Tunahitaji suluhisho la mafuriko mto msimbazi na siyo kujikita kwenye usafiri Jangwani tu

ego

JF-Expert Member
Apr 10, 2013
1,620
1,407
kwa mda mrefu jiji la Dar hukumbwa na mafuriko katika mto msimbazi yanayopelekea nyumba kadhaa kando kando ya mto msimbazi kuzingirwa na maji huku baadhi ya barabara kama magomeni eneo la jangwani kutopitika.

inashangaza kuona serikali inapanga kujenga daraja jangwani kama ndiyo suluhisho la jambo hili kwa kutatua shida ya usafiri tu na kutelekeza matatizo mengine.

Dar es salaam siyo ya wenye magari tu kusema waliojenga mabondeni shauri yao watafute pa kwenda bali tunahitaji kuondoa mafuriko mto msimbazi ikiwezekana kwa kuujengea mto msimbazi ili udongo usimomonyoke na kuziba mitaro na pia magugu na miti maji vinavyoota kuzuia maji kusafiri kwa kasi.

pia tunaweza kujenga mabwawa ya kutunza maji haya ili yasiganganie kukimbilia baharini kwa wakati mmoja.

tunahitaji kufikiri zaidi ya kuona magari yanayokwama na kuona nyumba zinazozingirwa na maji kama ni matatizo tuliyoyatengeneza wenyewe kwa kutokuwaelekeza hawa ni wapi sehemu sahihi ya kujenga kupitia mipango miji na hivyo ni wajibu wetu sote kutafuta suluhisho la mafuriko
 
Yaani nimesikitika sana kusikia wanataka kujenga daraja la juu kuanzia Magomeni mpaka fire.. Hayo ni matumizi mabaya ya fedha zetu watanzania.

Suluhisho la matatizo ya mto Msimbazi sio pale jangwani tu barabarani, matatizo mengi ya mto Msimbazi yana anzia katika mabonde yake huko kuanzia katika chanzo chake kilichopo kule Kisarawe.

Mfano rahisi ni project ya kujenga kingo za mto Ng'ombe unaopita Tandale imesaidia sana kuondoa mafuriko na kulinda barabara zilizopo maeneo ya mto huo.

Kiujumla ujenzi wa Daraja la Jangwani ni upigaji wa fedha zetu.. Mradi wa mto Msimbazi unatakiwa ushirikishe maeneo korofi yote na sio kuishia kujenga Daraja la kuvushia magari tu!
 
Nan ataweza kututetea mkuu SASHA Kageuka VASCO DA GAMA Hajui matatizo ya wananchi yeye hana muda was kutafakar maumivu ya wannchi Zaid ya kuongeza tozo kwa hawa hawa anaowaita wanyonge

Nadhan sababu hakuchaguliwa na sisi aliteuliwa na Rais aliyepita hajui maumivu yetu

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu hii sio rocket science,tulioishi wakati nchi ina heshima na adabu ule mto haujawahi kuleta mafuriko ,mafuriko yameletwa na sisi wenyewe na kuanzia vunja nyumba zote zilizojengwa kule mikokoni ,eneo ambalo mto unaingia baharini.
 
Nani aliwalazimisha kujenga mtoni? Mliamua wenyewe kwa hiari yenu, sasa mmeuziba mto haupitishi maji unavyopaswa, halafu mnakuja hapa kulalamika. Hameni mabondeni mkajenge nchi kavu. Mnataka pesa zetu za kodi zitumike kuhalalisha uzembe wenu wa kufikiri na kufanya maamuzi sahihi? Huo ni ufujaji wa pesa za walipa kodi.
 
Nani aliwalazimisha kujenga mtoni? Mliamua wenyewe kwa hiari yenu, sasa mmeuziba mto haupitishi maji unavyopaswa, halafu mnakuja hapa kulalamika. Hameni mabondeni mkajenge nchi kavu. Mnataka pesa zetu za kodi zitumike kuhalalisha uzembe wenu wa kufikiri na kufanya maamuzi sahihi? Huo ni ufujaji wa pesa za walipa kodi.
kuna haja gani ya kuwa na wizara ya ardhi na maendeleo ya makazi kama kila mtu ataamua mwenyewe pa kujenga wapi na awajibike kwa maamuzi yake.

kama serikali yenyewe yenye wataalamu na fedha ya kutosha imejenga kituo cha magari ya mwendo kasi ndani ya jangwani je mwananchi asiyejua chochote na fedha ya kudunduliza unategemea atafanya nini? Wizara ya ardhi inalo jukumu la kuwaonyesha watu mahali sahihi pa makazi, viwanda na ni maeneo gani yaachwe wazi. hawafanyi lolote hawa
 
Back
Top Bottom