Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 46,889
- 32,289
Wanabodi.
Kwa Watanzania wanaotakia mema nchi yetu wanampongeza Askofu wa Kanisa la (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Dr Martin Shao, kwa uzalendo wake alipowasihi madaktari waliogoma katika hospitali mbali mbali nchini ikiwemo hospitali ya KCMC kureja kazini huku wakiendelea na madai yao serikalini.
Wananchi wengi wamefedheheswa na kauli za Padri Babtiste Mapunda na Dr Slaa, kuunga mkono mgomo wa madaktari...Padri na Dr Slaa, waelezeni Watanzania kwa maoni yenu mgomo unamkomoa nani? Na kumuumiza nani? Je ni kweli migomo ya aina hii inawafikia walengwa na kuwaonjesha maumivu yatokanayo na mgomo?
Dr Slaa, tembelea muhimbili na kakae pale mapokezi walau kwa saa mbili tu ili uone mwenyewe wagonjwa wanavyoteseka na wengine wanavyokufa kwa kukosa huduma halafu uwaambie Watanzania mgomo uendelee hadi lini ama ujirudie mara ngapi ili kuwashikisha adabu hao unaodhani ndio wakosaji na wasiotaka kutoa stahiki ya madaktari..
Tunashindwa kuamini Dr Slaa na Padri Mapunda, wameshindwa kuwahurumia Watanzania wanaoteseka na huku wengine wakifa baada ya kukosa huduma ya kitabibu, miongoni wanaougua ni wanachama wa Chadema sasa watu hao wakifa si anapoteza wananchama.
Kwa Watanzania wanaotakia mema nchi yetu wanampongeza Askofu wa Kanisa la (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Dr Martin Shao, kwa uzalendo wake alipowasihi madaktari waliogoma katika hospitali mbali mbali nchini ikiwemo hospitali ya KCMC kureja kazini huku wakiendelea na madai yao serikalini.
Wananchi wengi wamefedheheswa na kauli za Padri Babtiste Mapunda na Dr Slaa, kuunga mkono mgomo wa madaktari...Padri na Dr Slaa, waelezeni Watanzania kwa maoni yenu mgomo unamkomoa nani? Na kumuumiza nani? Je ni kweli migomo ya aina hii inawafikia walengwa na kuwaonjesha maumivu yatokanayo na mgomo?
Dr Slaa, tembelea muhimbili na kakae pale mapokezi walau kwa saa mbili tu ili uone mwenyewe wagonjwa wanavyoteseka na wengine wanavyokufa kwa kukosa huduma halafu uwaambie Watanzania mgomo uendelee hadi lini ama ujirudie mara ngapi ili kuwashikisha adabu hao unaodhani ndio wakosaji na wasiotaka kutoa stahiki ya madaktari..
Tunashindwa kuamini Dr Slaa na Padri Mapunda, wameshindwa kuwahurumia Watanzania wanaoteseka na huku wengine wakifa baada ya kukosa huduma ya kitabibu, miongoni wanaougua ni wanachama wa Chadema sasa watu hao wakifa si anapoteza wananchama.