Tunajifunza nini juu ya hii habari ya Obama na rafiki yake wa Uganda?

CPA

JF-Expert Member
Mar 1, 2011
809
354
Obama na rafiki yake wa Uganda

18 Septemba 2012 15:03

Kama kuna rais ambaye watu wengi Uganda wangetaka kukutana naye ni rais wa Marekani Barack Obama.
Kijana Christopher Kule, mwenye umri wa miaka kumi na ambaye ni mwanafunzi wa shule ya msingi wilayani Kasese, nchini Uganda, hajaachwa nyuma katika ndoto hiyo.
Bila shaka wengi watasema yuko hatua nyingi mbele ya wale walio na ndoto ya kumuona Obama. Hii ni baada ya Kule kupokea majibu ya barua aliyomwandikia Rais Barack Obama kutoka kwa Obama mwenyewe.
Kijana huyo anaamini kuwa baada ya kuandikiana barua na Rais Obama, kuna matumaini kwamba siku moja atakutana naye.
Yote haya yanatokana na zoezi la kuandika barua ambalo Kule na wanafunzi wenzake walikuwa wanafanya darasani, baada ya kuagizwa na mwalimu wamwandikie barua mtu yeyote wakiomba msaada kwa jamii yao.
Barua ya Kule bila shaka ilimtia hamasa mwalimu wake wa kigeni kutoka Marekani ambaye alikuwa anafunza shuleni humo kwa muda.
Mwalimu huyo alisema kuwa nyanyake ni rafiki wa mmoja wa wasaidizi katika ikulu ya rais na kuahidi kuhakikisha kuwa ujumbe huo utamfikia rais Obama na bila shaka ahadi ikatimizwa , kwani barua ilimfikia rais Obama.
Kule alisema kuwa katika barua yake, alimwomba Obama kusaidia Uganda kuangamiza uasi na kuhamasisha amani.
Katika majibu yake kwa Kule, rais Obama alisema kuwa Marekani imejitolea kuangazia maswala kadhaa muhimu kote duniani kama haki za binadamu kwa sababu Marekani inapinga vikali ghasia na ukandamizaji dhidi ya watu wote. Pia alimtumia kijana huyo picha yake aliyokuwa ametia saini.
Rais Obama alipata muda wa kumjibu kijana Kule. Je marais wa Afrika wana muda wa kuzungumza na wananchi wao na kutoa mfano wa Obama kwa Afrika? Nini maoni yako?

Chanzo: bbcswahili.
 
Obama na rafiki yake wa Uganda

18 Septemba 2012 15:03

Kama kuna rais ambaye watu wengi Uganda wangetaka kukutana naye ni rais wa Marekani Barack Obama.
Kijana Christopher Kule, mwenye umri wa miaka kumi na ambaye ni mwanafunzi wa shule ya msingi wilayani Kasese, nchini Uganda, hajaachwa nyuma katika ndoto hiyo.
Bila shaka wengi watasema yuko hatua nyingi mbele ya wale walio na ndoto ya kumuona Obama. Hii ni baada ya Kule kupokea majibu ya barua aliyomwandikia Rais Barack Obama kutoka kwa Obama mwenyewe.
Kijana huyo anaamini kuwa baada ya kuandikiana barua na Rais Obama, kuna matumaini kwamba siku moja atakutana naye.
Yote haya yanatokana na zoezi la kuandika barua ambalo Kule na wanafunzi wenzake walikuwa wanafanya darasani, baada ya kuagizwa na mwalimu wamwandikie barua mtu yeyote wakiomba msaada kwa jamii yao.
Barua ya Kule bila shaka ilimtia hamasa mwalimu wake wa kigeni kutoka Marekani ambaye alikuwa anafunza shuleni humo kwa muda.
Mwalimu huyo alisema kuwa nyanyake ni rafiki wa mmoja wa wasaidizi katika ikulu ya rais na kuahidi kuhakikisha kuwa ujumbe huo utamfikia rais Obama na bila shaka ahadi ikatimizwa , kwani barua ilimfikia rais Obama.
Kule alisema kuwa katika barua yake, alimwomba Obama kusaidia Uganda kuangamiza uasi na kuhamasisha amani.
Katika majibu yake kwa Kule, rais Obama alisema kuwa Marekani imejitolea kuangazia maswala kadhaa muhimu kote duniani kama haki za binadamu kwa sababu Marekani inapinga vikali ghasia na ukandamizaji dhidi ya watu wote. Pia alimtumia kijana huyo picha yake aliyokuwa ametia saini.
Rais Obama alipata muda wa kumjibu kijana Kule. Je marais wa Afrika wana muda wa kuzungumza na wananchi wao na kutoa mfano wa Obama kwa Afrika? Nini maoni yako?

Chanzo: bbcswahili.


Ukitaka jibu lililo sahihi, tumia mifano hai ukianza na rais wetu. Huyu kijana (Kikwete) toka achukue hii nchi alitoa ahadi kibao kwa kila Mtanzania kuwa na maisha mazuri, walio wengi wetu tulichekelea mpaka tukasusa kula kwa ajili ya furaha ya ahadi hewa. Binafsi, nilimwandikia barua kulalamika juu ya kumuhamisha wizara Dr. Magufili toka Ujezi miaka ya nyuma kwani ujenzi ulisimama kwa kukosa mwangalizi ama usimamizi mzuri. Ilikuwa ni miaka minne iliyopita, mpaka leo hii sijata jibu. Unataka kuniambia inachuku miaka minne kumjibu mwananchi, kwa kazi gani anayoifanya zaidi ya kutalii? Isitoshe angeweza hata kunijibu kwenye ndege wakati akipumzika kucheza karata/bao na washikaji zake, ila hakutaka. Hapa Afrika, viongozi wanafikiri wao ndo Mungu hawatakiwi kukosolewa kwa lolote lile.
 
kikwete labda ile chopa ya raisi iharibike ndio atapata muda wa kujibu barua kama hizi.............
 
Ukitaka jibu lililo sahihi, tumia mifano hai ukianza na rais wetu. Huyu kijana (Kikwete) toka achukue hii nchi alitoa ahadi kibao kwa kila Mtanzania kuwa na maisha mazuri, walio wengi wetu tulichekelea mpaka tukasusa kula kwa ajili ya furaha ya ahadi hewa. Binafsi, nilimwandikia barua kulalamika juu ya kumuhamisha wizara Dr. Magufili toka Ujezi miaka ya nyuma kwani ujenzi ulisimama kwa kukosa mwangalizi ama usimamizi mzuri. Ilikuwa ni miaka minne iliyopita, mpaka leo hii sijata jibu. Unataka kuniambia inachuku miaka minne kumjibu mwananchi, kwa kazi gani anayoifanya zaidi ya kutalii? Isitoshe angeweza hata kunijibu kwenye ndege wakati akipumzika kucheza karata/bao na washikaji zake, ila hakutaka. Hapa Afrika, viongozi wanafikiri wao ndo Mungu hawatakiwi kukosolewa kwa lolote lile.
Mkuu mbona wewe ndio ulipata majibu mazuri? Magufuli si alirudishwa Wizara ya Ujenzi baada ya Rais kuisoma barua yako na kukubaliana na maoni yako!
 
Yaani Kikwetee akujibu barua wewe? Hana muda huo bana. Ngoja nikupe mfano hai.

Kuna mlemavu mmoja aliwahi kutoka Arusha kwenda kumtafuta rais wake amuelezee jinsi maosha yalivyo magumu.
Basi jamaa akajiandaa na vinauli vya kuokoteza, hatimaye akafanikiwa kupata nauli ya kumfikisha Dar, na hatimaye akafanikiwa kufika Dar mpaka posta mpya akasukuma baiskeli yake hadi getini Ikulu. Akagonga, akiomba kuonana na rais wake.

Baada ya mkuu kuambiwa kuna mlemavu anataka kuonana nae, ndipo alipotoa amri ambayo ilimfanya yule mlemavu ajute kuchukua uamuzi wa aina ile.

Yaliyomkuta yule mlemavu ni kukamatwa, kula kichapo, kusekwa rumande na kufunguliwa kesi ya kusababisha/kuleta fujo Ikulu. Kilichomuokoa ni wanaharakati wachache ambao hawakukubaliana na upuuzi huo.

Huyo ndio rais wetu na response kwa wale wanataka kuonana nae, Je atatoa wapi muda wa kukujibu barua yako?
 
Mkuu mbona wewe ndio ulipata majibu mazuri? Magufuli si alirudishwa Wizara ya Ujenzi baada ya Rais kuisoma barua yako na kukubaliana na maoni yako!


Ni kweli lakini Magufuli alirudishwa lini? Wizara ya ujenzi ilidorora vibaya sana baada ya yeye kuondolewa gafla. Suala hapa ni kujibu barua ambayo yeye he never did answer up to now.
 
Yaani Kikwetee akujibu barua wewe? Hana muda huo bana. Ngoja nikupe mfano hai.

Kuna mlemavu mmoja aliwahi kutoka Arusha kwenda kumtafuta rais wake amuelezee jinsi maosha yalivyo magumu.
Basi jamaa akajiandaa na vinauli vya kuokoteza, hatimaye akafanikiwa kupata nauli ya kumfikisha Dar, na hatimaye akafanikiwa kufika Dar mpaka posta mpya akasukuma baiskeli yake hadi getini Ikulu. Akagonga, akiomba kuonana na rais wake.

Baada ya mkuu kuambiwa kuna mlemavu anataka kuonana nae, ndipo alipotoa amri ambayo ilimfanya yule mlemavu ajute kuchukua uamuzi wa aina ile.

Yaliyomkuta yule mlemavu ni kukamatwa, kula kichapo, kusekwa rumande na kufunguliwa kesi ya kusababisha/kuleta fujo Ikulu. Kilichomuokoa ni wanaharakati wachache ambao hawakukubaliana na upuuzi huo.

Huyo ndio rais wetu na response kwa wale wanataka kuonana nae, Je atatoa wapi muda wa kukujibu barua yako?


Yaani aliamuru kumpiga Kikwete, samahani Kiwete kisa alikwenda kumlalamikia juu ya ugumu wa maisha? Si ni yeye aliyetoa ahadi feki kuwa maisha bora kwa kil mtanzania sasa watu wakitaka kujua ukweli anawafukuza tena? Kweli rais tunaye.
 
Ni kweli lakini Magufuli alirudishwa lini? Wizara ya ujenzi ilidorora vibaya sana baada ya yeye kuondolewa gafla. Suala hapa ni kujibu barua ambayo yeye he never did answer up to now.

Obama alijibu barua iliyofikishwa kwake na mtu wa ikulu kama ilivyoelezwa hapo. Sasa kama jamaa alituma kwa njia y posta inakuwa ni vigumu kwa Rais kuipata. Huenda washauri wake waliipata wakamshauri.

Lakini mbona nasikia JK alikuwa akijibu sms!
 
ah wapi JK wala asingeipata hiyo barua ingechanwa na sekretari wake au maafisa usalama wake
ule mtindo wa karani kusoma barua ya boss wake upo sana Tanzania hata kusoma email za boss wake
akiona barua au email ambayo kwake haina maana hatampelekea boss wake.
 
waafrika wanajibu wadada tu lol

:biggrin1: ni kweli kabisaa...alafu wanavosema marekani wanasisitiza haki za binadamu na kupinga ukandamizaji..mbona hapa bongo hawafanyi lolote...au kwa vile wameahidiwa kupata mikataba ya gas na oil basi mengine wamefumba macho
 
CPA Kumbe wewe mkenya? Hiyo lafudhi... Mhh!...alikuja kufunza,....nyanyake! Au ndo BBC swahili ya Kenya
 
Last edited by a moderator:
Kikwete kawaita yanga ikulu, kawaita na kuongea nao madaktari, kawaita bongo fleva kina juma nature , na juzi juzi kamuita diamond . Bado watu walimsema sana rais. Sasa sijui mnataka rais afanyaje???????
 
Wabongo kwa kushadadia mambo ya kipuuzi hamjambo, yaani mbona hilo halikuhitaji hata headlines waganda wanamatatizo lukuki lakini sio uasi kama ingekuwa Kivu au somalia sawa.

Yaaani mtoto wa miaka 10 uganda aombe msaada wa kuondoa waasi ambao hawapo, Jose au Kony mbona kitambo yuko chaka kasepa. Mbona tunawashobokea sana wazungu jamani hata kwa mambo ya kipuuzi.
 
Kikwete kawaita yanga ikulu, kawaita na kuongea nao madaktari, kawaita bongo fleva kina juma nature , na juzi juzi kamuita diamond . Bado watu walimsema sana rais. Sasa sijui mnataka rais afanyaje???????
hao wote aliowaita ni wanachama hai wa mabwepande..believe me
 
Back
Top Bottom