Tunahitaji Mabadiliko ya Sheria zinazokandamiza Haki za Mashoga Tanzania

Interest

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
3,434
7,055
Nakumbuka Rais Kikwete alipoulizwa msimamo wa Tanzania kuhusu Mashoga, alizungumza kidiplomasia kwamba Watanzania bado hawajawa tayari kuhusiana na mambo hayo.

Naye aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Benard Membe alisema wazi kwamba Watanzania hawataki ushoga na waliwakatalia wazungu walipojaribu kuipenyeza ajenda hiyo kinyemela..Sasa leo tunapoambiwa tulisaini mikataba ya kimataifa kutambua Haki za Binadamu ikiwemo ushoga. Nani alisaini? Kikwete? Mbona hatukujulishwa?

Tamko la Wizara ya Mambo ya Ndani limejikuta indirectly linathibitisha kwamba Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazokubaliana na suala la ushoga kama haki nyingine za binadamu. Yaani kama ni siri basi imebumburuka!

Huu ni ukombozi kwa wahusika wa vitendo hivyo. Kwa muda mrefu wamekuwa wakiishi kwa kunyanyapaliwa na kuonekana hawafai lakini kumbe serikali imesaini mikataba na jumuiya za kimataisha katika kuwatambua na kuwapatia haki zao.

Nashauri kuanzia sasa;

1. Zile NGOS zilizokuwa zikiwapatia washiriki wa mapenzi ya jinsia moja vilainishi na elimu kuhusu njia salama za kushiriki ngono bila madhara sasa zisibughudhiwe tena..

2. Polisi wawakamate na kuwafikisha mahakamani wale wote watakowafanyia dhihaka na kuwabughudhi mashoga

3. Sheria zinazokataza mapenzi ya jinsia moja zifutwe na adhabu ziondolewe

4. Jamii ielemishwe umuhimu wa kutambua haki zote za binadamu na kuziheshimu

5. Serikali iwe inawashirikisha wananchi kwa uwazi kuhusiana na mikataba mikubwa inayoingia na Jumuiya za Kimataifa ili kuepusha migogoro isiyo na ulazima.

Najua hili jambo ni zito na lina utata mkubwa hata huko juu kwa wakubwa hivi sasa. Naamini JPM amefura kwa hasira, lakini atafanyaje? Itambidi akubali tu, ndivyo mambo yalivyo!

Njia mbadala tuliyonayo ni kupitia upya mikataba ya kimataifa na kubadili mambo tusiyoyakubali kama taifa. Lakini tujiandae na consequences maana sisi ni taifa nyonge mbele ya wababe.

Swali muhimu ni; Je, tuko tayari kwa lipi?
 
Kwa kweli.. Mtoto wa former president atakuwa alijua suala la hii mikataba..
Vipi kuhusu sheria zetu zinazocondemn?
Mimi sio mwanasheria ila huenda mikataba hii tuliosaini inaweza kuwa na nguvu zaidi katika mahakama zetu pale kunapotokea mgongano wa kisheria baina ya sheria zetu na zile za kimataifa kulingana na mikataba tulioingia.
 
Mimi sio mwanasheria ila huenda mikataba hii tuliosaini inaweza kuwa na nguvu zaidi katika mahakama zetu pale kunapotokea mgongano wa kisheria baina ya sheria zetu na zile za kimataifa kulingana na mikataba tuliosaini.
Hakuna kitu kama hicho! Sheria za nchi kwanza na sheria mama ni Katiba!
 
Kuna kitu nakiona siyo kizuri hapa,nisingependa kuwaona watu ninaowaamini wakitetea huu upuuzi. Ushoga haukubaliki Tanzania.
 
Mimi sio mwanasheria ila huenda mikataba hii tuliosaini inaweza kuwa na nguvu zaidi katika mahakama zetu pale kunapotokea mgongano wa kisheria baina ya sheria zetu na zile za kimataifa kulingana na mikataba tuliosaini.
Sheria yoyote ikitiliwa sign ya makubaliano UN, hua ni wajibu iwekwe kwenye katiba ya Nchi husika.

Mfano wa mambo tulivyosign katika makubaliano UN ya haki za binaadam, ziliwekwa kwenye katiba ya nchi yetu.

PART 3 YA KATIBA.

Article 12) Equality of Human Beings. - Usawa wa kila binaadamu.

Article 13) Equality before the Law. - Usawa mbele ya sheria kwa kila mtu.

Article 14) The Right to Life. - Haki ya kuishi (Na ndio maana hukumu ya kifo Tanzania haitelelezwi, kwa kuhofia kuvunja haki hii.

Article 15) The Right to Personal Freedom. - Haki ya uhuru kwa kila mtu.

CHAPTER 6 YA KATIBA.

UASISI WA HAKI ZA BINAADAM NA UTAWALA BORA

Article 129) Uundwaji wa Tume/Commission ya Haki Za Binaadam.

Article 130) Kazi za hio Tume/Commission na Procedure za kupeleka malalamiko.

Article 131) Nguvu ya hio Tume/Commission na procedure za utendaji kazi.

NB Inawezekana wameiweka miongoni mwa sheria ndogo za hio CHAPTER 6 inayohusu haki za binaadamu ya Katiba yetu, ila wakagoma kutambua/kuweka vifungu vya sheria katika MARRIAGE ACT/SHERIA YA NDOA, kutambua ndoa za JINSIA MOJA.


Ushoga haipo wazi. Serikali wangetoa "go ahead" kwa wananchi kutoa hukumu kwa mashoga chini kwa chini, kama Uganda, kazi ingekua rahisi, wangetengwa na kufukuzwa mitaani, ila wameya kanyaga kutafutia kiki.
 
Kuna wanawake makahaba walikamatwa Dodoma hivi karibuni. Waliwekwa rumande kwa kosa la kujiuza miili yao. Na kamanda wa polisi alikuwa mkali kweli akiwaonyesha mbele ya waandishi wa habari huku akisema hawahitaji wanawake wanaojiuza Dodoma. Sasa kama mashoga watatambuliwa kisheria, hawa wanawake wanaojiuza tena kwa kufuata maumbile si watakuwa wameonewa! Nafikiri kabla ya kushauri mabadiliko kama haya ni vema kutafakari kwanza. Kuruhusu ushoga kutafungulia mlango kwa mengine yote kuruhusiwa pia. Maana huwezi ruhusu mashoga wafanye mambo yao halafu wanawake wanaojiuza kwa wanaume ukawakamata.
 
Sheria yoyote ikitiliwa sign ya makubaliano UN, hua ni wajibu iwekwe kwenye katiba ya Nchi husika.

Mfano wa mambo tulivyosign katika makubaliano UN ya haki za binaadam, ziliwekwa kwenye katiba ya nchi yetu.

Article 12) Equality of Human Beings. - Usawa wa kila binaadamu.

Article 13) Equality before the Law. - Usawa mbele ya sheria kwa kila mtu.

Article 14) The Right to Life. - Haki ya kuishi (Na ndio maana hukumu ya kifo Tanzania haitelelezwi, kwa kuhofia kuvunja haki hii.

Article 15) The Right to Personal Freedom. - Haki ya uhuru kwa kila mtu.


Ila hio ya ushoga haipo, ila hii barua ya leo imeleta sintofahamu.
Hii ya ushoga teknikali inaingia kote hapo. Simply because they are humans and such are human rights..
Upo?!
 
Back
Top Bottom