M-mbabe
JF-Expert Member
- Oct 29, 2009
- 13,203
- 23,020
Watanzania wenzangu hili swali si kwa ajili ya wanasiasa au wanaharakati pekee - ni swali linalopaswa kuelekezwa kwetu sote Watanzania tunaotamani demokrasia, haki na utawala bora virejee na kutamalaki katika jamii yetu.
Tusitegemee hata siku moja eti walio madarakani watakubali kirahisi uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi, it's only natural.
Which means inahitaji watu wengine walio nje ya madaraka ndiyo waweke msukumo mkubwa katika hili. Hata kama wadau wa maendeleo wa nchi yetu wanaunga mkono uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi, si wao wanaoweza kulianzisha - wao wanaweza tu kuwa chachu katika msukumo ambao wahusika (yaani sisi) watauanzisha wenyewe.
Natambua kipaumbele kwa sasa ni mapambano dhidi ya janga la korona, lakini hii haituzuii in the meantime kuwa na mikakati thabiti itakayopelekea uundwaji wa NEC huru.
Je, kuna mikakati yoyote? Imefikia wapi? Ni nini matarajio? Kama hakuna mikakati yoyote, uzi huu ni kwa ajili ya kutukumbukusha (wake up call) kuwa tunalo hili jukumu mbele yetu.
Wabilah Tawfiq
Bwana Yesu Asifiwe
Tumsifu Yesu Kristo
cc: Zitto, John Mnyika
Tusitegemee hata siku moja eti walio madarakani watakubali kirahisi uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi, it's only natural.
Which means inahitaji watu wengine walio nje ya madaraka ndiyo waweke msukumo mkubwa katika hili. Hata kama wadau wa maendeleo wa nchi yetu wanaunga mkono uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi, si wao wanaoweza kulianzisha - wao wanaweza tu kuwa chachu katika msukumo ambao wahusika (yaani sisi) watauanzisha wenyewe.
Natambua kipaumbele kwa sasa ni mapambano dhidi ya janga la korona, lakini hii haituzuii in the meantime kuwa na mikakati thabiti itakayopelekea uundwaji wa NEC huru.
Je, kuna mikakati yoyote? Imefikia wapi? Ni nini matarajio? Kama hakuna mikakati yoyote, uzi huu ni kwa ajili ya kutukumbukusha (wake up call) kuwa tunalo hili jukumu mbele yetu.
Wabilah Tawfiq
Bwana Yesu Asifiwe
Tumsifu Yesu Kristo
cc: Zitto, John Mnyika