Tunajenga Taifa lenye watu wa ajabu na madhara yake hayatakuwa na mwenyewe

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1583913874446.png

Tunajenga “Moral less, value less and ethical less political society”​

Tanatengeneza viongozi na jamii ambayo kwayo hakuna jambo lolote ambalo ni baya wala zuri na hakuna jambo linalokubalika au kutokukubalika.

Kwa taifa tunalojenga, uzuri au ubaya wa jambo haupo kwenye jambo lenyewe bali kwenye ‘Nani ni mnufakika na nani ni muathirika kwa uangalia usoni”. Kanuni inaayotumika kuamua ni rahisi lakini hatari sana. Kanuni hiyo ni ‘lolote ninalofanya mimi au linalofanyika kwa maslahi yangu ni sahihi na linakubalika na lolote analofanya mwingine au linalofanyika kwa maslahi ya mwingine si sahihi na halikubaliki’.

Kwa hiyo kama taifa tunashindwa kusema vitu 1,2,3 ni tatizo na havikubaliki bila kujali mfanyaji ni nani na mwathirika ni nani, na vitu 1,2,3 vinakubalika bila kujali mfanyaji ni nani na mwathirika ni nani.

Hali hiyo hupelekea kitu ambacho mtu anakipinga kwa mtu A tukio A akitetee kwa mtu B kwenye tukio hilo hilo au linalofana. Na hili ni kama vile amma hatulioni, au tunaliona lakini kila mtu anapuuza kana kwamba halipo, au ni jambo la kawaida.Lakini katika uhalisia wake ni moja ya mzizi wa matatizo makuu yanayotukabili na kama tutaendelea kuchukulia tabia hii kama jambo la kawaida, madhara yake yatakuwa serious Zaidi.

Kwa mfano, umevamiwa na vibaka, unalaani na unataka wachomwe moto, baadae mwanao anavamia na kuiba kwa jirani, unasema acha kijana aibe, kwani jirani hakujua wizi upo, kwa nini hakuweka walinzi? Yaani hatuoni kama tatizo ni kile kinachofanywa bali tunafikiri tatizo ni nani kafanya na nani kafanyiwa.

Aidha, katika mazingira hayo bado tunaamini tutamaliza tatizo la msingi, tunasahau kwamba wakati mmoja anaona ni tatizo na anazuia mwingine anafikiri ni sahihi na anahimiza kutokana na upande aliopo kwa wakati husika. Ni sawa na mlango ambao wakati mmoja akifungua mwingine anafunga na nyote mnaamini ipo siku huo mlango utafunguka.
 
... well said japo ungeunganisha kwenye thread moja ingekuwa bora zaidi. Actually summary ya ulichoandika ni "mkuki mtamu kwa nguruwe"; as simple as that.
 
Kabisa,kwa sasa uchochezi unategemea nani kafanya!Jambo lilelile likisemwa na fulani ni kosa na likisemwa na fulani ni halali!
... juzi Mangula kaugua ghafla and in less than a week ripoti ya Polisi imetoka tayari! Za akina Saa8, Lissu, Mawazo, Azory, Mwangosi, etc. etc. etc. mtazisikia tu! Kumbe binadamu wote sio sawa na wala hawastahili haki sawa kama tunavyoaminishwa.
 
... well said japo ungeunganisha kwenye thread moja ingekuwa bora zaidi. Actually summary ya ulichoandika ni "mkuki mtamu kwa nguruwe"; as simple as that.
Watu wanalalamika mada zinakuwa ndefu na wanapenda kusoma hoja fupi fupi.
 
Hali hiyo inatupelekea tunaacha kufikiria na kushughulika na matatizo ya msingi, bali kila mtu anafikiria namna ya kumtengenezea mwenzake tatizo. Mwishowe unakuta tunaachana kabisa na kushughulikia matatizo ya msingi na tuna shughulika na matatizo ambayo kimsingi hayapo, au kukazana kutengeneza matatizo bandia badala ya kushughulika na matatizo halisia ambayo tayari yapo.

Wakati huo huo tunaamini kwa mwenendo huo huo tutang'ara tu kama mataifa mengine ambayo yameng'ara duniani.Ni vyema tukafikiri Zaidi ni wapi tunataka kwenda na ili nini.
 
Kwa mfano linapotokea tatizo, badala ya ku focus tatizo hasa ni nini, chanzo na solution zinazowezekanika kisha kuchagua njia yenye manufaa zaidi; tunaanza kuulizana, muhanga ni CCM,CHADEMA au ACT? Je! msababishaji ni CHADEMA au CCM? Mwishowe hatushughuliki kabisa na tatizo la msingi zaidi ya kila mmoja kuishia kwenye level hiyo hapo ambayo haisaidii ku address tatizo la msingi kwa namna yoyote ile.

Ni kama vile kwetu vyama vya siasa vinatufanya tushindwe kufikiri katika utaratibu wa kawaida na hivyo kushindwa kujua lipi baya lipi jema, na ikiwa hivyo ndivyo, ni nini maana ya vyama vya siasa kwenye jamii yetu?
 
Tatizo watu wamesahau utaifa wanaleta uchama,mambo ya muhimu ya kitaifa wanaleta ushabiki kama wa Simba na yanga.na hii kitu ndio naona kabisa kitakuja kuleta mpasuko mwishoni tuje kubaguana sisi kwa sisi.tuweke utaifa kwanza pasipo angalia nani kasema kama jambo liko na manufaa ni kulichukua pasina kusema ni ccm au mpinzani kasema
 
Kwa kuwa haya yanatokea kwenye vyama vya siasa ambavyo ndivyo huzalisha viongozi ambao ndio hutunga sera na kufanya maamuzi mbali mbali; katika hatua ya juu kabisa itafika mahali tutakuwa na viongozi ambao kwao hakuna jema wala baya. Hakuna linalokubalika na lisilokubalika. Kitakachoamua lipi zuri lipi baya, ni muhusika kuangalia nani ni nani.

Katika hatua hiyo, kila atakayetunga sera atakuwa ha focus kwenye tatizo bali kwenye personalities, kila atakayefanya maamuzi atakuwa haangalii tatizo bali nani ni nani, kila atakayetunga sheria ataangalia watu badala ya kuangalia tatizo analotaka kutatua. Sasa fikiria ni nini kitakuwa kinafuata hapo? mahadhara ya mwenendo huu yatakuwa hayana mwenyewe.Ni bora kila mtu akajaribu kujiridhisha juu ya kila hatua anayoamua kuchukua au kutochukua na kufikiria matokeo yake katika hatua yake ya juu kabisa.
 
Huko tuendako hii nchi itakuja kuwa ya visasi sana,Leo ukiwa na power ukinitesa Mimi,kesho watoto wangu wakiwa na power lazima watalipiza kisasi kwa familia yako,na ndicho ninachokiona kiona ccm inatutengenezea
 
Tatizo watu wamesahau utaifa wanaleta uchama,mambo ya muhimu ya kitaifa wanaleta ushabiki kama wa Simba na yanga.na hii kitu ndio naona kabisa kitakuja kuleta mpasuko mwishoni tuje kubaguana sisi kwa sisi.tuweke utaifa kwanza pasipo angalia nani kasema kama jambo liko na manufaa ni kulichukua pasina kusema ni ccm au mpinzani kasema

Kama watu wataendelea kukaa madarakani bila ridhaa ya umma, suala la mgawanyiko halikwepeki. Hata itumike nguvu kiasi gani, lakini kitendo cha kuacha ukweli kutawala kisha zikatumika nguvu kutawala, hapo mgawanyiko haukwepeki.
 
Tufunge mjadala kwamba:Watanzania tuna unafiki mkubwa sana!!
Mtu yupo tayar kujisaliti, kijinyima au kujishusha kisa flan.Lakini haya yote shida ni 3 tu.
1UMASIKINI
2UJINGA
3MAGONJWA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
... juzi Mangula kaugua ghafla and in less than a week ripoti ya Polisi imetoka tayari! Za akina Saa8, Lissu, Mawazo, Azory, Mwangosi, etc. etc. etc. mtazisikia tu! Kumbe binadamu wote sio sawa na wala hawastahili haki sawa kama tunavyoaminishwa.
Alafu kuna mapung..ua...an kama kina Abuu Dharr marekani wanapokemea wanasema kwani ni nani kwettu!! Sisiemu imezalisha vilaza 100% Au anajiona yeyw yupo salama kwakuwa hana undugu na kina saa8, mawazo n the like.
 
View attachment 1383967
Tunajenga “Moral less, value less and ethical less political society”​

Tanatengeneza viongozi na jamii ambayo kwayo hakuna jambo lolote ambalo ni baya wala zuri na hakuna jambo linalokubalika au kutokukubalika.

Kwa taifa tunalojenga, uzuri au ubaya wa jambo haupo kwenye jambo lenyewe bali kwenye ‘Nani ni mnufakika na nani ni muathirika kwa uangalia usoni”. Kanuni inaayotumika kuamua ni rahisi lakini hatari sana. Kanuni hiyo ni ‘lolote ninalofanya mimi au linalofanyika kwa maslahi yangu ni sahihi na linakubalika na lolote analofanya mwingine au linalofanyika kwa maslahi ya mwingine si sahihi na halikubaliki’.

Kwa hiyo kama taifa tunashindwa kusema vitu 1,2,3 ni tatizo na havikubaliki bila kujali mfanyaji ni nani na mwathirika ni nani, na vitu 1,2,3 vinakubalika bila kujali mfanyaji ni nani na mwathirika ni nani.

Hali hiyo hupelekea kitu ambacho mtu anakipinga kwa mtu A tukio A akitetee kwa mtu B kwenye tukio hilo hilo au linalofana. Na hili ni kama vile amma hatulioni, au tunaliona lakini kila mtu anapuuza kana kwamba halipo, au ni jambo la kawaida.Lakini katika uhalisia wake ni moja ya mzizi wa matatizo makuu yanayotukabili na kama tutaendelea kuchukulia tabia hii kama jambo la kawaida, madhara yake yatakuwa serious Zaidi.

Kwa mfano, umevamiwa na vibaka, unalaani na unataka wachomwe moto, baadae mwanao anavamia na kuiba kwa jirani, unasema acha kijana aibe, kwani jirani hakujua wizi upo, kwa nini hakuweka walinzi? Yaani hatuoni kama tatizo ni kile kinachofanywa bali tunafikiri tatizo ni nani kafanya na nani kafanyiwa.

Aidha, katika mazingira hayo bado tunaamini tutamaliza tatizo la msingi, tunasahau kwamba wakati mmoja anaona ni tatizo na anazuia mwingine anafikiri ni sahihi na anahimiza kutokana na upande aliopo kwa wakati husika. Ni sawa na mlango ambao wakati mmoja akifungua mwingine anafunga na nyote mnaamini ipo siku huo mlango utafunguka.
MSHEMALIZAAA MICHANGO YA KUTOA VIONGOZI WENU KWANZA AMA MNAJAZA INZI JF
 
Tufunge mjadala kwamba:Watanzania tuna unafiki mkubwa sana!!
Mtu yupo tayar kujisaliti, kijinyima au kujishusha kisa flan.Lakini haya yote shida ni 3 tu.
1UMASIKINI
2UJINGA
3MAGONJWA

Sent using Jamii Forums mobile app
Lakini mkuu kuna watu wala si masikini ila wanayofanya yanasikitisha. Kuna watu wamesoma sana tu ila wanayofanya yanahuzunisha. Kuna watu ni wazima wa afya ila uzima huo wanaotumia kufanya mambo ambayo yana ukakasi mkubwa! Tunafanyaje sasa?
 
Back
Top Bottom