Tunamsaka RAIS WA 2015: Ulimboka STYLE au Zitto STYLE..

TAMKO

JF-Expert Member
Oct 11, 2011
1,090
762
Ndogu Watanzania wenzangu..

hususan watu makini nguli wa mitazamo humu Jamvini, tutafakari hili kwa uzito unaostahili, Tanzania Tuliyonayo leo, Tanzania iliyopoteza Muelekeo, Tanzania tajiri iliyobatizwa jina la maskini, Tanzania inayoongozwa na makatili, wauaji, watu wa Damu , wasiojali utaifa wala wataifa, inahitaji Raisi mpya 2015. na raisi wetu tuangalie je ni kweli bado tunahitaji raisi mwenye mlengo wa Ulimboka style au Zito Style?.

Kifupi Ulimboka style of President candidate ni mtu mwenye vitu Vingi vya kupoteza, ni jasiri wa kuanzisha au kuibua hoja nzito lakini si jasiri wa kuziendeleza hadi ukomo, akitishiwa kidogo huftata mkia akaogopa kutulia kwa kuhofia kupoteza malavidavi ya mkewe, watoto, familia, nyumba, mali, kazi eeee na mengi tu. Utaskia "bora ujikalie kimywa mkeo asijekuwa mjane bure..watoto wako watasomeshwa na nami au watakuwa wanamwita dady!!Dady!! nani?, he mkeo ataolewa na jamaa zako na mali zako jamaa waliomuoa mkeo wataziinjoi na hao jamaa zako au mkeo atawalazimisha watoto wako wawaite dady!! wewe ukiozea udongoni!!" sentensi kama hizo lazima zimpate na tusimlaumu sana akizithamini, Ukombozi wa Taifa letu unahitaji mtu hasa wa kujitoa sio hizi blabla.


Zitto style of President candidate ni mtu asiye vitu Vingi vya kupoteza, ni jasiri wa kuanzisha au kuibua hoja nzito akazisimimamia bila kuangalia uso mbuzi wa mtu. sisemi kwamba Zitto ana wasifu wa namna hii lakini kidogo anakaribia, si kama Mtu ambaye usiku anaambiwa na mkewe "Honey achana nao hao watakufanya nijiskie mnyonge wakikuua, je wewe unapenda kitanda hiki Deo aje akilalie na kuninanihii wewe ukifa?, je unapenda malavidavi yote haya nije kumgawia Mwaikonde wewe wakikuasasinate, achana nao honey tulee watoto wetu"..Hoja yangu naikita zaidi kufikiria kwamba yamkini tunahitaji candidate ambaye hana Mke wala watoto kwa sasa, Jasiri asiyeogopa, mwenye uzalendo wa kweli..

sred zangu, na mamia ya post zangu humu JF nimekuwa nikiwapinga vikali viongozi sampuli ya Zitto, kwa kijimsemo kwamba kama huna familia unayoiongoza (hasahasa mke na watoto) utawezaje kuongoza jamii, lakini kwa sasa tukio la ulimboka kutekwa na kupigwa na watu ANAOWAJUA yeye Ulimboka, hiyo june 28, 2012 na kutibiwa anakujua yeye hadi kurejea nchini Agost 12,2012.. na ukimya aliokuwa nao hadi leo tunakaribia kufunga jamvi la mwaka, kinyume na matarajio ya jamii yote kwamba angeunguruma kwenye media na kuweka mambo yote hadharani na kutuachia kazi wananchi, badala yake kachikichia, lazima mtu uwe na kitu cha kujiuliza hapa, kitu gani kilichomfanya aisaliti matarajio ya jamii na je tuna haja ya kuhitaji viongozi wa sampuli hii?..

ni hoja yangu tu waweza kuijadili kwa hoja pia na mtazamo wako..
 
mzee tupatupa mnamo 13 sept alipost kitu hiki

Yu wapi sasa? Yu wapi atueleze ukweli wa madhila aliyotendewa? Yu wapi aweke wazi majina ya watesaji na sababu zilizowafanya wamtese? Yu wapi aseme kama Msangi,RAMA AU mkenya alikuwapo matesoni mwake? Yu wapi amtaje aliyempora wallet yake? Yu wapi atoe tamko juu ya hatma ya walivyokuwa wanadai kama Madaktari? Hayupo. Kimyaaaaa. Ni msaliti.

lakini Boss ukaja ukihemea juu juu this way


sasa kakusaliti wewe kwa lipi?

kama kuteswa aliteswa yeye
akiamua kusamehe wewe umesalitiwa vipi?

madaktari si wana viongozi wengine?
angekufa je.wangeacha kudai madai yao?

Muache atazame maslahi ya mkewe na watoto....wake

wewe kama una ukereketwa haswa endesha mapambano,hakuna aliekuzuia...

hapo kwenye Red Ulimaliza kila kitu mkuu

mwingine tena akaja na hii



Wasaliti washindwe kuwa madaktari wenyewe, useme mtu wa watu Dr. Ulimboka?
-Amekusaliti nini?

-Wewe umefanya jitihada gani katika sehemu ya madai?

-Amerudi kazini?

-Nakujitolea kwake, (kwani yeye yuko katika NGO), madaktari wamefanya sehemu gani?

-Maelezo yake yalipo You tube hayatoshi, maelezo na uthibitisho havikutosha?

-Tume ya polisi iliyoundwa iko wapi? ilikupa majibu? au u-mbumbumbu wako wa kutofatilia unakurupuka na kushindwa kujua uulize wapi?

-Let's say akueleze wewe "Mzee Tupatupa" Akishakuelezea, utafanya nini?

Yaani,ulitegemea na uthibisho wote ule akueleze nini? what difference will it make if the "little" nformation abt his saga you have done NOTHING with it?!
Ukiskia umaskini wetu wa mawazo ndo huu sasa.

huyu nae akabisha
Dr. Ulimboka is sufferring from amnesia. Amekwishawasahau watu waliomtesa Hata wewe ungekuwa na amnesia kama ungeng'olew kucha na jino. We mwache huyo ndugu akae kwa amani.


mwenzangu huyu mwenye akili za kijiko cha chai nae akaona achangie maada hiyo hiyo

kikuweli kabisa leo mi nachelea kusema kwamba vijana wa humu JF lazma tutafeli na haya mapambano tunayoendela nayo kwasababu siku zote tunajadili matukio tu hata cku moja cjaona watu wakijadili jinsi gani tutajikwamua namna ya kuendeleza nchi yetu kiuchumi.we fikiria mtu na akili zake timamu anakuja na tukio la kitambo watu wajadili.kwann uclete hoja labda nchi yetu ifanyenn kwenye gesi iliyovumbuliwa mtwara.


huyu asiyejua maaana ya mapinduzi nae akaona heri alete hoja yake
watanzania pumbaf sana. Wako kwenye key board wanahamasisha wenzao, wakiambiwa maandamano hawaendi. Ukitrace back,hawa wote walikuwa wanawakejeli madaktari wakati wa mgomo na leo wanaulizia matokeo au feedback. Kina Kijo Bisimba waliandaa maandamano na kuhamasisha watu washiriki lakini tuliohudhuria tulikuwa wachache mno. Leo hii mtu anataka ukombozi na kuutafuta hataki.


huyu akawa kama mie hivi
Nilikua mshabiki wake,
Lakini kwa sasa nishajitoa. Naamini atakua kadakishwa zake, katulia!!
 
Ulimboka na Zitto wote vigeugeu.
Anayefaa kuwa rais 2015 ni
Dr.Slaa au Tundu Lissu.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Mnashangaza sana watz. Mlitaka Ulimboka aseme nn zaidi muamini?Aliitaja namba ya mtesaji wake na ku-confirm kuwa ndie. Mwanahalisi wakatoa wasifu na kazi ya mtu huyo....vyombo vyote viliona,wanachi, wanaharakati na hata wanajamvi hapa JF waliona.

Sasa mlitaka Ulimboka afanye nn zaidi? Afanye nn zaidi ya yy kuitwa tu kumtambua mtesaji wake? Afanye nn zaidi? Wale madaktar wenzie aliowapigania maslahi ba mazingira bora ya kazi wamerudi nyuma, wamemtenga hatujui, wamemsaliti hatujui au wameridhika hatujui

Wananchi ambao Ulimboka aliwapigania wapate huduma bora na matibabu ya uhakika yanayotofautisha daktari na mganga mpiga ramli wako wapi? Wameridhika na huduma za hospitali zetu? hatujui..wanaogopa kuacha wajane? au kung'olewa meno? hatujui...

Mlitaka Ulimboka afanye nn?ageuke polisi mkamataji,mwendesha mashtaka na hakimu ili amfunge mtesaji wake?


Poor Tanzania, Poor people..


Ulimboka did his part, and he didu it well enough....
 
mh, Zitto style anafaa saaana , ila ulimboka style nayo si mbaya maana naye ameonyesha usikivu, baada ya kuface the music, naaamini ana siri nzitto na watesi wake hivyo kwa ule usikivu na maonyo aliyopata toka kwa watesi wake na ametii basi si vibaya tumpe umakamu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom