Tunamkosea sana Mungu kwa kucheza Amapiano na Sindimba madhabahuni

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,104
7,857
Mmabo mengi waumini wenzangu tunayafanya kwa ama kutofikiria au kwa kuiga iga tu bila kutazama mantiki zake.

Imeibuka hii tabia ya kucheza mitindo ya kwenye disco na sehemu za ufuska na maovu mengine tukiwa madhabahuni. Juzijuzi nimetoka kuona video vijana wanatwanga sijui ndiyo Amapiano ile, wanabambiana kabisa madhabahuni, tena wakiongozwa na mchungaji wao. Hii siyo sawa. Najua nia ni kuwavutia vijana waje kwenye ibada na majumuiko mengine ya vijana ila Mungu inabidi abaki kuwa Mungu.

Napenda jinsi Wayahudi (na labda niseme hata Waislamu) wanavyoheshimu ibada na sala zao. Hawachanganyi madesa, kwanza wana muda maalumu, pia kuna mavazi maalumu, na hata jinsi ya kusali tu inaonyesha hili ni tendo la kipekee. Sasa wenzangu na mimi kila kitu mpela mpela tu.

Turudi tujitafakari ndugu zangu.
 
Njoo kwenye Usabato , Kanisa pekee Makini ambalo linakuunganisha Kiroho na Mamlaka za Juu mbinguni.

Sisi , ni maandiko tu Yaan Biblia , Ushuhuda na Imani ya Yesu

Hawa wengine wanawalia Pesa tu !!
 
20220705_172716.jpg


MmmMH WaloKoLe WaTAkUELEWa Kweli .
 
Basi huyo Mungu wenu ni wa kifara sana.

Btw, kwanini wanadamu mnamsemea Mungu?? Mungu hajawahi Kuongea wala kuweka masharti.
 
2 Samweli 6:12-22

Mbona Daudi alicheza kwa nguvu mbele ya Mwenye enzi MUNGU mpaka mavazi yakaanguka.
Mkuu samahani kama nitakukwaza,tuwe siriasi kidogo, yaani sisi katika kuabudu tufuate utamaduni wa Kiyahudi kama mleta mada anavyo pendekeza?!! Yaani sisi?! Mfano mimi mnyakyusa niache kumtukuza Kyala gwangu baada ya mavuno kwa vimele na kapote huku nikichagizwa na ngoma za magosi, samba,ndingala ni ing'oma nikahangaike na Mungu wa Yakobo, sijui na nani huko?
Tubadilike Watanzania, tusiendeshwe na mapokeo ya dini.
 
😂😂😂😂😂😂😂uncle watuache tumtumikie Mwenyezi Mungu kwa style zetu,nyakati zinabadilika
Mkuu samahani kama nitakukwaza,tuwe siriasi kidogo, yaani sisi katika kuabudu tufuate utamaduni wa Kiyahudi kama mleta mada anavyo pendekeza?!! Yaani sisi?! Mfano mimi mnyakyusa niache kumtukuza Kyala gwangu baada ya mavuno kwa vimele na kapote huku nikichagizwa na ngoma za magosi, samba,ndingala ni ing'oma nikahangaike na Mungu wa Yakobo, sijui na nani huko?
Tubadilike Watanzania, tusiendeshwe na mapokeo ya dini.
 
2 Samweli 6:12-22

Mbona Daudi alicheza kwa nguvu mbele ya Mwenye enzi MUNGU mpaka mavazi yakaanguka.
Hivi mlishashindwa kusoma biblia kabisa mmeish kupotoshwa na vifungu vya Kukaririshwaaa: Tatzo Sadaka ina nguvu kuliko Maandiko uko makanisani kwenu.
 
Hivi mlishashindwa kusoma biblia kabisa mmeish kupotoshwa na vifungu vya Kukaririshwaaa: Tatzo Sadaka ina nguvu kuliko Maandiko uko makanisani kwenu.
Wewe uliyesoma tupe kifungu ambacho tunakatazwa kumchezea Mungu...

Sadaka inanguvu ukimtolea Mungu kwa imani...

Pia maandiko ni taa na mwanga wa njia zetu...
 
Wewe uliyesoma tupe kifungu ambacho tunakatazwa kumchezea Mungu...

Sadaka inanguvu ukimtolea Mungu kwa imani...

Pia maandiko ni taa na mwanga wa njia zetu...
Haya ndo matatzo ya kurithi mpaka dini, Sifanyag kaz ya Kuelimisha asie na uelewa endelea kucheza mpaka Jeje na Tetema kanisani.
 
Mmabo mengi waumini wenzangu tunayafanya kwa ama kutofikiria au kwa kuiga iga tu bila kutazama mantiki zake.

Imeibuka hii tabia ya kucheza mitindo ya kwenye disco na sehemu za ufuska na maovu mengine tukiwa madhabahuni. Juzijuzi nimetoka kuona video vijana wanatwanga sijui ndiyo Amapiano ile, wanabambiana kabisa madhabahuni, tena wakiongozwa na mchungaji wao. Hii siyo sawa. Najua nia ni kuwavutia vijana waje kwenye ibada na majumuiko mengine ya vijana ila Mungu inabidi abaki kuwa Mungu.

Napenda jinsi Wayahudi (na labda niseme hata Waislamu) wanavyoheshimu ibada na sala zao. Hawachanganyi madesa, kwanza wana muda maalumu, pia kuna mavazi maalumu, na hata jinsi ya kusali tu inaonyesha hili ni tendo la kipekee. Sasa wenzangu na mimi kila kitu mpela mpela tu.

Turudi tujitafakari ndugu zangu.
Mtoa Mada pole ndugu yangu ulichochelewa kujua ni kwamba watu wanadhani Allah anaenda na digitali, Watu wanapenda Mkate.
 
Haya ndo matatzo ya kurithi mpaka dini, Sifanyag kaz ya Kuelimisha asie na uelewa endelea kucheza mpaka Jeje na Tetema kanisani.
Sijarithi dini, maana najua dini ni njia...

Imeshanifanya namjua YESU KRISTO/MUNGU

anakaa ndani yangu na ni kiongozi wa maisha yangu sina shaka nae.
 
Back
Top Bottom