Tunamkumbuka Mwalimu Julius and we. Je, tunamfahamu mama yake mzazi?

Konzo Ikweta

JF-Expert Member
Oct 3, 2013
735
1,464
MFAHAMU BIBI CHRISTINA MGAYA WA NYANG'OMBE

Ameandika Francis Daudi

Hayati Bibi Christina Mgaya wa Nyang'ombe alikuwa mke wa tano(Kati ya wake 22) wa chifu Nyerere Burito. Hayati Bi. Mgaya ndiye mama mzazi wa baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Chifu Burito alikuwa kiongozi wa kabila la Zanaki wa Butiama wakati wa Ukoloni. Alitawala kuanzia 1912 mpaka mwaka Machi 30, 1942 alipofariki.

Inasemekana Bibi Mgaya wa Nyang'ombe alizaliwa mwaka 1897. Alijaaliwa kupata watoto sita ambao ni Nyerere (Julius)Kambarage, Nyangete Nyerere, Nyakahu Nyerere, Nyakigi Nyerere, Kizurira (Joseph)Nyerere na kitindamimba aliyeitwa Kiboko (Josephat) Nyerere.

Hivyo utaona mama huyu alikuwa na kazi kubwa ya malezi kwa watoto, akiwemo Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye alikuja kuwa baba wa Taifa letu.

Kwa sifa zake, Inaelezwa Bibi Christina Mgaya alikuwa mtu mwenye busara kubwa na aliyependa kuongea kwa mafumbo yenye kubeba mafunzo Fulani.

Hata Mwalimu Nyerere alipokuwa raisi bado bibi huyu aliendelea kushiriki shughuli za shamba na hata sherehe za utamaduni na watu wengine hapo Butiama kabla ya umauti kumkuta mwaka 1997.

Kulingana na Mzee Peter DM Bwimbo Katika kitabu chake kinachoitwa: ‘MLINZI MKUU WA MWALIMU NYERERE’ anaeleza kwamba Mwalimu Nyerere alimuheshimu sana mama yake, Bibi Mgaya Nyang’ombe.

Mara zote akiwepo Butiama, aliamka mapema kabla ya kufanya chochote alienda kumsalimu. Hata kulipotokea jambo ndani ya familia, aliheshimu kauli ya mama yake bila kujali madaraka yake kama raisi wa nchi.

Inaaminika alifariki akiwa na miaka 105( mwaka 1997) amezikwa karibu kabisa na kaburi la Chifu Nyerere Burito.

Ingawa maandiko mengine yanaeleza kuwa alizaliwa mwaka 1897 hivyo basi kwa mwaka 1997 angekuwa na miaka 100.
Kiufupi, Bibi Christina Mgaya wa Nyang'ombe ni sehemu muhimu sana katika uandishi wa historia ya Tanzania.

Yeye ni kati ya WANAWAKE waliosahaulika kabisa katika kurasa za historia yetu lakini ujenzi wa TAIFA hili uliitaji mtu aliyepitia malezi muhimu hasa utotoni. Ambaye alifunzwa tangu utotoni kupenda watu, kutetea watu na kuamini katika Misingi ya HAKI na USAWA.

Bila shaka elimu hii hakuipata kwa kumsoma KARX MARX au PLATO, ilianzia kwa mama ambaye hakupata kabisa elimu rasmi. Ila mwenye ucheshi, mkarimu na upendo wa hali ya juu. Huyu ndiye mama yake Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

FB_IMG_15643343022003277.jpeg
 
Alikuwa mzee sana lakini kichwani akiwa bado vizuri. Hapo pichani akimshukuru Mungu kwa mwanae kutumikia uraisi miaka zaidi ya 20 na kumaliza salama.

Picha ilipigwa Nyerere alipofika Butiama baada ya kustaafu urais.
Ahsante kwa maelezo ya ziada
 
MFAHAMU BIBI CHRISTINA MGAYA WA NYANG'OMBE

Ameandika Francis Daudi

Hayati Bibi Christina Mgaya wa Nyang'ombe alikuwa mke wa tano(Kati ya wake 22) wa chifu Nyerere Burito. Hayati Bi. Mgaya ndiye mama mzazi wa baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Chifu Burito alikuwa kiongozi wa kabila la Zanaki wa Butiama wakati wa Ukoloni. Alitawala kuanzia 1912 mpaka mwaka Machi 30, 1942 alipofariki.

Inasemekana Bibi Mgaya wa Nyang'ombe alizaliwa mwaka 1897. Alijaaliwa kupata watoto sita ambao ni Nyerere (Julius)Kambarage, Nyangete Nyerere, Nyakahu Nyerere, Nyakigi Nyerere, Kizurira (Joseph)Nyerere na kitindamimba aliyeitwa Kiboko (Josephat) Nyerere.

Hivyo utaona mama huyu alikuwa na kazi kubwa ya malezi kwa watoto, akiwemo Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye alikuja kuwa baba wa Taifa letu.

Kwa sifa zake, Inaelezwa Bibi Christina Mgaya alikuwa mtu mwenye busara kubwa na aliyependa kuongea kwa mafumbo yenye kubeba mafunzo Fulani.

Hata Mwalimu Nyerere alipokuwa raisi bado bibi huyu aliendelea kushiriki shughuli za shamba na hata sherehe za utamaduni na watu wengine hapo Butiama kabla ya umauti kumkuta mwaka 1997.

Kulingana na Mzee Peter DM Bwimbo Katika kitabu chake kinachoitwa: ‘MLINZI MKUU WA MWALIMU NYERERE’ anaeleza kwamba Mwalimu Nyerere alimuheshimu sana mama yake, Bibi Mgaya Nyang’ombe.

Mara zote akiwepo Butiama, aliamka mapema kabla ya kufanya chochote alienda kumsalimu. Hata kulipotokea jambo ndani ya familia, aliheshimu kauli ya mama yake bila kujali madaraka yake kama raisi wa nchi.

Inaaminika alifariki akiwa na miaka 105( mwaka 1997) amezikwa karibu kabisa na kaburi la Chifu Nyerere Burito.

Ingawa maandiko mengine yanaeleza kuwa alizaliwa mwaka 1897 hivyo basi kwa mwaka 1997 angekuwa na miaka 100.
Kiufupi, Bibi Christina Mgaya wa Nyang'ombe ni sehemu muhimu sana katika uandishi wa historia ya Tanzania.

Yeye ni kati ya WANAWAKE waliosahaulika kabisa katika kurasa za historia yetu lakini ujenzi wa TAIFA hili uliitaji mtu aliyepitia malezi muhimu hasa utotoni. Ambaye alifunzwa tangu utotoni kupenda watu, kutetea watu na kuamini katika Misingi ya HAKI na USAWA.

Bila shaka elimu hii hakuipata kwa kumsoma KARX MARX au PLATO, ilianzia kwa mama ambaye hakupata kabisa elimu rasmi. Ila mwenye ucheshi, mkarimu na upendo wa hali ya juu. Huyu ndiye mama yake Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

View attachment 1165727
Francis,
Ningependa kuchangia moja katika niyajuayo ya Bi. Nyang'ombe mama yake Baba wa
Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
.

Mkasa huu amenihadithia Mama Daisy mke wa Abdul Sykes ambao ulitokea katika miaka
ya mwanzo ya TANU baada ya Mwalimu Nyerere kurejea kutoka UNO mwaka wa 1955.

Ilikuwa kawaida ya TANU ikiwa wana jambo muhimu na kubwa wanataka kujadili kufanya
kikao nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukukuu.

Pamoja na kuwa watakuwa na kikao walikuwa na kawaida ya kuwa katika nyumba ile na
watu wao wa karibu.

Bi. Mruguru bint Mussa mama yake Abdul atakuwapo, Bi. Nyang'ombe mama yake
Nyerere pia atakuwapo halikadhalika Mama Maria Nyerere atakuwapo hapo.

Inawezekana hawa walijumuishwa katika mkusanyiko ule wa viongozi wa TANU kama
kichaka cha kuficha yale yaliyokuwa yakijadiliwa ili ionekane kuwa hapakuwa na kitu
pale nyumbani kwa Abdul ila ni ndugu kutembeleana.

Ingia katika link hiyo hapo chini usikilize taharuki iliyokumba moja ya kikao kama hiki
siku Mwalimu Nyerere alipougua ghafla baada ya chakula cha mchana na ikadhaniwa
amelishwa sumu na maadui wa TANU.


Mwandishi katika video hii anaanza kuzungumza katika dakika ya 40:40



1564691834960.png


Bi. Mruguru bint Mussa Mama yake
Abdulwahid Sykes


1564691888067.png


Bi. Nyang'ombe Mugaya Mama yake Baba wa Taifa

1564691952802.png


Kushoto Bi. Mwamvua bint Mashu (Mama Daisy), wa tatu
Bi. Titi Mohamed akifuatiwa na Bi. Zainab mke wa Tewa
Said Tewa
 
Back
Top Bottom