Tunajifunza nini kwa yanayotokea nchini Marekani kwa Rais aliyeko madarakani kufunguliwa mashitaka?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,479
30,144
Wote ni mashahidi kwa yanayotokea nchini Marekani hivi sasa kwa Bunge la nchi hiyo kuanza mchakato wa kumfungulia mashtaka Rais wa nchi hiyo kwa matumizi mabaya ya madaraka.

Kwa kifupi katika kuelezea kuhusu sakata hilo ni kuwa inadaiwa kuwa Rais Trump alitumia vibaya madaraka yake kwa kumpigia simu kiongozi wa nchi ya Ukraine mwezi July mwaka huu, ili amchunguze kiongozi mwenzake Joe Baden, katika biashara zake anazofanya nchini huko, ili ibainike kama rushwa imetumika.

Madhumiuni yake makubwa yakiwa ni kumkomoa na kumdhalilisha mgombea huyo wa chama cha Democrats, ambaye ameonyesha kuwa atakuwa tishio kwake katika uchaguzi ujao wa Urais nchini Marekani.

Ndipo hapo ninapojiuliza kama nchi tunapata somo gani katika sakata hilo la kumchunguza Rais aliyeko madarakani, tena uchunguzi huo ukirushwa Live na vituo kadhaa vya lunimga nchini humo kikiwemo kituo maarufu kabisa duniani cha CNN?

Najaribu kujiuliza hivi Rais wetu, ameshavunja Katiba ya nchi yetu Mara ngapi?

Hivi alipopiga marufuku vyama vya siasa vya upinzani visifanye mikutano yoyote ya kisiasa hapa nchini hadi mwaka 2020, wakati yeye na chama chake cha CCM kila kukicha tunawaona nchi nzima wakizunguka na kufanya kampeni, je hajavunja Katiba ya nchi??

Tujiulize hivi hili sakata la uchaguzi wa serikali za mitaa jinsi ulivyovurugwa na hao wasimamizi wa uchaguzi, kwa kuwapendelea waziwazi wagombea wa chama tawala cha CCM na kuwaonea wagombea wa vyama vya upinzani, hivi kwa kufanya hivyo Rais wetu, hajavunja Katiba kweli?

Kama Rais kabla hajaingia madarakani anaapa kulinda na kuitii Katiba ya nchi ni kwanini basi yeye aachiwe aisigine Katiba ya nchi yetu atakavyo?

Je, Bunge letu halijayaona hayo?

Ni kwanini basi Bunge letu halianzishi mchakato wa "impeachment" kwa Rais wa nchi hii?

Naomba tuchangie kwa staha, mada hiyo muhimu sana kwa mustakabali wa Taifa letu, bila ya kujali itikadi zetu za kisiasa.
 
Hatuna cha kujifunza, maana kama Taifa hatujui tunataka kuelekea wapi, Kila tunachofanya ni siasa na tuna focus uchaguzi tu.
 
kuna tofauti kubwa kati ya kifo na usingizi.
tulizana kisha ndio uje na huo mfananisho
 
Kwa katiba tuliyo nayo hakuna wa kumgusa rais sio bunge wala mahakama
 
Kuyaleta mambo ya Marekani huku bongo ni kujivuruga tu.
 
Kuyaleta mambo ya Marekani huku bongo ni kujivuruga tu.
Hatujivurugi Mkuu Data

Kwa kuwa tunaambiwa kuwa hao Marekani ndiyo mama wa Demokrasia duniani, kwa hivyo yatupasa tufuate nyayo zao
 
Mzungu na mtu mweusi ni watu wawili tofauti saana tu na ndio maana hata ujirani hatuna nao. Mungu ana akili nyingi sana.

Hapa ukiona watu kama Jaji Mkuu, Spika, Mawaziri nk nk wanavyomsujudia rais, unashangaa hawa watu wanaendaga kwenye nyumba za ibada kufanya nini na huku mungu wao hayuko huko??? Very perplexing really.
 
Wote ni mashahidi kwa yanayotokea nchini Marekani hivi sasa kwa Bunge la nchi hiyo kuanza mchakato wa kumfungulia mashtaka Rais wa nchi hiyo kwa matumizi mabaya ya madaraka.

Kwa kifupi katika kuelezea kuhusu sakata hilo ni kuwa inadaiwa kuwa Rais Trump alitumia vibaya madaraka yake kwa kumpigia simu kiongozi wa nchi ya Ukraine mwezi July mwaka huu, ili amchunguze kiongozi mwenzake Joe Baden, katika biashara zake anazofanya nchini huko, ili ibainike kama rushwa imetumika.

Madhumiuni yake makubwa yakiwa ni kumkomoa na kumdhalilisha mgombea huyo wa chama cha Democrats, ambaye ameonyesha kuwa atakuwa tishio kwake katika uchaguzi ujao wa Urais nchini Marekani.

Ndipo hapo ninapojiuliza kama nchi tunapata somo gani katika sakata hilo la kumchunguza Rais aliyeko madarakani, tena uchunguzi huo ukirushwa Live na vituo kadhaa vya lunimga nchini humo kikiwemo kituo maarufu kabisa duniani cha CNN?

Najaribu kujiuliza hivi Rais wetu, ameshavunja Katiba ya nchi yetu Mara ngapi?

Hivi alipopiga marufuku vyama vya siasa vya upinzani visifanye mikutano yoyote ya kisiasa hapa nchini hadi mwaka 2020, wakati yeye na chama chake cha CCM kila kukicha tunawaona nchi nzima wakizunguka na kufanya kampeni, je hajavunja Katiba ya nchi??

Tujiulize hivi hili sakata la uchaguzi wa serikali za mitaa jinsi ulivyovurugwa na hao wasimamizi wa uchaguzi, kwa kuwapendelea waziwazi wagombea wa chama tawala cha CCM na kuwaonea wagombea wa vyama vya upinzani, hivi kwa kufanya hivyo Rais wetu, hajavunja Katiba kweli?

Kama Rais kabla hajaingia madarakani anaapa kulinda na kuitii Katiba ya nchi ni kwanini basi yeye aachiwe aisigine Katiba ya nchi yetu atakavyo?

Je, Bunge letu halijayaona hayo?

Ni kwanini basi Bunge letu halianzishi mchakato wa "impeachment" kwa Rais wa nchi hii?

Naomba tuchangie kwa staha, mada hiyo muhimu sana kwa mustakabali wa Taifa letu, bila ya kujali itikadi zetu za kisiasa.
Mind your business upuuzi wa US waachie Wao.
 
Eheee mwenyezi Mungu naomba nijaarie uhai niweze shuhudi chama chochote cha upinzani kishike Dola ni kitendo kama serikali ya sasa ya CCM inavyoendeshwa, nchi ili nione na wao watalia na kulalamika kama wenzao
 
Hatujivurugi Mkuu Data

Kwa kuwa tunaambiwa kuwa hao Marekani ndiyo mama wa Demokrasia duniani, kwa hivyo yatupasa tufuate nyayo zao
Donald hawatamfanya chochote, afu ask yourself, marekani ina miaka mingapi na hiyo demokrasia ukicompare na Tz
 
Donald hawatamfanya chochote, afu ask yourself, marekani ina miaka mingapi na hiyo demokrasia ukicompare na Tz
Ngoja tuone........

Kwa kuwa huo ni mchakato wa kumfungulia mashitaka, iwapo itathibitika kuwa kuna ushahidi wa kutosha kufanya hivyo
 
Wote ni mashahidi kwa yanayotokea nchini Marekani hivi sasa kwa Bunge la nchi hiyo kuanza mchakato wa kumfungulia mashtaka Rais wa nchi hiyo kwa matumizi mabaya ya madaraka.

Kwa kifupi katika kuelezea kuhusu sakata hilo ni kuwa inadaiwa kuwa Rais Trump alitumia vibaya madaraka yake kwa kumpigia simu kiongozi wa nchi ya Ukraine mwezi July mwaka huu, ili amchunguze kiongozi mwenzake Joe Baden, katika biashara zake anazofanya nchini huko, ili ibainike kama rushwa imetumika.

Madhumiuni yake makubwa yakiwa ni kumkomoa na kumdhalilisha mgombea huyo wa chama cha Democrats, ambaye ameonyesha kuwa atakuwa tishio kwake katika uchaguzi ujao wa Urais nchini Marekani.

Ndipo hapo ninapojiuliza kama nchi tunapata somo gani katika sakata hilo la kumchunguza Rais aliyeko madarakani, tena uchunguzi huo ukirushwa Live na vituo kadhaa vya lunimga nchini humo kikiwemo kituo maarufu kabisa duniani cha CNN?

Najaribu kujiuliza hivi Rais wetu, ameshavunja Katiba ya nchi yetu Mara ngapi?

Hivi alipopiga marufuku vyama vya siasa vya upinzani visifanye mikutano yoyote ya kisiasa hapa nchini hadi mwaka 2020, wakati yeye na chama chake cha CCM kila kukicha tunawaona nchi nzima wakizunguka na kufanya kampeni, je hajavunja Katiba ya nchi??

Tujiulize hivi hili sakata la uchaguzi wa serikali za mitaa jinsi ulivyovurugwa na hao wasimamizi wa uchaguzi, kwa kuwapendelea waziwazi wagombea wa chama tawala cha CCM na kuwaonea wagombea wa vyama vya upinzani, hivi kwa kufanya hivyo Rais wetu, hajavunja Katiba kweli?

Kama Rais kabla hajaingia madarakani anaapa kulinda na kuitii Katiba ya nchi ni kwanini basi yeye aachiwe aisigine Katiba ya nchi yetu atakavyo?

Je, Bunge letu halijayaona hayo?

Ni kwanini basi Bunge letu halianzishi mchakato wa "impeachment" kwa Rais wa nchi hii?

Naomba tuchangie kwa staha, mada hiyo muhimu sana kwa mustakabali wa Taifa letu, bila ya kujali itikadi zetu za kisiasa.
Kwenye sual la mikutano ya vyama vyao siasa, Rais hajavunja Katiba na ushahidi upo. Kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Rais hajavunja Katiba na ushahidi upo.
 
... among others, MHUNI akipenyeza kuwa kiongozi wenu basi mjitayarishe kulima kwa meno yenu
Hiyo ni kweli kabisa ndio maana Watanzania tuko makini sana. Hatuwezi kuwaingiza madarakani wahuni ambao hata uchaguzi wa mwenyekiti tu hawataki kufanya. Wakipata urais si tutakuwa kama Swaziland; Samahani eSwatini!!!
 
Back
Top Bottom