Yuyo Ahumile Shamalendi
JF-Expert Member
- Mar 10, 2018
- 993
- 782
Wakuu natumai mu wazima wa afya.
Kama mada inavyokuja ni huku kumlaumu baba yetu, kumbe huku chini kuna watoto hawawajibiki vizuri maagizo ya baba yao.
Ni hivi huku Wilayani Mbarali mjini Rujewa watu waliandikwa majina mwezi wa tano ili serikali ije itoe msaada wa vyandarua au net lakini cha ajabu mpaka leo wamepewa wachache, wengine wanaambiwa hawana vikaratasi vya kuwatambulisha kua walijiandikisha, sasa swali linakuja kwamba wao walivokua wanawaandika majina kwanini hawakuwapatia hivyo vikaratasi Wakawapatia wachache tu?
Hizo ndiyo sababu mojawapo za kuchukia viongozi wetu kumbe wapo wasababishi.
Viongozi najua mnapitiapitia humu, wafuatilieni hao wa chini wenu, hasa mabalozi, wenyeviti wa vitongoji ili muone hili zoezi kama lilienda kiufasaha.
Malalamiko hayo nimeyakuta kwenye mtaa au kitongoji cha Luwilindi mtoni mtaa ambao ipo ofisi ya TAKUKURU Rujewa Mbarali Mbeya.
Wakina mama wanalaumu kwanini waliandikwa majina, wanachezewa hivo wakati wao ndo wapiga kura wa kuaminiwa.
Kama mada inavyokuja ni huku kumlaumu baba yetu, kumbe huku chini kuna watoto hawawajibiki vizuri maagizo ya baba yao.
Ni hivi huku Wilayani Mbarali mjini Rujewa watu waliandikwa majina mwezi wa tano ili serikali ije itoe msaada wa vyandarua au net lakini cha ajabu mpaka leo wamepewa wachache, wengine wanaambiwa hawana vikaratasi vya kuwatambulisha kua walijiandikisha, sasa swali linakuja kwamba wao walivokua wanawaandika majina kwanini hawakuwapatia hivyo vikaratasi Wakawapatia wachache tu?
Hizo ndiyo sababu mojawapo za kuchukia viongozi wetu kumbe wapo wasababishi.
Viongozi najua mnapitiapitia humu, wafuatilieni hao wa chini wenu, hasa mabalozi, wenyeviti wa vitongoji ili muone hili zoezi kama lilienda kiufasaha.
Malalamiko hayo nimeyakuta kwenye mtaa au kitongoji cha Luwilindi mtoni mtaa ambao ipo ofisi ya TAKUKURU Rujewa Mbarali Mbeya.
Wakina mama wanalaumu kwanini waliandikwa majina, wanachezewa hivo wakati wao ndo wapiga kura wa kuaminiwa.