Tunaelekea shimoni jamani naomba mnielewe

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
Kama wapo viongozi wanaonunua viongozi wengine hilo ni tatizo kubwa kweli kweli, lakini cha kujiuliza wanafanya hivyo ili iweje katika hatua ya juu kabisa? na katika mazingira kama hayo , expectation yao ni ili mwisho iwe nini?

Haya, Hao wanaohongwa ni wapinzani (ndio mbadala). Wanahongwa milioni mbili wanaachana na uongozi. Mara wanatamani kuhongwa ajira za ualimu (sifa wanazo za kuwa waalimu by competence lakini wanafikiri wanatakiwa wapate by favoritism). Mbona viongozi hawa wanakuwa na "Low expectation" kiasi hiki jamani?

Haya ukirudi kwa upande mwingine; sisi sote tumeweka matumaini yetu yote kwa makundi tajwa hapo juu. Sasa fikiria ni nini hatma yetu?

Wakuu; Tatizo letu watanzania ni kufikiri. Tuna tatizo kubwa sana kwenye namna tunavyofikiri na nilazima tulielewe hili na kulikubali kwanza. Tuna "Very low expectation & vision". Wanaokuwa viongozi kwenye vyama na mwishowe kwenye nchi wanatokana na sisi, kwa hiyo vile walivyo, ni reflection ya tulivyo.

Enyi watu mnaoamini mna uelewa mzuri, mna dhamira njema, ni waadilifu, mna maono mapana, wazalendo na mmejaa utu ndani yenu; Acheni kukaa kimya bila kusema wala kufanya chochote na kuacha mambo yawe yatakavyokuwa kama vile hamuhusiki wala hamuwajibiki kwa vyovyote vile. Tutaelekea shimoni kweli nawaambieni. Tushirikianeni kwanza kuboresha namna tunavyofikiri na kuwasaidia wengine kufanya hivyo hivyo ili kutoka miongoni mwetu, tuweze kuwa na viongozi wenye vision pana ambao watakuwa ni msaada zaidi kwetu na kwa nchi yetu baadae.

Suala la chama gani kinashinda uchaguzi halina maana ikiwa watu ni wale wale na wote wana matatizo yale yale na mawazo na expectations za namna ile ile.

Naombeni mnielewe tafadhali!
 
Tunakuelewa. Lakini, hatuelekei shimoni. Kupokea au kutoa rushwa ni udhaifu wa watu binafsi. Si wa nchi wala wananchi wake.
Angekuwa mmoja sawa ila wilaya? any way hilo la rushwa ni moja tu ila yapo matukio mengi ukiyatafakari utakubaliana na mimi kwamba Tatizo letu liko kwenye namna tunavyofikiri na expectations na tatizo hilo liko kwenye jamii changanyikeni. Sasa kwa kuwa viongozi wote bila kujali chama hutokea huko, hayo ndio matokeo yake.
 
Picha inayopatikana katika sakata hili ni kwamba chadema kina wanachama wa ajabu sana ambao wanaweza kununulika kiwepesi

Hii ina maana kwamba nassari na lema wamejiaibisha wenyewe kwa kuonesha ubovu wa wanachama wao. Nassari na lema.wametuonesha wazi kuwa asilimia kubwa ya viongozi wao ni wapokea rushwa na wepesi kushawishika.

Madiwani walionunuliwa wanatoa taswira ya.aina ya viongozi waliopo chadema.

Kama unaviongozi ambao wanaweza kununulika basi ujue chama chako kimejengwa na misingi ya kupenda rushwa na pia si chama kinachopaswa kuongoza watu.

Lema na nassari wanadhani wanamuumbua DC na Rais kumbe wanajiumbue wenyewe kwa kutuonesha aina ya wanachama walionao.

Chadema mnakiua chama chenu wenyewe kwa kutuonesha aina ya viongozi mlionao
 
ccm imeamua liwalo na liwe

Kwamba kwa gharama yoyote lazima washinde viti vyote vya udiwani vitakavyo rudiwa Arusha, kuwa uchaguzi ujao dogo Nasari ajue hata kama akishinda, ubunge byebye, kuwa Lema Arusha atashinda kwasababu mgombea wa chama kijani hakubaliki ndani ya chama chake.

Kuwa mbona hata ule uchaguzi wa vitongoji chama vidole viwili walishinda lakini mshindi wa chama kijani alitangazwa lakini chama cha vidole viwili hawakufanya chochote.

Kwamba wale madiwani walio ondoka chama vidole kwenda chama kijani waliahidiwa ahadi lukuki kutokana na order kutoka kwa wakubwa juu.
 
Kama wapo viongozi wanaonunua viongozi wengine hilo ni tatizo kubwa kweli kweli, lakini cha kujiuliza wanafanya hivyo ili iweje katika hatua ya juu kabisa? na katika mazingira kama hayo , expectation yao ni ili mwisho iwe nini?

Haya, Hao wanaohongwa ni wapinzani (ndio mbadala). Wanahongwa milioni mbili wanaachana na uongozi. Mara wanatamani kuhongwa ajira za ualimu (sifa wanazo za kuwa waalimu by competence lakini wanafikiri wanatakiwa wapate by favoritism). Mbona viongozi hawa wanakuwa na "Low expectation" kiasi hiki jamani?

Haya ukirudi kwa upande mwingine; sisi sote tumeweka matumaini yetu yote kwa makundi tajwa hapo juu. Sasa fikiria ni nini hatma yetu?

Wakuu; Tatizo letu watanzania ni kufikiri. Tuna tatizo kubwa sana kwenye namna tunavyofikiri na nilazima tulielewe hili na kulikubali kwanza. Tuna "Very low expectation & vision". Wanaokuwa viongozi kwenye vyama na mwishowe kwenye nchi wanatokana na sisi, kwa hiyo vile walivyo, ni reflection ya tulivyo.

Enyi watu mnaoamini mna uelewa mzuri, mna dhamira njema, ni waadilifu, mna maono mapana, wazalendo na mmejaa utu ndani yenu; Acheni kukaa kimya bila kusema wala kufanya chochote na kuacha mambo yawe yatakavyokuwa kama vile hamuhusiki wala hamuwajibiki kwa vyovyote vile. Tutaelekea shimoni kweli nawaambieni. Tushirikianeni kwanza kuboresha namna tunavyofikiri na kuwasaidia wengine kufanya hivyo hivyo ili kutoka miongoni mwetu, tuweze kuwa na viongozi wenye vision pana ambao watakuwa ni msaada zaidi kwetu na kwa nchi yetu baadae.

Suala la chama gani kinashinda uchaguzi halina maana ikiwa watu ni wale wale na wote wana matatizo yale yale na mawazo na expectations za namna ile ile.

Naombeni mnielewe tafadhali!
Rushwa inapelekea uchaguzi kurudiwa na kulitia taifa hasara ya mamilioni wahusika wote wasimamishwe kazi kupisha uchunguzi
 
Picha inayopatikana katika sakata hili ni kwamba chadema kina wanachama wa ajabu sana ambao wanaweza kununulika kiwepesi

Hii ina maana kwamba nassari na lema wamejiaibisha wenyewe kwa kuonesha ubovu wa wanachama wao. Nassari na lema.wametuonesha wazi kuwa asilimia kubwa ya viongozi wao ni wapokea rushwa na wepesi kushawishika.

Madiwani walionunuliwa wanatoa taswira ya.aina ya viongozi waliopo chadema.

Kama unaviongozi ambao wanaweza kununulika basi ujue chama chako kimejengwa na misingi ya kupenda rushwa na pia si chama kinachopaswa kuongoza watu.

Lema na nassari wanadhani wanamuumbua DC na Rais kumbe wanajiumbue wenyewe kwa kutuonesha aina ya wanachama walionao.

Chadema mnakiua chama chenu wenyewe kwa kutuonesha aina ya viongozi mlionao
Sikubaliani nawe sana Mkuu, hii imeonesha ni kwa kiasi gani watanzania tuna expect low. Ukumbuke hao wote walioshiriki mchakato huo wamekuwepo hapo walipo by chance! Kwa hiyo ni sample ya general population .
 

Shamba la bibi!
Ile kauli "Ikulu ni mahala patakatifu... Ikulu sio pango la walanguzi na wala rushwa ..." imesahaulika!
 
Tunakuelewa. Lakini, hatuelekei shimoni. Kupokea au kutoa rushwa ni udhaifu wa watu binafsi. Si wa nchi wala wananchi wake.
Anapokuwa mmoja ni udhaifu wake,lakini wakifika watano linakuwa ni tatizo letu. Nionavyo tunafanana kama maembe,atoaye rushwa anawalakini lakini apokeaye naye ni hatari zaidi. Huyu anaweza kuuza hata nchi kama bei ikitimia.
 
Kwa kuongezea, kuna shida kubwa ya namna tunayo-define mafanikio (success). Kwa tulio wengi, mafanikio ni kuwa na majumba, magari, viwanja vingi etc. Yaani kama wewe ni engineer, tutasema umefanikiwa si kwa kujenga mabarabara na majumba imara etc., bali kwa mali unazomiliki.

Kama wewe ni daktari, tutasema umefanikiwa si kwa kufanikiwa kupata jawabu ya tatizo sugu linalomsumbua mgonjwa, bali kwa idadi ya nyumba na magari unayomiliki. Na kwamba sherehe ya harusi ya kijana wako iligharimu fedha nyingi kiasi gani.

Kama wewe ni mhadhiri, tutasema umefanikiwa kwa kupima utajiri ulionao, si kwa umahiri wako katika kufundisha na tafiti unazofanya zinavyosaidia kuyaelewa matatizo yetu kwa upana na kuyapatia ufumbuzi.

Kwangu mimi, hili ndilo tatizo mama na msingi wake ni poverty mentality. Kwa kuwa wengi wetu tumekulia kwenye umaskini, tunapopata mafasi ya kula, tuna tabia ya kukwapua matonge makubwa makubwa kwa kuwa tuna wasiwasi chakula kilichopo hakitamtosha kila mmoja wetu.
 
Picha inayopatikana katika sakata hili ni kwamba chadema kina wanachama wa ajabu sana ambao wanaweza kununulika kiwepesi

Hii ina maana kwamba nassari na lema wamejiaibisha wenyewe kwa kuonesha ubovu wa wanachama wao. Nassari na lema.wametuonesha wazi kuwa asilimia kubwa ya viongozi wao ni wapokea rushwa na wepesi kushawishika.

Madiwani walionunuliwa wanatoa taswira ya.aina ya viongozi waliopo chadema.

Kama unaviongozi ambao wanaweza kununulika basi ujue chama chako kimejengwa na misingi ya kupenda rushwa na pia si chama kinachopaswa kuongoza watu.

Lema na nassari wanadhani wanamuumbua DC na Rais kumbe wanajiumbue wenyewe kwa kutuonesha aina ya wanachama walionao.

Chadema mnakiua chama chenu wenyewe kwa kutuonesha aina ya viongozi mlionao
Si tu wananunulika bali hata hapo walipo wamepanunua.
 
Kama wapo viongozi wanaonunua viongozi wengine hilo ni tatizo kubwa kweli kweli, lakini cha kujiuliza wanafanya hivyo ili iweje katika hatua ya juu kabisa? na katika mazingira kama hayo , expectation yao ni ili mwisho iwe nini?

Haya, Hao wanaohongwa ni wapinzani (ndio mbadala). Wanahongwa milioni mbili wanaachana na uongozi. Mara wanatamani kuhongwa ajira za ualimu (sifa wanazo za kuwa waalimu by competence lakini wanafikiri wanatakiwa wapate by favoritism). Mbona viongozi hawa wanakuwa na "Low expectation" kiasi hiki jamani?

Haya ukirudi kwa upande mwingine; sisi sote tumeweka matumaini yetu yote kwa makundi tajwa hapo juu. Sasa fikiria ni nini hatma yetu?

Wakuu; Tatizo letu watanzania ni kufikiri. Tuna tatizo kubwa sana kwenye namna tunavyofikiri na nilazima tulielewe hili na kulikubali kwanza. Tuna "Very low expectation & vision". Wanaokuwa viongozi kwenye vyama na mwishowe kwenye nchi wanatokana na sisi, kwa hiyo vile walivyo, ni reflection ya tulivyo.

Enyi watu mnaoamini mna uelewa mzuri, mna dhamira njema, ni waadilifu, mna maono mapana, wazalendo na mmejaa utu ndani yenu; Acheni kukaa kimya bila kusema wala kufanya chochote na kuacha mambo yawe yatakavyokuwa kama vile hamuhusiki wala hamuwajibiki kwa vyovyote vile. Tutaelekea shimoni kweli nawaambieni. Tushirikianeni kwanza kuboresha namna tunavyofikiri na kuwasaidia wengine kufanya hivyo hivyo ili kutoka miongoni mwetu, tuweze kuwa na viongozi wenye vision pana ambao watakuwa ni msaada zaidi kwetu na kwa nchi yetu baadae.

Suala la chama gani kinashinda uchaguzi halina maana ikiwa watu ni wale wale na wote wana matatizo yale yale na mawazo na expectations za namna ile ile.

Naombeni mnielewe tafadhali!
Tumekuelewa Ila naomba nawe uelewe pia ni Chama kongwe Cha kinyani a. k. a Makinikia ndio kinaelekea shimoni Kama kondoo, maana hakuna namna inabidi kife tuu
 
Rushwa inapelekea uchaguzi kurudiwa na kulitia taifa hasara ya mamilioni wahusika wote wasimamishwe kazi kupisha uchunguzi
Usijadili sana madhara ya malaria halafu ukasisitiza kuwa inaweza sababisha kifo. Jadili kwa nini malaria na kama ipo namna ya kuzuia malaria isitokee na njia hiyo iwe ya kuaminika. Vinginevyo mjadala hauwezi kuwa na tija sana maana tutajadili aliekufa na malaria leo kesho atakufa mwingine tutajadili tena hivyo hivyo hadi nasi tutakufa.
 
Back
Top Bottom