Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
Hivi ni kweli malengo ya CCM ya 1977 na ya leo bado yale yale?
Makamu wa M/kiti wa CCM(Zanzibar) ambaye pia ni rais wa Zanzibar Ndugu Amani Karume jana akiwa Bagamoyo amefungua rasmi maadhimisho ya miaka 33 ya kuzaliwa kwa CCM amesema CCM ni imara na moja CCM ni kama mwalimu wa vyama vyote vya siasa.
Aidha amesema azma ya CCM ni kuendeleza mazuri yote ya TANU na ASP na kuyaacha mabaya pamoja naKuendelea kuimarisha uhuru wa Tanzania ikiwa ni pamoja na kudumisha Mapinduzi ya ZanzibarKuendelea kuimarisha umoja na mshikamano wa kitaifaKuendelea kupanua na kuimarisha demokrasia ndani ya Chama chini ikiwa ni pamoja na kufungua milango ya demokrasia Zanzibar.
Aidha CCM inaendelea kuimarisha umoja na mshikamano wa kitaifa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mfumo wa vyama vingi hauwi sababu ya chuki na msambaratiko wa umoja wa kitaifa, amani na mshikamano. Katika msimamo huo CCM imeweza kufikia MUAFAKA na CUF, hatua ambayo imetoa fursa kwa Zanzibar kurejesha hali ya amani, utulivu na mashirikiano, hivyo kuweza kupiga hatua kubwa ya maendeleo.
Lakini hakusita vile vile kuweka kijembe kuwa si lazima kila mtu awe kiongozi unaweza kutaka kuwa kiongozi na usichaguliwe nafikri alikwa akiwaeleza wale wanaonyemelea kiti cha urais Zanzibar baada ya yeye kumaliza kipindi chake cha pili hasa Ghalib Bilal aliyeuwania mara mbili na kuukosa
Akizunguza katika mkutano huo Katibu mkuu wa CCM Yusufu Makamba amerudia usemi wake kuwa wanaompinga rais Kikwete ni wehu kwa vile Kikwete ni zaidi ya chama na yuko tayari kupelekwa Mahakamani kwa kauli yake hiyo.
Naye makamu mwenyekiti wa CCM (Bara), Pius Msekwa akihutubia wanafunzi wa vyuo vikuu vya mjini Dodoma alimesema kuwa yeye ndiye aliyemuandaa Rais Jakaya Kikwete tangu akiwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akiwa kijana mdogo na kuwa alikuwa mwanachama mwaminifu tangu wakati akiwa kijana mdogo , Msekwa alisema CCM kinawaandalia wasomi hao mazingira ya kuundiwa mkoa wao wa kichama.
Chama cha Mapinduzi (CCM) kilizaliwa tarehe 5 Februari, 1977 kutokana na kuvunjwa kwa vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) na Afro-Shirazi Party (ASP).
Katika Mkutano Mkuu wa Pamoja wa TANU na ASP uliofanyika tarehe 22 Septemba, 1975 Rais wa TANU, Mwalimu Nyerere alisisitiza kwamba Tanzania ni nchi yenye Chama kimoja;
Mwalimu alipendekeza kuunganishwa kwa TANU na ASP na kuundwa kwa chama kipya. Pendekezo hilo liliwasilishwa kwa wanachama wa TANU na ASP zaidi ya asilimia 90 ya wanachama walikubaliana na pendekezo la Mwalimu Nyerere. Tume ya watu 20 ilipewa jukumu la kutayarisha Katiba ya Chama kipya. Mwenyekiti wa Tume hiyo alikuwa Sheikh Thabit Kombo na Katibu wake alikuwa Ndugu Pius Msekwa.
Wajumbe wa Tume ya Watu 20 ya kuandaa Katiba ya CCM:-
Kutoka TANU:
1. Ndugu Peter A. Kisumo 2. Ndugu Pius Msekwa 3. Ndugu Daudi N. Mwakawago 4. Ndugu Kingunge Ngombale-Mwiru 5. Ndugu Jackson Kaaya 6. Ndugu Peter S.Siyovelwa
7. Ndugu Nicodemus M. Banduka 8. Ndugu Lawi N. Sijaona 9. Ndugu Beatrice P. hango
10. Ndugu Basheikh A. Mikidadi
Kutoka ASP:
1. Sheikh Thabiti Kombo 2. Ndugu Ali Mzee 3. Ndugu A.S. Natepe 4. Ndugu Seif Bakari 5. Ndugu Hamisi Hemed 6. Ndugu Rajab Kheri 7. Ndugu Asia Amour 8. Ndugu Hassan N. Moyo 9. Ndugu Juma Salum 10. Ndugu Hamdan Muhiddin
Tunajifunza nini kutokana na historia ya TANU na ASP na baadaye CCM
inayotimiza umri wa mtu mzima sasa?
Source: Magazeti ya Mwananchi Habari Leo Majira Tovuti mbalimbali na mimi
mwenyewe
Makamu wa M/kiti wa CCM(Zanzibar) ambaye pia ni rais wa Zanzibar Ndugu Amani Karume jana akiwa Bagamoyo amefungua rasmi maadhimisho ya miaka 33 ya kuzaliwa kwa CCM amesema CCM ni imara na moja CCM ni kama mwalimu wa vyama vyote vya siasa.
Aidha amesema azma ya CCM ni kuendeleza mazuri yote ya TANU na ASP na kuyaacha mabaya pamoja naKuendelea kuimarisha uhuru wa Tanzania ikiwa ni pamoja na kudumisha Mapinduzi ya ZanzibarKuendelea kuimarisha umoja na mshikamano wa kitaifaKuendelea kupanua na kuimarisha demokrasia ndani ya Chama chini ikiwa ni pamoja na kufungua milango ya demokrasia Zanzibar.
Aidha CCM inaendelea kuimarisha umoja na mshikamano wa kitaifa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mfumo wa vyama vingi hauwi sababu ya chuki na msambaratiko wa umoja wa kitaifa, amani na mshikamano. Katika msimamo huo CCM imeweza kufikia MUAFAKA na CUF, hatua ambayo imetoa fursa kwa Zanzibar kurejesha hali ya amani, utulivu na mashirikiano, hivyo kuweza kupiga hatua kubwa ya maendeleo.
Lakini hakusita vile vile kuweka kijembe kuwa si lazima kila mtu awe kiongozi unaweza kutaka kuwa kiongozi na usichaguliwe nafikri alikwa akiwaeleza wale wanaonyemelea kiti cha urais Zanzibar baada ya yeye kumaliza kipindi chake cha pili hasa Ghalib Bilal aliyeuwania mara mbili na kuukosa
Akizunguza katika mkutano huo Katibu mkuu wa CCM Yusufu Makamba amerudia usemi wake kuwa wanaompinga rais Kikwete ni wehu kwa vile Kikwete ni zaidi ya chama na yuko tayari kupelekwa Mahakamani kwa kauli yake hiyo.
Naye makamu mwenyekiti wa CCM (Bara), Pius Msekwa akihutubia wanafunzi wa vyuo vikuu vya mjini Dodoma alimesema kuwa yeye ndiye aliyemuandaa Rais Jakaya Kikwete tangu akiwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akiwa kijana mdogo na kuwa alikuwa mwanachama mwaminifu tangu wakati akiwa kijana mdogo , Msekwa alisema CCM kinawaandalia wasomi hao mazingira ya kuundiwa mkoa wao wa kichama.
Chama cha Mapinduzi (CCM) kilizaliwa tarehe 5 Februari, 1977 kutokana na kuvunjwa kwa vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) na Afro-Shirazi Party (ASP).
Katika Mkutano Mkuu wa Pamoja wa TANU na ASP uliofanyika tarehe 22 Septemba, 1975 Rais wa TANU, Mwalimu Nyerere alisisitiza kwamba Tanzania ni nchi yenye Chama kimoja;
Mwalimu alipendekeza kuunganishwa kwa TANU na ASP na kuundwa kwa chama kipya. Pendekezo hilo liliwasilishwa kwa wanachama wa TANU na ASP zaidi ya asilimia 90 ya wanachama walikubaliana na pendekezo la Mwalimu Nyerere. Tume ya watu 20 ilipewa jukumu la kutayarisha Katiba ya Chama kipya. Mwenyekiti wa Tume hiyo alikuwa Sheikh Thabit Kombo na Katibu wake alikuwa Ndugu Pius Msekwa.
Wajumbe wa Tume ya Watu 20 ya kuandaa Katiba ya CCM:-
Kutoka TANU:
1. Ndugu Peter A. Kisumo 2. Ndugu Pius Msekwa 3. Ndugu Daudi N. Mwakawago 4. Ndugu Kingunge Ngombale-Mwiru 5. Ndugu Jackson Kaaya 6. Ndugu Peter S.Siyovelwa
7. Ndugu Nicodemus M. Banduka 8. Ndugu Lawi N. Sijaona 9. Ndugu Beatrice P. hango
10. Ndugu Basheikh A. Mikidadi
Kutoka ASP:
1. Sheikh Thabiti Kombo 2. Ndugu Ali Mzee 3. Ndugu A.S. Natepe 4. Ndugu Seif Bakari 5. Ndugu Hamisi Hemed 6. Ndugu Rajab Kheri 7. Ndugu Asia Amour 8. Ndugu Hassan N. Moyo 9. Ndugu Juma Salum 10. Ndugu Hamdan Muhiddin
Tunajifunza nini kutokana na historia ya TANU na ASP na baadaye CCM
inayotimiza umri wa mtu mzima sasa?
Source: Magazeti ya Mwananchi Habari Leo Majira Tovuti mbalimbali na mimi
mwenyewe