Kakumamoto
JF-Expert Member
- May 6, 2015
- 1,652
- 2,533
Okey, Rio hapost chochote kwenye mitandao yake ya kijamii kuhusu uwepo wake Tanzania, nakubaliana nae kuwa hapangiwi katika hilo. Huenda yeye na mkewe ni wakubwa kuliko Tanzania kama Nchi hivyo hawezi kutupa 'air time'. Je Wizara iliyohusika kumleta chini ya Waziri Makonda wao wanapost kwenye mitandao ipi ili dunia ijue Rio na Mkewe wako Tanzania? Sisi kama nchi tunautumiaje uwepo wa Rio na Mkewe kuutangaza huo utalii Makonda anaosema? Maana tumeishia kulaumu Rio hapost kwenye mitandao yake ya kijamii! Sisi tunamtumiaje? Maana inabidi sisi tumtumie kadiri tuwezavyo picha zitumwe kwa wingi dunia ijue. Kama si hivyo ni Upuusi kama upuusi mwingine. AFCON ni kubwa sana, Rio hawezi kusema chochote bila ruhusa ya CAF, haiwezekani. Matangazo na promo zote ziko chini ya CUF, sisi labdatualike timu kubwa zicheze kwenye viwanja vyetu vipya.