Tunajivunia/tunavumilia kuwa watz

Chief Ken Lo

Member
Sep 14, 2011
56
4
wakuu hii kitu inanipasua kichwa kwa mrefu sana....
1) naomba mnisaidie katika hili wanajamvi, hivi tunajivunia kweli kuwa wananchi wa hii nchi???kwa lipi???????????
2)kama tunavumilia kuwa watz, ni sababu gani za msingi zinazotupa huo uvumilivu????
nawasilisha
 
Usiulize Tanzania itakufanyia nini au ikmekufanyia nini. Jiulize utaifanyia nini nchi yako. Hivi is it fair kukaa na kulalamika kila siku kuhusu hii nchi? Ninachoamini,hata CCM wakiondoka madarakani kikaja chama kingine kikatawala. Hakuna mabadiliko makubwa yatakayoweza kutokea iwapo sisi Watanzania hatutakubali kubadilika na kuwa na upendo na taifa hili. Tatizo lililopo ni kuwa tunadhani iwapo chama kingine kitatawala matatizo tuliyonayo yatamalizika. Ufisadi utamalizika iwapo mimi na wewe tutabadilika na kuuchukia. Na matatizo ya kiuchumi kamwe hayawezi kumalizika leo au kesho bali inahitaji sera nzuri na muda pia unahitajika.
Kwa hiyo Watanzania tunapaswa kuacha ushabiki wa vyama ambao hauwezi kutusaidia lolote.
 
Binafsi jibu langu ni ndiyooooooooo, najivunia kuwa mtanzania. Natena nina kila sababu ya kujivunia. Ni kweli nchi yetu inapitia kipindi kiguma sana hasa katika nyanja nzima ya uongozi. Jambo hili lisitukatishe tamaa hadi tukaanza kuhisi kama hatuna tene sababu ya kujivunia utanzania wetu.

Tanzania ni nchi ya amani na pia ni nchi iliojaaliwa rasilimali nyingi sana. Lakini tatizo tulilonalo ni uongozi wetu. Hapa kwa kweli kuna shida sana na inatubidi tuchukue hatua la sivyo taifa letu litaangamia huku twalitazama.

Wito kwa watanzania wenzangu, chonde chonde tusikate tamaa kiasi hicho kwani hata wazee wetu walipigania uhuru kwa moyo mmoja na wakashinda. Aluta continuaaaaaaaaaaa!
 
Usiulize Tanzania itakufanyia nini au ikmekufanyia nini. Jiulize utaifanyia nini nchi yako. Hivi is it fair kukaa na kulalamika kila siku kuhusu hii nchi? Ninachoamini,hata CCM wakiondoka madarakani kikaja chama kingine kikatawala. Hakuna mabadiliko makubwa yatakayoweza kutokea iwapo sisi Watanzania hatutakubali kubadilika na kuwa na upendo na taifa hili. Tatizo lililopo ni kuwa tunadhani iwapo chama kingine kitatawala matatizo tuliyonayo yatamalizika. Ufisadi utamalizika iwapo mimi na wewe tutabadilika na kuuchukia. Na matatizo ya kiuchumi kamwe hayawezi kumalizika leo au kesho bali inahitaji sera nzuri na muda pia unahitajika.
Kwa hiyo Watanzania tunapaswa kuacha ushabiki wa vyama ambao hauwezi kutusaidia lolote.
\

Mawazo yako ni mazuri ila hoja zako zinapingana na mtazamo wako, ndugu yangu sera za maendeleo ktk nchi zinaandaliwa na kusimamiwa na chama kinacho shika hatamu, so, ili upate sera nzuri ni kwa maendeleo ya nchi ni lazima upate chama chenye sera mbadala na zinazokidhi mahitaji ya nchi hiyo. Hivyo huwezi kukwepa kuwa shabiki wa cha(vya)ma otherwise hujitambui nafasi na umuhiu wako katika kuleta maendeleo ya nchi yako ....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom