Tunaishukuru TBC kuonesha Kombe la Dunia 2022, lakini kulikuwa na mapungufu mengi

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,305
12,600
TBC ni chombo umma wa watanzania kinachoendeshwa kwa Kodi za watanzania wote. Ninamshukuru waziri mwenye dhamana ya michezo, waziri wa habari na mawasiliano na Mkurugenzi wa TBC kwa kuwafikiria matajiri wao (walipa Kodi) kuwaletea matangazo ya moja kwa moja kutoka Qatar, ahsanteni sana kwa kuwaza jambo hili. Labda shukrani nyingi zaidi ziende kwa Rais Dr. Samia kwa kuruhusu hili lifanyike kwa kutumia Kodi za wananchi, umeupiga mwingi kwakweli.

Lakini shughuli nzima ilikuwa na mapungufu yafuatayo.
1. Kukosekana kwa baadhi ya mechi. TBC haikuonyesha mechi zote, kama vile ilikuwa inatufanyia hisani TU watanzania kwa kutuchagulia mechi ipi tuangalie na ipi tusiangalie.

2. Kuchanganya channel ya matangazo ya taifa na michezo pamoja. Tulitegemea TBC ingekuwa na channel ya sports ili kuepuka kuchanganya matukio ya kitaifa na serikali na michezo.

3. Wachambuzi wa mpira hawakuwa na ubora. Wanaborongaboronga TU wakati hii ndiyo TV ambayo ingetakiwa na Quality wachambuzi.

4. Watangazaji wa mpira. Hawakuwa na mvuto zaidi ya kujua kiarabu TU. Hawavutii kuwasikiliza, unatamani waache kusimulia ili tuangalie TU wenyewe.

Ushauri: Sisi ndio wenye TBC, hivyo matangazo ya mpira lazima yawe ALL or NONE, sio vuguvugu kama vile. Bora muache kabisa ili watu wajioange kuliko vile. Chukueni wachambuzi ikiwezekana kutoka media nyingine binafsi. Kulikuwa na ugumu gani kutumia channel ya TBC2 au nyingine kwa michezo TU?

Ahsante ni TBC
 
Mbona watangazaji walikuwa wazuri tu au mlitaka watangazeje kwani labda mapungufu makubwa yalikuwa ni kuonyesha mechi chache kwa hapo kweli walituudhi sana.
 
Kabla Kombe la Dunia halijaanza walitangaza mapema kabisa kuwa wataonyesha mechi 28 sasa kuwapa lawama kwa kutoonyesha mechi zote huo ni ulalamishi.

Kwa upande wa wachambuzi na watangazaji mi sijaona tatizo naona wako poa tu.
 
4. Watangazaji wa mpira. Hawakuwa na mvuto zaidi ya kujua kiarabu TU. Hawavutii kuwasikiliza, unatamani waache kusimulia ili tuangalie TU wenyewe.
Utasikia Meeesssssiii.... yababaaa yababaaa
yaani watangazaji ni dhahiri wanaonesha mahaba makubwa kwa andunje
 
Kuonyesha mechi 24 ni sawa na kumpa fulana tu mtu asiyekuwa na nguo. Yaani matako yako nje lakini mabega na tumbo limefichwa,
 
Kulaumu watangazaji bila kufafanua mapungufu yao hio ni chuki,nadhan ulitarajia mechi itangazwe na your favorite presenters kitu ambacho hakiwezekani,kwa sisi tuliofatilia michuano mwanzo mwisho kupitia tbc vijana walifanya kazi yao vizuri otherwise ni mapungufu tu kidogo ya kibinadam
 
TBC ni chombo umma wa watanzania kinachoendeshwa kwa Kodi za watanzania wote. Ninamshukuru waziri mwenye dhamana ya michezo, waziri wa habari na mawasiliano na Mkurugenzi wa TBC kwa kuwafikiria matajiri wao (walipa Kodi) kuwaletea matangazo ya moja kwa moja kutoka Qatar, ahsanteni sana kwa kuwaza jambo hili. Labda shukrani nyingi zaidi ziende kwa Rais Dr. Samia kwa kuruhusu hili lifanyike kwa kutumia Kodi za wananchi, umeupiga mwingi kwakweli.

Lakini shughuli nzima ilikuwa na mapungufu yafuatayo.
1. Kukosekana kwa baadhi ya mechi. TBC haikuonyesha mechi zote, kama vile ilikuwa inatufanyia hisani TU watanzania kwa kutuchagulia mechi ipi tuangalie na ipi tusiangalie.

2. Kuchanganya channel ya matangazo ya taifa na michezo pamoja. Tulitegemea TBC ingekuwa na channel ya sports ili kuepuka kuchanganya matukio ya kitaifa na serikali na michezo.

3. Wachambuzi wa mpira hawakuwa na ubora. Wanaborongaboronga TU wakati hii ndiyo TV ambayo ingetakiwa na Quality wachambuzi.

4. Watangazaji wa mpira. Hawakuwa na mvuto zaidi ya kujua kiarabu TU. Hawavutii kuwasikiliza, unatamani waache kusimulia ili tuangalie TU wenyewe.

Ushauri: Sisi ndio wenye TBC, hivyo matangazo ya mpira lazima yawe ALL or NONE, sio vuguvugu kama vile. Bora muache kabisa ili watu wajioange kuliko vile. Chukueni wachambuzi ikiwezekana kutoka media nyingine binafsi. Kulikuwa na ugumu gani kutumia channel ya TBC2 au nyingine kwa michezo TU?

Ahsante ni TBC
Hapo kwenye namba 3 Sasa..
Hasa Yule Mzee wa kuitwa Liki Abdallah yaani mtupu kweli kweli,ati mechi ya Argentina na Croatia ile penalty ya Julian Alvarez anakwambia ati ingekuwa ligi ya uingereza isingekuwa penalt !! Utasema Sheria ya penalty kick ya uingereza (FA) Ipo tofauti na sehemu nyingine duniani,!! Yaani aibu niliona Mimi,Yule Mzee wack sana, halafu ati anakwambia Alvarez alijipeleka kuwa fouled !
Ama kweli wajinga ndio waliwao
 
Kabla Kombe la Dunia halijaanza walitangaza mapema kabisa kuwa wataonyesha mechi 28 sasa kuwapa lawama kwa kutoonyesha mechi zote huo ni ulalamishi.

Kwa upande wa wachambuzi na watangazaji mi sijaona tatizo naona wako poa tu.
Walikueleza sababu? Walikuomba ushauri?
 
Sema inshu ya kuonyesha mechi 28 kati ya 64 ilikua changamoto asee
Wamesahau kuwa kombe la dunia nibsehemu ambayo watoto na vijana wanapotengenezea ndoto zao, ndipo wanapowapata role model wao kwenye mpira wa miguu. Ni darasa kwa waamuzi na makocha wetu.
 
Hapo kwenye namba 3 Sasa..
Hasa Yule Mzee wa kuitwa Liki Abdallah yaani mtupu kweli kweli,ati mechi ya Argentina na Croatia ile penalty ya Julian Alvarez anakwambia ati ingekuwa ligi ya uingereza isingekuwa penalt !! Utasema Sheria ya penalty kick ya uingereza (FA) Ipo tofauti na sehemu nyingine duniani,!! Yaani aibu niliona Mimi,Yule Mzee wack sana, halafu ati anakwambia Alvarez alijipeleka kuwa fouled !
Ama kweli wajinga ndio waliwao
Alianza kuangalia TV tangu enzi hizo tv Iko kwa sheikh yahaya TU hapa dar
 
Back
Top Bottom