Tunajadili katiba tunasahau kanuni za bunge

Nikupateje

JF-Expert Member
Dec 22, 2009
1,334
988
Mjadala wa katiba mpya unaendelea na unapata waelewaji wengi kadiri siku zinavyokwenda.

Lakini kadiri unavyoendelea ndivyo unavyodizi kufunika mambo mengine ambayo pia ni ya msingi na yanapaswa kushugulikiwa.

Ukizikagua kanuni kanuni za bunge utaona tunapiga kelele kila siku kulalamika madaraka makubwa ya rais.

Lakini tunasahau kumbe hata spika ana madaraka makubwa vilevile. Mbunge anaweza kufukuzwa kikaoni na ata kufungiwa kama ilivyotokea ka Zitto Kabwe na kama Samwel Sitta wakati fulani alimtoa nje John Cheyo.

Lakini hakuna kifungu hata komoja kinachoeleza kwamba spika anaweza kuwajibishwa akivunja kanuni.

Mtakumbuka bunge hili la Anne Makinda yametikea makosa kadhaa moja kwa moja yakimhusu Spika.

Wakati wa kugombea unaibu spika tunakumbuka CC na CHADEMA waliweka wagomea. Yule tuliemuita mpambanaji wa ufisadi Engineer Rozi Manyanya alileta swali kwa mgombea wa CHADEMA akiuliza Chama chama chake kimesema kutomtambua rais sasa anawezaje kuongoza bunge?

Tundu Lissu aliinua mkono na kufafanua swali hilo si sehemu yake kwani hoja iliyop si ya uchaguzi wa rais bali ni uchaguzi wa naibu spika. Anne makinda badala ya kukiri au kukataa alirukia na kusema "Na wewe hivyohivyo Tundu Lissu unaingilia mawazo ya mwenzio".

KIla aliyetazama aliona spika kachemsha kwani hata hakutaja mwongozo kama nilivyomnukuu. Ndipo mgombea wa CHADEMA akalazimishwa kujibu swali.

Wakat analijibu alisema "pamoja na kutengua kanuni" na wala hakufika mbali Spika akarukia na kusema "ondoa hiyo kauli, nani kavunja kanuni, ina maana mimi spika nimevunja kanuni?".

Huu ni mfano wa spika kuwa katika hali ya kutowajibishwa. Ukweli kanuni ilivunjwa.

Mfano mwingine ni pale Sofia Simba alipoteuliwa kuwa mjumbe wa kamati ya SADEC wakati hakuhojiwa kama wengine. Akina Zitto walikuja na kusisitiza bunge linatakiwa lifuate kanuni lakini haikufua dafu.

Hii yote ni kwa sababu kanuni zimemuweka spika kama vile yuko juu ya sheria.

Naamini spika atapenda tuendelee hivihivi tumsahau upande huu.

Kumbe huku nako kunahitaji kushughulikiwa. Tunaweza kujidhani kanuni hazituhusu lakini ukiachilia mbali ukweli kwamba kila mmoja ni mbunge mtarajiwa, bado hata sasa uwezekano wa mbunge kunyanyaswa na spika huku spika akijua wazi hakuna litakalomtokea.

Mnaionaje hii.
 
katiba kwanza hiii ndio sheria mama hizo za bunge na za uchaguzi na nyinginezo zitabadilika aoutomatical
 
Unadhani katiba itagusa ubabe wa spika.

Kama katiba ambayo ni sheria mama itakuwa nzuri na yenye manufaa kwa watanganyika wote,basi hata hizi shria ndogo ndogo zitakuwa pia nzuri kwani hazipaswa kukingana na katiba ambayo ni sheria mama.
 
Hiyo ndio kazi tunawaachia wabunge wapya wapambane na spika kubadilisha sheria kandamizi za kijinga huko bungeni. Sisi huku nje tutapambana na hizi zilizo katika uwezo wetu (in our reach), KATIBA
 
Maafa Mengine ya CCM Tanzania Hayo. Kila Kona ya Nchi Wameharibu. Hata Bunge Lenyewe Linatakiwa Taratibu Zibadilishwe Kuleta Usawa na Haki ili Policies Zinazo Zungumziwa Ziwe Zinawakilisha Wananchi Wote Tanzania. Hatuwezi Kuwa na Vyama Vingi Tanzania Lakini CCM Ndio Waamuzi wa Kila Jambo. Maamuzi ya CCM na Historia Yao Si Tunaifahamu? Kinacho Shangaza Wengi Mpaka Sasa, Hakuna Kiongozi Yeyote wa Taifa Kutoka CCM Anaye Kuja Hadharani Kupigania Swala la Katiba au Taratibu za Bunge. Hivi Ni Kweli Viongozi wa CCM Wote Ni Vichwa Mbovu? au Wamefungwa na Mganga Gani? Hili Swala La Katiba na Taratibu za Bunge Vinazuia Maendeleo ya Nchi Yetu. Kweli CCM ni Binadamu wa Aina Yake. CCM Inatulutea Playbook ya Mugabe ZANU-PF na Kamwe Hatukubali.

"Katiba na Taratibu za Bunge Hazita Subiri 2015. Miezi Tu Imebaki...Tuwafukuze Wezi Ikulu na Kisha Bungeni"
 
Kama alivyosema Mtawala, katiba ndiyo sheria mama na hii inamgusa kila Mtanzania. Katiba inaitwa constitution na nikutoka katika katiba tunapata Regulations, By law n.k. Kwa mantiki hiyo udhaifu wa katiba unaweza kuwa extrapolated kwenye sheria na kanuni.
Tukumbuke kuwa udhaifu wa kanuni hauletwi na kanuni bali yule anyesimamia kanuni. Ni kanuni zile zile alizotumia Sitta ndizo anatumia Makinda. Tofauti ni kuwa Sitta alidhamiria kuliendesha bunge kwa kasi na viwango na kwahiyo alisimamia sheria na kanuni hata pale zilipowagusa CCM na Mafisadi. Bunge likawa kimbilio la wananchi. Kwa bahati mbaya Kanuni za CCM haziruhusu mambo yanayolijenga taifa bali kulinda maslahi ya kikundi cha watu wasiozidi 20 wanaolitafuna taifa. Sitta akatupwa nje.
Mama Makinda amewekwa pale na watu maalumu kwa lengo maalumu, si sahihi kumlaumu kwasababu anatekeleza matakwa ya mabosi wake kiutawala na kifedha. Udhaifu wake si udhaifu wa kanuni za bunge, ni udhaifu wa maslahi na kukosa moyo wa uzalendo. Ni bora awe spika kwa miaka 5 kuliko kuwaudhi mafisadi kwa siku moja. Historia itatueleza huko tuendako. Ni bahati mbaya lakini si wananchi walivaa kofia na sare za kijani?
 
Back
Top Bottom