NtakuwaSikuchukui
Member
- Feb 9, 2012
- 26
- 10
Kama kuongea jamani tumesema sana juu ya safari za rais huyu,ni kweli safari nyingi ni wazi ni kukwepa majukumu yake ya kushughulikia kero za watanzani, kwa kuogopa kugombana nao waliomweka madarakani.Safari nyingi zisizo na msingi ni upotevu mkubwa wa kodi za watanzania,inafika mahali ndege inachukuliwa kama boda boda,umelala umeamka unasema unaomba ufikishwe maramoja Uk au Marekani wakati tangu ameingia madarakani amezidi kuwaweka kwenye umaskini mkubwa watanzania hadi sasa navyo ongea hali ni mbaya ya uchumi.
Sina mengi ila ni waombe wana JF na hasa sana wale wabunge na viongozi wengine kuna haja ya kuwa na sheria itakayosimamia safari zote za rais au waziri wa mambo ya nje ili kuokoa upotevu usio wa lazima wa kodi za watanzania.Sheria hiyo ibainishe:
MNAONAJE WANA JF?
Sina mengi ila ni waombe wana JF na hasa sana wale wabunge na viongozi wengine kuna haja ya kuwa na sheria itakayosimamia safari zote za rais au waziri wa mambo ya nje ili kuokoa upotevu usio wa lazima wa kodi za watanzania.Sheria hiyo ibainishe:
- Safari za msingi kwa viongozi kupanda ndege kulingana na vigezo mbalimbali vitakavyowekwa kama vile hali ya uchumi,matatizo ya ndani ya nchi yanaitaji utatuzi wa haraka n.k
- Idadi maalumu ya watu watakaopata zali kupanda ndege kulingana na majukumu yao husika kwa taifa,ambayo itazingatia hali halisi ya uchumi na mambo mengine.Hapa sio kuwapa watu zawadi ya kupanda ndege kiolelaolela kama ilivyo sasa hata kama hausiki.
- Rais hanabudi kugeuza haraka sana tena sana pale matatizo yanapotokea nchini na hakuna mtu wa kutatua ila yeye rais.mfano mgomo wa madaktari,rais alikuwa bubu na kuchelewa kutatua tatizo ilo.
- TUENDELEZE MENGINE HAPA.............
MNAONAJE WANA JF?