naggy
Member
- Apr 27, 2011
- 97
- 152
Nilisikitishwa sana na udhaifu wa M/kiti wa bunge wa kikao cha jana jioni jinsi alivyokuwa mshabiki wa vituko bungeni hadi kupelekea kushindwa kuongoza kikao. Leo hali hii imejitokeza tena kwa M/kiti wa leo mh. Jenister Muhagama. Tatizo langu kwa viongozi hawa ni wao kushabikia malumbano yasiyo ya kujenga ya wabunge wa upinzani na wale wa chama tawala. Kimsingi, Spika au m/kiti hapaswi kuegamia upande wowote ki itikadi. Lakini hawa wameshindwa kulisimamia hilo na ndo maana siku hizi kila siku wanajitetea kwa waandishi wa habari kuwa wao wanatenda haki ili tu wasihukumiwe vibaya na umma wa watanzani. Najiuliza bila kupata majibu. Hivi huyu Mwigulu Nchemba (mb) anatumwa na chama? Kwa nini katika kuchangia kwake anakwenda kinyume na kanuni za bunge na spika anayekuwepo anamwachia? Kwa mfano katika kikao cha leo, hoja iliyoyoko mezani ni ofisi ya rais utumishi wa umma,utawala bora na maadili. Mbunge anapoinuka ni lazima achangie hotuba ya waziri ambayo ndo hoja yenyewe, sio kuchangia hoja ya mchangiaji mwingine. Sasa mbunge anapoinuka na kuchangia hoja ya upinzani ambayo ni ki mantiki ni sawa na mchango wa mbunge mwingine inawachanganya wasikilizaji. Mtoa maoni ya upinzani hana muda wa kujibu hoja za wabunge kwa sababu kanuni haziruhusu. Nchemba kwa tabia yake hiyo anawalazimisha wabunge wa upinzani wajibu hizo hoja anazoaitoa ili asipotoshe umma, na hapa ndiyo vurugu mechi huanza. Jenister Muhagama alipaswa kulizuia hili na kumuongoza mbunge ajikite kwenye hoja kama alivyokuja kumwelekeza mwishoni. Ameruhusu marumbano yasiyo na tija yaliyopoteza muda wa bunge. Kwa hali hii ni lazima kiti kilaumiwe. Maoni ya kambi ya upinzani yatajibiwa na waziri husika wakati wa majumuisho. Kama chama kinamuona Nchemba ni hodari wa kuzima hoja za wapinzani basi wamshauri rais ampe wizara awe rais. Watanzania tunahitaji malumbano ya hoja zenye kujenga sio hizo za kinanchemba ambazo zinatuchefua na kutufanya tusione maana ya kusikiliza majadiliano ya bunge.