni ustaarabu na kukiri changamoto na kueleza namna ya kuzikabili ni uongozi.
Tutafakari kabla ya kuamua. Tuepuke mihemko na ushabiki ili tuamue kwa usahihi.